Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

MHE. ESTHER M. MMASI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa nafasi hii, awali ya yote ninamshukuru Mwenyenzi Mungu kwa nafasi hii aliyonipatia na pia wananchi wangu kutoka Kilimanjaro akina mama wale kwa upendo wao ninawashukuru sana, niombi langu kwa Mwenyenzi Mungu aweze kuniongoza kwa hekima za Kimungu niweze kuutumikia utumishi wangu huu kwa moyo wa uadilifu, kwa moyo wa kujitoa na kujituma, nitamsihi sana Mwenyenzi Mungu anisimamie katika utumishi wangu huu mpya.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada yakusema hayo, nimesimama mbele yako kumpongeza Mheshimiwa wetu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Joseph Pombe Magufuli, kwa hotuba yake nzuri. Hotuba yake ilivaa kiatu cha Mtanzania mwenye kipato cha hali ya chini, kiatu chake kilivaa kila aina ya mtu ambaye alikuwa na uhitaji na imani yake katika Serikali yetu hii ya Awamu ya Tano.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuanza tu kuchangia moja kwa moja katika hotuba hii mimi nitapenda kujikita kwenye mambo mawili kama siyo matatu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nikaanza na kwenye suala la ajira, ni kweli kwenye ukurasa ule wa 15, Mheshimiwa Rais alianza kuonyesha kwamba na alikiri pale kwamba ni kweli Tanzania suala la ajira bado ni changamoto kubwa na ukiangalia takwimu zinasema ingawa uchumi umekuwa kwa asilimia 7.1 lakini asilimia 28 ya Watanzania bado ni maskini. Lakini katika kutatua changamoto hii Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli alielekeza hisia zake na alielekeza weledi wake kwa kusema kwamba njia mojawapo ya kujitoa kwenye umaskini ni pamoja na kuwa na viwanda na akasema pale tukiwa na uchumi unaotegemea viwanda pengine tutazalisha ajira za asilimia kama 40 hivi. Sasa katika hili mimi nitapenda kuchangia changamoto ambazo tuko nazo na ndiyo imekuwa kama ajenda ya dunia lakini pia imekuwa ni ajenda ya Watanzania walio wengi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuanza na suala la ajira. Katika suala hili la viwanda Mheshimiwa Dkt. Joseph Pombe Magufuli, alianza kwa kuonyesha kwamba ni vema sana uchumi wa Tanzania ukalenga ule ubepari wa Kitaifa na tukatoka kwenye ubepari mamboleo. Ubepari mamboleo ni uchumi ule unaokuzwa au unaojengwa kwa uchuuzi, yaani hautumii malighafi ya ndani wewe unaagiza malighafi kutoka nje unalisha viwanda vya ndani, na kwa kufanya hivi kutoka kwenye ubepari mamboleo kwenda kwenye ubepari wa Kitaifa ndiyo njia pekee ya kujenga uchumi wa Tanzania na uchumi wa viwanda ulioimarika na kasema kwamba pamoja na viwanda hivi aliweka umuhimu wa kukuza sekta ya uvuvi, kilimo na ufugaji na katika hotuba yake pia alipokuwa anaongea na wafanyabiashara alionyeshwa kusikitika kwake na akasema inasikitisha sana kuona Tanzania ndiyo nchi pekee yenye mifugo mingi ikianza na Ethiopia Tanzania ikiwa ya pili lakini hatuna viwanda vya samli, hatuna viwanda vya ngozi, leo hii hatuna viwanda vya uvuvi alionyeshwa kusikitishwa.
Sasa katika mchango wangu katika sekta hizi tatu ni upi? Mimi nitapenda kusema kwamba ukianza na suala zima la kilimo ni kwamba ifike sasa Serikali yetu iweze kutambua changamoto kubwa ambazo tuko nazo.
