Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa dakika tano. Kwanza napongeza jitihada nyingi za Serikali ambazo inazifanya kwenye maeneo mbalimbali na kwa namna ambavyo Mawaziri wamejitahidi kufanya kazi kwenye hizi report zao.

Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Rais kwa kuwajali wakulima na wafugaji kwa kupunguza maeneo ya hifadhi ili wakulima wetu na wafugaji wapate maeneo na mahali pa kukaa salama bila ugomvi kwenye maeneo yao.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili nimshukuru Rais kwa kutoa vitambulisho kwa sababu, wajasiriamali wetu sasa wameanza kutambulika na mwisho wa siku watakua, watakuwa ni watu ambao wana uwezo wa kutambulika na watakuwa wakubwa na watakuwa na uwezo wa kukopesheka hapo mbele.

Mheshimiwa Spika, lakini jambo la tatu kuna jambo ambalo nimeliona na Wabunge wengi hawajasema, Rais ameweza kufanya kazi kubwa ya kusaidia kupata matrekta NBC imetoa matrekta, mkulima analipa milioni mbili down payment na leo wakulima wengi wameweza kusambaziwa matrekta nchini.

Mheshimiwa Spika, kwake kuna matrekta 89 yameingia, Wabunge wenzangu mpigieni Makofi Mheshimiwa Spika wetu. Kwa Mheshimiwa Nkamia yameshaingia matrekta 52, kwangu Kiteto yameshaingia matrekta 105. Kwa hiyo, Mheshimiwa Rais ameshafanya kazi kubwa kwa wakulima wetu kwa kuwatambua ili wakapate kufanya kazi kwenye maeneo yao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hili suala la TARURA linatupa shida kidogo. Siku za nyuma Madiwani wetu na baraza walikuwa na uwezo wa ku-coordinate zile barabara na kuona wapi pana daraja na wapi pana shida. Sasa hili suala la TARURA kutoleta taarifa kwenye Baraza la Madiwani tunashindwa ku- coordinate na ku-monitor hizi barabara, hata kwa kujua gharama. Hili suala litaendelea kuharibu barabara nyingi, suala la hizi barabara ambazo unakuta wameleta pesa za dharura kwa ajili ya kutengeneza maeneo korofi, huwezi kujua ni kiasi gani, huwezi kujua wanatengeneza wapi, huwezi kudhibiti angalau na kujua kwamba, kilichoingia ni kipi na kilichotoka ni kipi ili kuwabana watendaji wakandarasi kwenye maeneo yetu.

Mheshimiwa Spika, sasa naomba kushauri. TARURA, TAMISEMI iweze kutusaidia kuhakikisha kwamba, hawa watu wa TARURA wawe wanaripoti kwenye Baraza, watoe ripoti pesa zilizoingia, viwango vya barabara vinavyojengwa kwa wakati huo, pesa za dharura na kila kitu chote ule mchanganuo upate halafu na sisi Baraza la Madiwani tutoe ripoti na ile ripoti iwe inakuja mpaka mkoani, mkoani iweze kuja kwenye Taifa kwa mazingira ya kila wilaya kuweza ku- monitor barabara zilivyo na uharibifu wake.

Mheshimiwa Spika, jambo lingine; watendaji wa vijiji na kata mimi napata mshangao. Utumishi wa nchi hii unafanana kama Hati Miliki ya Ndoa ya Kikatoliki kwamba, mpaka ufe au mwenzako afe hamuwezi kuachana. Hii ni shida kubwa unakwenda mahali kijiji kimechanga Sh.2,700,000/=. Juzi nimepigiwa simu hapa, wananchi wanahitaji kupauwa jengo lao, Mtendaji wa Kijiji amechukua pesa, amekwenda amenunua mizigo yake amechakachua, amerudi hapa, haitoshi, hakuna kikao, hakuna kamati, hakuna nini, wanamuuliza anasema hakuna, amekuwa mbabe. Ukienda naye sambamba ni kwamba, mbele wanasema sasa mtumishi ukitaka kumhamisha wanakwambia awe na cheque mkononi, cheque mkononi, unafanyaje?

Mheshimiwa Spika, ukiondoka anakaa hivyo, keshokutwa mchango mwingine, wananchi wanaacha kuchangia maendeleo yao. Lazima TAMISEMI iamue mtumishi mbadhirifu level ya kijiji aidha apewe adhabu ya kuondolewa kazini tuajiri wengine ndio maana tuna wasomi wako mtaani. Tuamue, hii inaweza ku-discipline nchi hii, otherwise ni kwamba, tutaendelea kuwa na debate, Mkurugenzi hawezi ku-manage hawa watu wote, hata akim-manage anamhamisha anakompeleka si kuna Watanzania walewale, si kuna kijiji kilekile, si kuna kata ileile, atachangisha ataharibu. Sasa hii contract ya mtumishi wa Serikali ya Tanzania ambaye hawezi kumeguka akaachwa, eti formular sijui mpaka uajiriwe, ukaulizwe, mupeane adhabu, barua za onyo, hatutafika na wananchi chini wanaumia.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naombe kushukuru jitihada nyingi za Serikali zinazofanyika. Napongeza na kuunga mkono hoja. Ahsante sana.