Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nipongeze kazi ya Kamati mbili na wachangiaji wote wamefanya kazi nzuri sana.

Mheshimiwa Spika, la kwanza, viwanda vyetu ya Agro-Processing ambavyo ni priority namba moja; viwanda vya kubangua korosho, vya kusindika alizeti, ufuta, pamba, kuzalisha mafuta ya kula, viwanda vya nguo, viwanda vya bidhaa za ngozi vinahitaji hatua madhubuti za kuvilinda dhidi ya ushindani wa aina mbili. Kwanza, ushindani wa bei ya malighafi kwenye soko unaosababisha viwanda vyetu kukosa malighafi na pili, bidhaa zinazozalishwa kwenye viwanda hivyo kushindwa kukabiliana na bidhaa za aina hiyo hiyo zinazoagizwa kutoka nje ambazo hata tukitoza kodi asilimia 35 bado bei ya bidhaa hizo sokoni inakuwa ndogo kwa sababu huko zilipotoka zilizalishwa kwa mamilioni ya tani kwa gharama ndogo ya jumla kwa ajili ya soko zima la dunia kulinganisha uzalishaji mdogo wa hapa nchini wa mia na maelfu ya tani ambayo yanalenga soko dogo la ndani ya nchi.

Mheshimiwa Spika, kwa hali hiyo, upo umuhimu mkubwa wa kuchukua hatua za lazima. Kwanza, kuhakikisha viwanda vyetu vinakuwa na uhakika wa kupata malighafi na hatua ambazo zitapendekezwa na wataalam zitatusaidia sana kupata maamuzi sahihi kwa ajili ya kulinda viwanda vyetu vya ndani. Pili, tunahitaji kutengeneza utaratibu wa makusudi wa kukabiliana na wimbi la waingizaji kutoka bidhaa kutoka nje kwa kutumia viwango maalum vya kikodi vitakavyotozwa kwa utaratibu wa kutoza kwa tani badala ya asilimia ambayo itasaidia kulinda viwanda vyetu vya ndani.

Mheshimiwa Spika, kilimo chetu kinahitaji mbolea kama kweli tunataka kuongeza uzalishaji kwenye sekta ya kilimo. Uagizaji wa mbolea kutoka Ulaya hadi mbolea imfikie mkulima umekuwa ukigharimu fedha nyingi mno kwa mkulima. Serikali imeshawakaribisha wawekezaji kujenga viwanda vya mbolea hapa Tanzania, tunachotaka sisi ni ukweli na uwazi kwenye uwekezaji. Tunajua mwekezaji anahitaji mtaji ili awekeze lakini mtaji ule sisi tuna maslahi nao tunataka tujue, mtaji ule ndiyo unaotafsiri gharama za mitambo, majengo, teknolojia, uendeshaji ikiwepo kulipa wafanyakazi na usafiri na usafirishaji hadi kwenye soko. Pia ni lazima tujue tunamsaidiaje mwekezaji kupata malighafi anazohitaji kwenye kiwanda kutoka ndani ya nchi na kwa gharama gani?

Mheshimiwa Spika, ili tujue vizuri lazima tulinganishe model yake ya kifedha na ile model ya mfano ambayo imetengenezwa na wataalam wa Serikali ili tuweze kubaini hasa hasa je kuna udanganyifu au hakuna kwa sababu bila kufanya hivyo tutaingia kwenye machaka ambayo tuliwahi kuingia zamani. Kwa mfano, katika model moja ya kifedha iliyochambuliwa tulikuta gharama za wafanyakazi wote 1,000 ikiwemo wafagizi wote wamewekewa mshahara wa kila mfanyakazi dola 3,000 yaani Sh.6,430,000 jambo ambalo ni kinyume cha uhalisia kwenye ukweli na uwazi. Kwa hiyo, lazima tuwe makini mno ili kuhakikisha tunalinda maslahi ya Taifa kikamilifu, viwanda vya mbolea vinahitaji gesi asilia kwa mfano na mali ghafi nyingine lazima tujue gezi asilia ataipata kwa gharama gani na faida ya nchi itakuwa kiasi gani.

Mheshimiwa Spika, mwezi huu Februari tunaendeleza mazungumzo na wawekezaji kwenye eneo hili la viwanda vya mbolea na mwelekeo ni mzuri naamini tutafikia makubaliano mazuri. Haiwezekani tukubali kiwanda ambacho eti kitapata hasara kwa miaka zaidi ya 10 wakati ambako ile financial model inaonyesha kuna udanganyifu ambao utamfanya mwekezaji yeye aanze kwa kupata faida ya dola kama 600,000 kabla hata hajaanza uzalishaji halafu ile mizania yake itasoma hasara kwa zaidi ya miaka 10. Kwa hiyo, sasa hivi Serikali ya Awamu ya Tano ipo makini katika kujenga utaratibu wa win win situation ili tunapoingia kwenye kiwanda lazima tuhakikishe faida ya nchi inaonekana kwa wazi na uhakika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)