Moja, ikiwa ni vikwazo vya kisheria, ukiangalia hasa sheria hii ya Vyama vya Ushirika, mathalani mimi ninayetoka Kilimanjaro, leo siwezi kulima kahawa na nikawa na direct control na ile kahawa. Watu wengi walikuwa discourage waka-prone zile kahawa ambalo ni zao kuu la uchumi na tunajua kabisa mchango wa zao kuu kama hili. Kwa hiyo, hii inakatisha tamaa, ifike sasa tutoke kwenye sheria kandamizi, sheria za kikoloni ambazo haziwezi kumsaidia Mtanzania wa leo. (Makofi)
Lakini pia katika suala zima la ajira, mimi ninafikiri ifike sasa Tanzania ichukue hatua madhubuti, mimi niliangalia juzi bajeti ya Kenya ya mwaka 2014/2015 ni bajeti ya juzi tu, niliona pale wenzetu walivyojidhatiti katika suala la ajira, kuna mfuko pale wa vijana, lakini mfuko huu kwa Tanzania yetu ya leo mfuko huu umefichwa katika Baraza la Taifa la Uwekezaji. Mimi ninashauri, kwa ombi ninaomba sana Wizara husika iweze kutoa mfuko ule pale ulipo, uwe ni mfuko wa kujitegemea vijana wetu waweze kupata ajira kupitia mfuko ule. Kwa nchi ya Kenya waliweza kutenga shilingi trilioni 8.1 sawa na pesa za Kitanzania shilingi bilioni 32.4, kwa pesa za Kitanzania hizi ni hatua madhubuti katika kumsaidia Mtanzania.
Lakini pili, nikija haswa kwenye suala la hili la ajira nafikiri sasa ifike muda ofisi husika au Wizara husika iweze kutumia tafiti zinazofanyika Tanzania. Mathalani, katika taasisi za umma kuna convocation office kule wanafanya tracer studies nyingi na kuonyesha na kubaini kijana huyu anayemaliza leo kesho atakuwa wapi na anafanya nini.
Mheshimiwa Naibu Spika, ombi langu kwa Wizara husika ni kwamba tafiti ziingizwe kwenye matumizi, donors wengi wanatoa pesa nyingi ziende kwenye tafiti lakini haziingizwi kwenye matumizi.
Mathalani tunaenda kwenye uchumi wa viwanda tusipojikita kwa kuangalia suala la research and development siamini kama tutafika. Juzi watu wengi walikuwa wanajiuliza hapa tutalindaje viwanda vyetu, jibu ni kwamba tutahitaji kutupa jicho letu kwenye upande wa pili, suala la research and development tulipe uzito wa hali ya juu. Walimu wanakesha maofisini wanafanya tafiti, lakini tafiti zile zimebaki kuwa kwenye makabati. Ninaomba ofisi husika iweze kutoa uzito wa pekee kwenye suala research and development, tukifanya hivi tutalinda uchumi wetu wa Tanzania, tutalinda viwanda vyetu vya ndani.
Mheshimiwa Naibu Spika, nikija kwenye suala la elimu, ninashukuru Mheshimiwa Rais alionyesha umuhimu kwamba elimu iwe bure, lakini changamoto nikianza pale mimi nilipopita mathalani Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, nimefanya research nimetembea na data nitakazozitoa ni data ambazo nimezitoa field, ninaongea kwa masikitiko makubwa, ninaongea nikiumia na nimeguswa sana. Mathalani Chuo Kikuu cha Dar es Salaam chuo kikubwa kama kile hakina hostel kwa wanafunzi, wanafunzi wanauwawa, wanafunzi wanapigwa risasi, mwaka jana tarehe 15 Desemba kijana mwaka wa nne wa CoET alipigwa risasi akiwa anasoma Yombo five, lakini pia mwaka 2013, ninakumbuka ilikuwa tarehe 23 Aprili, kijana Henry Chuo cha Uhasibu Arusha alipigwa risasi akiwa anasoma, akiwa anatoka bwenini…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Michael muda wako umekwisha.