Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote, naomba nikupongeze wewe Spika wetu, kwa kutuongoza vizuri, lakini pia nizipongeze Kamati zote za Bunge zilizowasilisha taarifa zao nzuri sana. Vile vile niwapongeze Manaibu wangu wawili ambao kwa kweli wametoa ufafanuzi mpana, japo kwa muda mfupi sana.

Mheshimiwa Spika, yangu ni machache tu kwa ajili ya kuelezea kwa ujumla. Kwanza naomba nikuhakikishie wazi kwamba, Kamati ya TAMISEMI ambayo tunafanya nayo sisi Ofisini kwetu, imekuwa msaada mkubwa sana kutupa maelekezo muhimu kwa ajili ya Taifa letu. Nataka tuweke hizi rekodi vizuri kwa sababu leo hii unaona ni mashahidi karibuni wajumbe wote hapa wakisimama, wanazungumzia vituo vya afya, wanazungumzia hospitali za Wilaya, wanazungumzia barabara na wanazungumzia elimu. Hii yote japo inawezekana kuna upungufu wa hapa na pale, lakini ukifanya tathmini ya huko tulikotoka na tulipo hivi sasa ni vitu viwili tofauti. Kwa hiyo naishukuru sana Kamati kwa ushauri wake, mkubwa sana. Kamati hii kwa kweli imeweza kufanya mambo makubwa sana na ripoti yao tunaishukuru sana na naomba niseme wazi kwamba wametusaidia sana kuhakikisha Wizara hii inakwenda vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna mambo mbalimbali ya kiujumla, ambayo sisi kwa upande wetu tunaomba tuyachukue kwa ajili ya kwenda kuyaboresha zaidi na hasa katika suala zima la bajeti, japokuwa tunafahamu mgao kama Naibu wangu alivyosema hapa, mgao ni kiduchu na napenda Wabunge wafahamu kwamba mtandao wa barabara ambao TARURA inahudumia ni wastani wa kilomita 127,000, kwa hiyo ni changamoto kubwa. Hata hivyo, sisi kama Serikali tutaendelea kuangalia jinsi gani tutafanya na hasa team yangu sasa hivi, kupitia Mtendaji Mkuu wa TARURA, niliwalekeza kwamba waone jinsi gani watafanya licha ya hizi fedha tunazopata katika Mfuko wa Barabara lakini wafanya resource mobilization kutoka maeneo mengine. Hivi sasa tuko katika negotiation na wenzetu wa World Bank kuangalia jinsi gani tutafanya kuiwezesha TARURA iweze kufanya kazi vizuri.

Mheshimiwa Spika, maeneo mengine ni kwa ujumla, tumesikia changamoto mbalimbali kwamba wakati mwingine fedha kutoka maeneo mengine zinakuwa na upungufu hasa katika kuimarisha sekta ya afya na hasa katika miundombinu. Naomba niseme kwamba tumelichukua hili na ndio maana katika maelekezo yetu, tunaenda kuangalia jinsi gani tutafanya, lengo kubwa ni kwamba miundombinu iendelee kujengwa vizuri.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, naomba niwashukuru sana Wabunge; katika haya mapinduzi makubwa, Wabunge wamefanya kazi kubwa sana katika maeneo mbalimbali. Katika ujenzi wa vituo vya afya, tunaona jinsi gani Wabunge wameamua kujipambanua wenyewe kushiriki vya kutosha, hili lazima hansard iweze kunukuu vizuri, kwamba Wabunge wa Bunge hili, wameweza kudiriki kufanya kazi kubwa sana. Nina imani katika ujenzi wa hospitali za wilaya ambao tumeuanza na tunaendelea nao hivi sasa, hospitali 67, lakini mwaka huu wa fedha tena tunaendelea na hospitali 27 kama Naibu wangu alivyosema, naamini tutafika vizuri.

Mheshimiwa Spika, na hata hivyo nafahamu kuna hospitali zipo, lakini hali yake ni mbaya, kwa sababu hata hapa nikisimama nikisema pale Kongwa kwa Spika wangu, hospitali yake ya Wilaya bado tia maji, tia maji. Kwa hiyo ni maeneo ambayo niseme kwamba, japokuwa wengine wanazo hospitali za wilaya, lazima twende tukaziangalie jinsi gani tutazifanya ziweze kutoa huduma vizuri zaidi. Hili ndiyo jambo ambalo tunaenda kufanya mwaka huu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba nikutoe mashaka kwamba, kuna maeneo mbalimbali tutayapa kipaumbele kwa lengo kubwa la kuona jinsi gani wananchi wetu, wanapata huduma vizuri.

Mheshimiwa Spika, pia kulikuwa na hoja ya Mbunge wangu, Mbunge wa Tanga nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo lile tumeshalifanyia kazi na barua imeshakwenda kwake kupitia kwa Mkurugenzi, lakini tumemkopi, kama hajaipata, basi tutawasiliana baadaye, lakini kila kitu kiko sawsawa kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni, aondoe hofu katika jambo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema haya, naomba niseme kwamba naunga mkono hoja za Kamati hizi zote ambazo zimewasilishwa vizuri sana na Wenyeviti wa Kamati. Ahsante sana.