Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kusema machache katika taarifa hizi za Kamati mbili zilizowasilishwa hapa Bungeni leo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimejifunza jambo leo na hili ni kuonesha ni kwa kiasi gani sasa kazi nzuri zinazofanywa na Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, zinakubalika pande zote, kwamba hata wale ambao hapo awali walikuwa wakibeza yale makubwa anayoyafanya sasa unaona wameanza kuyakubali kwa njia nyingine tofauti. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijakuja hapa nilipitia Hansard za Bunge kuona maoni ya Wabunge wakati wa mjadala wa IPTL ulipokuwa ukijadiliwa hapa Bunge. Yalikuwa ni maoni ya Kambi ya Upinzani kwamba tuachane na miradi midogo midogo ya kutengeneza umeme nchini tuje na miradi mikubwa, hata kama nchi itasimama kufanya shughuli nyingine kwa miaka mitano, lakini ikitatua tatizo la umeme, huo utakuwa uamuzi wa basara sana. (Makofi)

MBUNGE FULANI: Yes! Yes!

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikarudi nikaangalia Hansard za Bunge la Bajeti mwaka jana. Waliotoa maoni hayo wakati Serikali imeanza kuzungumzia suala la Stiegler’s gorge, wakaanza kusema kwamba mradi huo si sahihi kwa sababu unaharibu mazingira. Leo tumekuja hapa tena tunasikia hoja zinazidi kubadilika ninachomaanisha kwamba mradi huo sasa sio sahihi mkandarasi aliyepewa hana uwezo wa kujenga. (Makofi/ Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini inakuja hoja nyingine mpya kwamba mradi huo Watanzania wasiutegemee kesho au kesho kutwa nani alisema mradi mkubwa kama huu unaweza ukajengwa ndani ya mwaka mmoja? (Makofi)

MBUNGE FULANI: Mmmh!

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo unaweza kuona ni kwa namna gani Watanzania wanaanza kukubali na kuzielewa kazi nzuri zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano. Sasa hili ni jambo zuri kwa sababu umeme ambao unakuja kujengwa kwenye nchi hii, unakwenda kuondoa matatizo mengi ambayo yamekuwa yakiisumbua nchi kwa muda mrefu. Wakati mradi huu ukiendelea miradi mingine ya kuimarisha umeme inaendelea kufanywa ili Tanzania isiwe gizani wakati wa kusubiri mradi huu. Watanzania wanaelewa kwamba tunakoelekea sasa tunakwenda kulitatua tatizo hili moja kwa moja. Kwa hiyo, naipongeza sana Serikali kwa maamuzi haya magumu wanayoyafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, limezungumzwa suala hapa pia la LNG na kuna msemaji mmoja alitoa taarifa kwamba wananchi wasahau kuhusu LNG kwa sababu baada ya sheria mpya za kutunza rasilimali za nchi hii zilizotungwa mwaka 2017, hakutokuwa na mtu atakayetamani kuja kufanya miradi ya LNG.

Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri haya masuala ya gesi ni masuala sensitive sana si kila mmoja anaweza kuyasema yana technicalities zake. Taifa halikuwa likitafuta Mkandarasi kwa ajili ya kujenga LNG, lakini waliokuwa wakifanya kazi ya gesi kwenye Kitalu Block one na Block two baada ya kugundua gesi nyingi wakasema hii gesi huwezi kuiuza hapa ndani ni lazima itengenezewe plant za LNG iuzwe nje. Serikali ikawaambia badala ya Block one kujenga LNG yake na Block two kujenga LNG yake, shirikianeni mjenge plant moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa maana kwamba Equinor ambao zamani walikuwa wakifahamika kama Statoil wakishirikiana na ExxonMobil ambao ndio wako block one washirikiane na Shell ambaye ndio alinunua hisa za British Gas (BG) ambaye na yeye anashirikiana na Ophir Energy na Pavilion Energy kwamba hawa washirikiane kwa pamoja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa wakati Statoil ambao ni Equinor leo wanahangaika na hili Shell alikuwa busy na Plant ya Msumbiji, kwa hiyo wakawa hawashirikiani vizuri. Equinor wakaamua kupambana kuishauri Serikali iwaruhusu wajenge plant yao wenyewe na mwezi wa Disemba Serikali imeridhia kwamba nyinyi Equinor mnaweza kuendelea na plant yenu. Leo mtu akisema hapa wananchi washukuru Mungu kuhusu LNG maana yake anazungumza jambo asilolijua. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niishauri tu Serikali hapa sasa kwa sababu mradi wa LNG ni mkubwa na kwa kuwa mmewaruhusu Equinor kuendelea na LNG basi kiundwe kitengo maalum cha kushughulika na hiyo LNG kama ilivyofanywa kwenye Stiegler’s gorge. Kwamba kumekuwa na kitengo maalum kinashughulikia uendelezaji tu wa Stiegler’s gorge na kwenye LNG vile vile kiundwe kitengo cha namna hiyo ili hawa Equinor wawe na mtu ambaye wanadili naye moja kwa moja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa haya mambo ya gesi usipoyajua kwa kweli yatakusumbua na ndio maana mtu anaweza kuja hapa akahoji, bomba kubwa la gesi mpaka leo utilization yake ni 7% tu, hiyo ndio sahihi kwa sababu bomba lile halikujengwa ili lijae ndani ya miaka miwili. Kwa sababu kama lingejaa ndani ya miaka miwili ndio ingekuwa hasara. Lile bomba linatakiwa lisijae hata ndani ya miaka
20. Kwa hiyo, kama leo liko 7% maana yake ujenzi ule uliona mbali zaidi na tuna sababu ya kuipongeza Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Watanzania waanze kuzoea vitu vikubwa vinavyojengwa kwa fedha za ndani, yale mengi ambayo tulikuwa tukiamini huko nyuma kwamba hayawezi kutekelezeka ndani ya Awamu ya Tano yanatekelezeka. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikienda kwenye Kamati nyingine ya Ulinzi na Mambo ya Nje…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha muda wa Mzungumzaji)