Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kunipa nafasi hii. Nitaongea kiungwana sana katika hoja zangu nitaziwasilisha na nakusudia kuzungumzia mambo mawili tu. Zanzibar ilipata uhuru tarehe 10 Disemba, 1963 lakini baada ya kupata Uhuru wananchi wa Zanzibar wakaona haitoshi…

T A A R I F A

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea. Zanzibar ilipata Uhuru tarehe 10 Disemba, 1963 ikafanya Mapinduzi tarehe 12 Januari, 1964. Nazungumzia Uhuru, independence and revolution are two different things. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yako mataifa ambayo wakati wanatawaliwa na Wakoloni walifanya mambo makubwa ya kuwaletea maendeleo ya kujenga barabara, miundombinu ya viwanja vya ndege kama vile South Africa na Angola lakini wananchi wa nchi hizo wakaona haitoshi kwa sababu hawakuwa huru. Kwa hiyo, kwa kuwa Mheshimiwa Profesa Kabudi yupo na yeye ni mtaalamu wa historia na sheria anajua hili kwamba kitu kinachoitwa uhuru ni muhimu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kabudi wakati anafundisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, tulikuwa tunafuatilia sana hotuba zake nzuri, alikuwa anatufundisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulivyo pamoja na umuhimu wa Katiba Mpya. Mwenyezi Mungu amejalia sasa ndiyo umefungwa kengele, wewe ndiyo Waziri wa Katiba na Sheria wa nchi hii, ule mchakato wa Katiba Mpya umekwama wapi Mheshimiwa Profesa Kabudi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, miongoni mwa ma- champion wa nchi hii wa kuhakikisha kwamba nchi inapata uhuru ni wewe. Mheshimiwa Profesa Kabudi utaandika historia kubwa sana ikiwa yale uliyokuwa unayasema, unayapigania wakati uko nje na sasa wewe ndiyo Waziri wa Katiba na Sheria ukiweza kuyatekeleza utaacha historia kubwa sana kwenye nchi hii. Vinginevyo the vice versa is true kwamba kumbe ulichokuwa unakisema haukiamini kama utashindwa kutelekeleza ukitoka kwenye nafasi yako bila kuwa na Katiba Mpya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni jambo ambalo nilikuwa nataka niseme kwa sababu namuona Mheshimiwa Profesa Kabudi yupo hapa ili ajue kwamba ana dhima hiyo ya kuhakisha nchi yetu inapata Katiba Mpya. (Makofi)

T A A R I F A

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee kwa sababu siyo kila taarifa unaweza ukaijibu.

Mheshimiwa mwenyekiti, ukisoma taarifa ya Kamati ya Katiba na Sheria, ukurasa wa 39 - 40 inazungumzia juu ya uwepo wa Mfuko wa Taifa wa Vijana ambao pia nimemsikia vizuri Makamu Mwenyekiti wa Kamati hii akisema kwamba 2016/2017 ulitengewa shilingi bilioni 1 na 2017/2018 wakapewa shilingi bilioni 2. Mimi bado si muhenga, bado nipo kwenye kundi la vijana lakini Mfuko huu siujui. Mheshimiwa Mhagama hizi fedha mnapeleka wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mapendekezo ya Kamati nayaunga mkono kwamba inatakiwa kwenda kufanya ufuatiliaji juu ya fedha za vijana zilipopelekwa. Nasema hivyo kwa sababu moja Mheshimiwa Mhagama, kuna Mfuko wa Uwezeshaji wa Rais na unajulikana na upo nchi nzima, hata ukija Lindi pale ofisi zao zipo. Huu Mfuko wa Vijana ulio chini ya Waziri Mkuu, mbona hatuufahamu?

T A A R I F A

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimtoe wasiwasi, Halmashuri yetu ina Wabunge wawili, mimi na Mheshimiwa Nape. Wewe muulize tu, sijawahi kukosa kuhudhuria kikao chochote cha Baraza la Madiwani, hata vikao Kamati za Fedha, nikiwa Dodoma nawahi kwenda Lindi. Kwa hiyo, hatuna wasiwasi, tunahudhuria.

MWENYEKITI: Hata kipindi cha korosho?

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Ndiyo, hata kipindi cha korosho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachokisema ni kwamba ukifika Lindi leo ukimuuliza kijana Mfuko wa Uwezeshaji wa Rais unajulikana. Mimi sijaongea from nowhere, hiki ndicho kilichoandikwa na Kamati kwamba hizi fedha Kamati inaomba kwenda kuvifuatilia hivyo vikundi vilivyopewa fedha. Sasa mimi kuunga mkono hoja ya Kamati inakuwa kosa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachosema ni kwamba Kamati yenyewe wameweka wasiwasi kwamba kuna umuhimu wa kufuatilia. Mimi naunga mkono Mheshimiwa Mchengerwa fuatilieni kwa sababu wanasema hapa kuna SACCOS zimekopeshwa, mimi Mbunge kutoka…

T A A R I F A

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni muungwana, nimelelewa kiungwana na naheshimu sana watu wote, nakushukuru sana. (Makofi)