Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi jioni hii nichangie kuhusu mawasilisho ya hizi Kamati tatu. Jambo la kwanza, napenda nimshukuru Mwenyenzi Mungu kwa kutuwezesha jioni hii kuwepo mahali hapa kwani bila yeye sisi hatuwezi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jioni ya leo, napenda kuchangia mada zifuatazo. Suala la kwanza ni kuhusu uhaba wa vyumba vya madarasa. Hivi karibuni yalitoka matokeo ya darasa la saba hali iliyopekelea kuonekana ufaulu umekuwa mkubwa ambao hauendani na sambamba na vyumba vya madarasa. Hali hii ilipelekea watoto wengi kukosa vyumba madarasa na hatimaye wengine wakaanza kusoma wengine wamechelewa kuanza kusoma. Hali hii inakatisha tamaa wazazi hata na watoto wenyewe kwa sababu wanaona wenzao wameanza kusoma wengine hawajaanza kusoma. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niombe Serikali ili kuweza kumaliza hili tatizo ni vyema basi wafikie mahali pa kutumia takwimu kutoka kwenye Halmashauri zetu hususani takwimu ambazo ni maoteo ya watu wanaomaliza shuleni. Wakiweza kutumia hizi takwimu za maoteo watajua upungufu upo kiasi gani na mahitaji kiasi, watakapojua hivyo wataweza kuwasadia kama ni wadau wa elimu, wazazi, walezi ili kujumuika ku-cover ule upungufu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala lingine nataka niongelee kuhusu utitiri wa kodi uliokithiri katika Halmshauri zetu. Ni ukweli usiopingika kwamba uhai wa Halmashauri yoyote unategemea makusanyo ya kodi lakini kodi hizi kwa sasa baada ya Serikali Kuu kuchukua vyanzo vingi vya mapato kutoka kwenye Halmashauri zetu, Halmashauri zimebakia hazina kitu hivyo zimebuni njia mbalimbali za kupata kodi. Matokeo yake kumekuwa kuna msururu wa kodi mkubwa sana ambapo wananchi maskini hawezi kulipa. Matokeo yake wanatengeza njia za kusababisha kukwepa kodi au kutokulipa kodi bila shuruti. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niiombe Serikali iweze kutengeneza mazingira rafiki au elimu itolewe kwa hao wananchi ili waweze kulipa kodi bila shuruti kwa sababu tumeshuhudia, tumesikiliza kwenye taarifa ya habari tumeona Singida kule mauaji yametokeo, raia ameuwawa kwa risasi lakini raia huyu chanzo chake tumeambiwa alikwepa kodi. Kwa hiyo, niiombe Serikali ihakikishe kunakuwa na mazingira rafiki ya ulipaji wa kodi lakini pia na hawa watu wanaokusanya kodi wawe ni marafiki kwa walipa kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala lingine napenda kuzungumzia ukatili wa kijinsia. Ukatili wa kijinsia sasa hivi umekuwa mkubwa kupita kiasi ambapo wanafunzi wetu wanabakwa, wanalawitiwa na wanafanyiwa vitendo hivi na watu tu wenye akili zao timamu lakini hata huko shuleni wanafunzi kwa wanafunzi wanalawitiana. Kwa hiyo, niiombe sasa Wizara ya Elimu na TAMISEMI tuangalie tunamalizaje suala hili, kujenga mabweni mfano ya Ihungo Sekondari, yale majengo yakijengwa vizuri wanafunzi wataepuka kufanya vitendo vya ubakaji na kulawitiana. Nishauri tena wazazi tusipeleke shule watoto wenye umri mdogo kwa sababu ndio wanaoathirika kwa kuharibiwa na kaka zao. (Makofi)

Suala lingine ni upandaji madaraja kwa walimu. Walimu kwa sasa wamekosa morale ya kufanya kazi...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)