Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Sixtus Raphael Mapunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia majukumu au kazi za Kamati hizi mbili zilizoko mbele yetu. Awali ya yote, nichukue fursa hii kuwashukuru sana Wenyeviti wa Kamati zote mbili kwa jinsi walivyotuwasilishia kwa ufasaha sana kazi zao; lakini pili, kutuelezea changamoto na namna bora ya kuondokana na zile changamoto ili Bunge lako Tukufu lipate fursa nzuri ya kuishauri Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mnajili wa kuchangia hoja yangu ya leo, itoshe tu kuongea mambo mawili ambayo yanatokana na mjadala wetu wa leo; lakini vile vile katika kuwekana sawa ili kama kuna jambo linapotosha humu ndani, wote tulielewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mijadala imeendelea huku ndani ikielezea separation of power, good governance, uhuru wa hii mihimili mitatu na majukumu ya hii mihimili mitatu. Sisi kama Bunge tunapata fursa ya kufanya kazi zetu kwa Ibara ya 62, 63 na kuendelea ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unaposema mgawanyo wa kimajukumu wa hii mihimili mitatu, kama msemaji aliyepita, Mheshimiwa Salome Makamba aliposema separations of power halafu akaiacha hewani; separation of power haimaanishi hii mihimili mitatu ifanye kazi kwa kujitegemea, ndiyo maana kuna kitu kinaongezeka. Separation of power, checks and balance ikimaanisha, the three pillars should work independently, lakini katika kufanya kazi kule pamoja, inategemeana. Ndiyo maana kunakuwa na checks and balance.

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda kidogo kwa manufaa ya watu ambao hawakuwahi kumsoma Montesquieu na Jean-Jacques Rousseau hebu tuwasaidie kidogo waweze kujua. Huu msingi wa separation of power, unatokana na maandikio aliyowahi kuyaandika Baron De Montesquieu, huyu ni mwanafalsafa wa Kifaransa kwenye kitabu chake cha The Spirit of Law cha mwaka 1748. Katika kuelezea alisema tunapaswa kuwa na mfumo ambao kila organ inajitegemea ili kuepusha fusions of power kwenda kwa entity moja. Maana yake alikuwa anapinga kipindi kile mifumo ya aristocracy, alikuwa anapinga mifumo ya ki-monarchy, alikuwa anapinga mifumo ya autocracy. Sasa katika kuweka hivi ndio sisi hapa tunakuwa tunatunga sheria, sasa nikamshangaa sana ukiunganisha hoja ya Mheshimiwa Salome na ya Mheshimiwa Kubenea zinakuja kukutana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kubenea anasema sisi tutunge sheria, tukishatunga sheria, hatuwezi tena sisi tukatafsiri sheria, hatuwezi sisi tena tuka-enforce law. Tuna maeneo yetu sisi lazima tuishie, ndio maana kuna msemo wa Kilatini unaosimamia hilo unasema trias politica principle ukimaanisha (The separation of power, checks and balances). Hii mifumo lazima ifanye kazi kwa kutegemeana, huwezi ukawa na Mahakama isiyokuwa na aliyeanzisha shtaka yaani Executive katika maana ya Polisi. Huwezi ukawa na mtafsiri wa sheria bila kuwa na mtu aliyetunga sheria. Hawa watu wote wanafanya kazi kwa kushirikiana. Kikubwa zaidi kinachonishangaza, sikutegemea kama hii ingekuwa kweli ajenda ya kujadiliwa kwenye nyumba hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Siku ya Wanasheria. Mwanasheria amemwalika Polisi, Mwanasheria kwa hiari yake mwenyewe ameamua kumwalika mgeni rasmi awe Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya au mtu mwingine yeyote, tatizo liko wapi? Hivi kweli ukiweka red carpet pale ukawaweka Majaji, ukamweka na Mkuu wa Mkoa, maana yake kweli Mkuu wa Mkoa ni mkubwa kuliko Jaji au Jaji Mkuu kuliko Mkuu wa Mkoa? Ile ni context, ile ni shughuli kama shughuli nyingine ina taratibu zake haiingilii mamlaka ya Jaji kama Jaji na wala haiingilii mamlaka ya Mkuu wa Mkoa kama Mkuu wa Mkoa.

T A A R I F A

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilichotaka kusema hapa kwa kuanza hii mifano ya nyuma, hii mihimili mitatu inafanya kazi kwa kutegemeana sana. Bunge lako tukufu lisiwe sehemu ya kufarakanisha kwa kuweka chuki, nani mkubwa, nani mdogo, hoja ambazo hazitusaidii, ni vyema tujielekeze kwenye kuifanya hii mihimili ifanye kazi zake ufasaha, Wenyeviti wa Kamati wameelezea hapa changamoto zao, tuwasaidie kwenye kutatua changamoto ili kazi zao ziwe nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, naomba niongee kidogo kwenye mobile court. Mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Katiba na Sheria na Mheshimiwa Kubenea ni Mjumbe mwenzangu, wote tulikuwa kwenye kikao, sielewi amefanya kwa makusudi kwa kutaka kupotosha au hajui maana ya mobile court. Ukisoma Ripoti ya UNDP kuhusu Mahakama zinazotembea, ripoti iliyofanyia kazi Sierra Leone, Democratic Republic of Congo na Somalia inaeleza mobile court au Kiswahili (Mahakama inayotembea). Mobile Courts are defined as the formal courts that conduct proceedings in location other than their home Offices, usually in remote areas where no justice service are available.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa anachotaka kuongelea ni kwamba, mobile courts si lile gari, mobile court ni kwamba zile huduma zinatoka Mahakamani tulivyozoea kuziona, zinaenda sehemu nyingine, zinaweza zikawa kwenye bajaji, zikawafikisha Mahakimu na timu wakafanya kazi zao kule au wakatumia mfumo mwingine wowote wa kufika kule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama mnakumbuka scenario kama hii iliwahi kutokea kipindi cha genocide Rwanda, walikuwa na court zao zilikuwa zinaitwa Gacaca ambao watu walikuwa wanatoka wanakwenda maeneo ambapo watu hawajapata huduma na kwa sababu Mahakama zilikuwa zina msongamano sana wa watu na cell zilikuwa zimejaa, wakalazimika kutafuta mechanism ya kutatua matatizo. Mobile courts labda kwa lugha tunaweza tu tukasema, kuna hizi mobile banks mnaziona eeh, au mobile clinic haimaanishi kuwa lile gari, unaweza ukatumia chombo chochote…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante kwa mchango mzuri, kengele ya pili, Mheshimiwa Mlinga.

MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.