Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Mgeni Jadi Kadika

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi. Nitajikita kwenye Wizara ya Afya hususani Bima ya Afya (NHIF). Kwa kweli kila mtu anahitaji kuwa na afya nyema, Taifa lililokuwa halina afya basi halina maendeleo wala halizalishi uchumi wala hatutazaana kwa haraka, naam! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, taarifa ya Wizara ya Afya kuhusu bima wanasema mpaka sasa hivi wanaotumia bima ni 34% tu. Hicho ni kiasi kidogo, bado Serikali haijajipanga kutoa afya kwa wote. Watu wengi hawana bima ya afya na tuna maradhi mengi yanatusumbua kama vile kansa, kisukari na maradhi mengine. Kwa hiyo, Serikali ifanye kila jitihada kutumia bima ya afya na wale waliokuwa hawajajiunga wajiunge. Wizara itoe elimu na ihamasishe ili watu wote wajiunge kwenye bima ya afya ili wapate matibabu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilipata fursa ya kwenda Rwanda ili kuona Bima ya Afya inavyofanya kazi ni tofauti wanavyofanya hapa kwetu. Kule tajiri, maskini wote wanapata fursa sawa za kutibiwa. Wao kule wanatibiwa kwa mfumo wa daraja, tajiri anatibiwa kwa daraja lake, mwenye kipato kikubwa anatibiwa kwa daraja lake na watu wa kati na wa chini wana madaraja yao na wale waliokuwa na hali zao ni duni kabisa basi wanatibiwa bure wakiwamo hao maskini, watoto chini ya miaka mitano, walemavu pamoja na wajawazito. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sisemi kwamba kwa nchi yetu wajawazito watibiwe bure, watibiwe kwa daraja, wale masikini kabisa ambao hawana hata hela ya kupanda daladala basi watibiwe bure. Tulikaa na Wizara ya Afya na wakasema watafanya mazungumzo ili kuleta Muswada hapa Bungeni tuweze kutunga sheria ya watu wote wapate fursa sawa ya kupata matibabu. Naiomba Serikali iharakishe kuleta Muswada huo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nizungumzie sasa masuala ya UKIMWI. Katika Mkoa huu wa Dodoma kuna asilimia kubwa ya maambukizi, kwanza ilikuwa 2.3% mpaka sasa hivi waathirika wamepanda imekuwa 5%. Je, Serikali inasemaje kuhusu Mkoa wa Dodoma? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sisi kama viongozi hapa Bima ya Afya wanatibu Mbunge na mweza wake na watoto wanne. Hata hivyo, kuna Wabunge wengine humu hawana wenza, hana mke na mwingine hana mume, kwa nini asitumie fursa hii kutibu wazazi wake? (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)