Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Ubadilishaji Hadhi Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi, Kimisi, Ibanda na Rumanyika – Orugundu kuwa Hifadhi za Taifa

Hon. Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Ubadilishaji Hadhi Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi, Kimisi, Ibanda na Rumanyika – Orugundu kuwa Hifadhi za Taifa

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kupata dakika tano na bila kupoteza muda niunge mkono maamuzi haya ya Serikali, niipongeze Serikali, niipongeze Wizara kwa uamuzi huu.

Mheshimiwa Spika, katika mchango wangu kwa sababu ni mtaalam na mimi katika sekta ya Maliasili na Utalii basi nitatoa angalizo na ushauri zaidi na dakika tano ulizonipa ni kidogo lakini nitajaribu kuzitumia vizuri.

Mheshimiwa Spika, la kwanza, naomba Serikali iiangalie hii TANAPA kwa macho mawili sasa kwa sababu tunaiongezea mzigo TANAPA, ni sawasawa na gari unaliongezea shehena ya mzigo, kwa hiyo ulaji wake wa mafuta, tyres na break utaongezeka zaidi. Kwa hiyo, TANAPA iangaliwe kwa macho mawili kwa sababu matumizi yake yatakuwa ni makubwa zaidi. Tukumbuke kwamba TANAPA ina hifadhi 16 na ni tano tu ndiyo zinazojitegemea zilizobakia zote zinategemea huku. Kwa hiyo, uwezo wa TANAPA kurudisha kwenye Serikali utakuwa mdogo na lazima tuiangalie kwa macho mawili.

Mheshimiwa Spika, kitu cha pili ambacho naiomba Serikali hiki ikifanye kwa umakini mkubwa na kitapunguza gharama, ni ushirikishwaji wa wananchi katika zoezi hili. Ningependa hifadhi hii iwe ni hifadhi ya mfano sasa katika Taifa ili kuondoa yale malalamiko yote yaliyokuwepo katika hifadhi. Sitaki kuamini kwamba ushirikishwaji wa wananchi umekamilika au wameshirikishwa kikamilifu. Sijui approach iliyotumika, nimesoma kabrasha lote sijaona, lakini niseme tu kwamba kama wananchi watashirikishwa kikamilifu na wakapewa alternative nyingine za maisha yao, wao ndiyo watakuwa walinzi wa kulinda hili.

Mheshimiwa Spika, nimeshamshauri Mheshimiwa Waziri mara nyingi, Zanzibar katika mapori tulikuwa na walinzi zaidi ya 30 sasa hivi kila pori linalindwa na walinzi watano kwa sababu wananchi wenyewe ndiyo wanaolinda maeneo yao, lakini wamepangiwa na wameshirikishwa. Sasa sijui samples maana yake nimesoma ameshirikisha Kamati za Ulinzi na Usalama, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya lakini hajataja kijiji hata kimoja ambacho ameshirikisha na ametumia approach gani kuwashikirikisha wananchi na kwa kiasi gani na wao wametoa maoni yao na kukubali, kwa sababu ni lazima itapishana, vijiji 48 kila kijiji kina mahitaji yake tofauti.

Mheshimiwa Spika, uthibitisho katika hilo ukisoma ukurasa wa 15 na ukurasa wa 17, kwenye fungu lile 314 na fungu 332 litakupa uthibitisho kwamba ushirikishwaji wa wananchi umekuwa mdogo wasingeweza kuvunja beacons ambazo zimewekwa. Kwa hiyo, waliwashirikisha katika kuonesha ile mipaka ya asili lakini hawajawashirikisha katika zoezi hili zima ambalo wanataka kulifanya nao watafaidika vipi na watakuwa na sehemu gani. Wananchi wakishirikishwa vizuri nasema tena kwamba ulinzi ambao TANAPA watapata kazi kubwa ya kulinda utakuwa umekatika kwa sababu wananchi wenyewe ndiyo watakaolinda wakijua watafaidika vipi katika hili. Katika hili pia sijaona kama ametaja WMS, je, katika vijiji hivi 48 vyote hakuna kijiji ambacho kina WMS ambayo ipo pale na imeshiriki vipi na imetoa maoni gani.

Mheshimiwa Spika, la mwisho kabisa, uwekezaji wowote, baada ya sasa umeshawekeza kazi kubwa sana iliyopo na ya gharama kubwa ni marketing. Sasa Serikali pamoja na TANAPA sijui imejipanga vipi kwa sababu hiki ni kitu kipya kinaanzishwa katika suala zima la marketing. Marketing ni gharama kubwa, inahitji watu wenye weledi, watu ambao wanaujua undani wa yale mapori na kilichomo mule ndani na namna gani wamejipanga kuitangaza hii ili sasa lile lililokusudiwa liweze kufikiwa. Marketing kwa maana mbili; marketing kwa maana ya wale wawekezaji watakaokuja kuwekeza pale, namna gani wamewahamasisha, wamewatengenezea miundombinu ya kuhamasika kuwekeza pale, lakini marketing na ya wageni ambao sasa waje kutembelea pale.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu ya dakika tano, nakushukuru sana.