Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Ubadilishaji Hadhi Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi, Kimisi, Ibanda na Rumanyika – Orugundu kuwa Hifadhi za Taifa

Hon. Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Ubadilishaji Hadhi Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi, Kimisi, Ibanda na Rumanyika – Orugundu kuwa Hifadhi za Taifa

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Kwanza, Tanzania tumebahatika kuwa kwenye eneo zuri sana la vivutio hivi vya utalii. Ukiangalia ikolojia yetu Tanzania na ukiangalia vivutio vya utalii Tanzania na tukijilinganisha na dunia sisi tuko kati ya wale watano bora duniani kwenye vivutio vya utalii. Kwa mfano, ukiangalia GDP ya Taifa letu na ukiangalia fedha za kigeni za Taifa letu leo utalii unaongoza nchi yetu hii kwenye fedha za kigeni. Kwa takwimu za mwaka jana zilikuwa ni shilingi bilioni 2.4 ambayo ni asilimia 28 ya fedha zote za kigeni zinatokana na utalii.

Mheshimiwa Spika, sasa utalii huu unawezeshwa na zile hifadhi zetu za Serengeti ikiongoza, KINAPA, Tarangire, Manyara, Arusha na Ngorongoro pia. Tunahitaji Wizara ikawa na vision yenye mwelekeo au mpango mkakati sahihi. Watuambie ule mpango mkakati wa 2022 umefikia wapi ili ku-double GDP na forex kwenye utalii? Kwa mfano, Southern Corridor, Ruaha, Mikumi na kwingine, hizi hifadhi tano ambazo ndiyo zina break even, ambazo zinazalisha zile nyingine na TANAPA wanafanya kazi nzuri sana chini ya Jenerali Waitara kama Mwenyekiti wa Bodi, Allan Kijazi - Mkurugenzi wa Bodi, kwa kweli nawapongeza sana TANAPA kwa kazi kubwa sana wanayoifanya, wanafanya kazi kubwa sana na nzuri katika Taifa letu lakini tujiangalie kidunia miundombinu hii ya utalii ikoje? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa takwimu za mwaka juzi tunaonekana kwenye ushindani wa miundombinu ya utalii zikiwepo barabara zetu, viwanja vyetu vya ndege, vyuo vinavyohudumia watalii, hoteli kwa pamoja tunashika nafasi ya 110 kati ya nchi ya 133. Sasa ni namna gani tunaimarisha hii miundombinu kwenye hifadhi zetu iweze kwenda sambamba na kuhakikisha tuna- double GDP na forex yetu na kuhakikisha hifadhi zote hizi mpaka za Moyowosi anazosema Mheshimiwa Nsanzugwanko na Tanzania yote Mwenyezi Mungu aliyotujalia mambo haya yanakuwa ni endelevu. Tukiwekeza vizuri hapa, hata sekta nyingine zikisuasua lakini hii Mwenyezi Mungu aliyotupatia tuhakikishe inakwenda kwa kasi kubwa. Kwa hiyo, tuwekeze miundombinu ya kutosha kwenye sekta hii. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia ile asilimia 10 ambayo TANAPA wanachangia kwenye Mfuko Mkuu basi iondolewe moja kwa moja irudi kwenye miundombinu ya utalii. Vilevile Southern Corridor ambayo imeshaanza tusiiachie katikati na hizi nyingine zote ambazo zimeletwa kwa Azimio hili tuziangalie ili Tanzania iwe ni sehemu nzuri na salama kwa vivutio vyetu.

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa muda ulionipatia. (Makofi)