Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Peter Joseph Serukamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Spika, nami nawapongeza viongozi wa Kamati zote mbili walioleta report yao hapa ndani. Naomba nijadili zaidi kwenye kilimo. Toka tumepata uhuru kuna mazao ndiyo mazao ya kimkakati Tanzania kwa maana ya kahawa, katani, chai, korosho pamoja na pamba pamoja na palm oil. Nimeamua kuangalia uzalishaji wetu wa haya mazao na ili twende mbele kiuchumi lazima tuongeze uzalishaji. Uzalishaji wa kahawa Tanzania ni tani 100,000; kwa nchi 10 bora duniani Brazil wanazalisha tani 2,500,000; Vietnam tani 1,650,000; Colombia tani 800,000; Indonesia tani 600,000; Ethiopia ambayo ni ya tano duniani inazalisha tani 4,84000.

Mheshimiwa Spika, kwa nini nasema haya? Nataka sasa kama Taifa tuanze kujielekeza kwenye uzalishaji, tuache kuhangaika na kutatua matatizo ya siku, maana mwaka jana 100,000, mwaka huu 100,000, mwaka keshokutwa, hii siyo sawa. Leo hii tuna matatizo ya fedha za kigeni, tutazipataje; ni kwa ku- export mazao yetu haya ya biashara. Ili tuweze kuongeza uzalishaji, najua hili jambo wengi hawalipendi, lakini ni lazima tuanzishe mashamba ya biashara, lazima tuanzishe commercial farming in Tanzania kwa sababu ardhi tunayo, maji tunayo, lakini tusipo-embrace commercial farming na commercial farming ina faida zifuatazo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwanza watahangaika na ubora; pili, watahangaika na quantity; watahangaika kutafuta soko, watatoa ajira, watatoa mafundisho, watatoa pembejeo, watatafuta za kwao, lakini watalipa kodi, lazima kama Taifa tuseme tunapoenda ndani ya miaka mitatu ijayo, tutaondoka kwenye kahawa kutoka 100,000 kwenda 500,000 na unajua maana yake nini? Maana yake unaingiza fedha nyingi za kigeni hata bei ya dunia ikianguka kwa sababu quantity inakubeba bado itakusaidia kama Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitakwenda kwenye katani, katani iliyokuwa inazalishwa miaka ya 1970 leo haipo, leo katani duniani bei imepanda, lakini tunazalisha tani 50,000, lakini tuna uwezo wa kuzalisha tani 1,000,000, tufanye nini? Ni lazima tuhangaike, tuondoke kwenye 50,000 ili twende kwenye tani angalau 500,000 na tukifika tani 1,000,000 maana yake tutaingiza dola milioni 700 kwenye uchumi wa Tanzania, lakini ili tufike tuhakikishe watu wengi household nyingi zinalima mkonge, tuhakikishe financing inakaa vizuri. Lakini ili commercial farming ifanye kazi lazima tulete wanasema Wazungu legal framework with clarity.

Mheshimiwa Spika, Mfalme wa Dubai wakati anafanya mabadiliko Dubai Baktoum familia yake walimfuata wakasema wewe mzee mbona unagawa ardhi yetu ya Dubai kwa Wachina, Wahindi na Wazungu; aliwaangalia akawajibu jambo moja tu, siku ambapo Mchina na Mhindi yuko Airport anaondoka na ghorofa lake mniite, hata sisi akija mtu tukampa ardhi, akalima, tukiamua kumfukuza haondoki na ardhi hawezi kuibeba, kwa hiyo lazima tubadilishe mindset kwenye agriculture, we can’t go like this.

Mheshimiwa Spika, nitakwenda kwenye chai, Tanzania tunazalisha tani 19,000 tu, wakati Wakenya ambao wana eneo dogo kuliko sisi wanazalisha tani 300,000 na leo Kenya ni ya tatu kwa chai duniani, maana yake ni nini; kwa sababu wame- embrace mashamba makubwa, wamewekeza na ukitoka tani 18,000 ukafika tani 300,000 tu, maana yake unaingiza kwenye economy dola nyingi sana na GDP ya kilimo itatoka kutoka asilimia 30 mpaka 50 kwa sababu tunayo ardhi, tuna watu na tuna mvua. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitakwenda kwenye korosho, nasikiliza kelele za korosho, unajua maana yake nini, ni kelele za kitu kidogo wanataka kupigania watu wote. Tanzania tunazalisha tani 210,000, lakini kwenye korosho Vietnam wanazalisha tani milioni 1,200,000; Nigeria tani 900,000; India tani 600,000; Cote d’Ivoire tani 600,000; maana yake ni nini? Sisi Tanzania tunayo capacity ya kutoka 200,000 kufika 1,000,000. Leo ukitoka hapa 200,000 ukafika 1,000,000, 200,000 unapata dola milioni 600 kwenye economy dola maana yake ukienda 1,000,000 unaongelea shilingi ngapi ni six time five that is three billion dollars kwenye economy yako. Tunapambana kupigania umaskini wetu, lakini ili watu wa korosho walime wengi, tutengeneze commercial farming, wale wenye commercial farming, wanatafuta soko duniani na watawachukua hawa wachache, tutakwenda mbali kama Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, namalizia suala la pamba angalia pamba leo mwaka jana tumezalisha tani 200,000, lakini kama nchi tuna uwezo wa kufika hata tani 500,000. Mimi nasema lazima mawazo ya Mheshimiwa Waziri wa Kilimo, Mheshimiwa Waziri wa Ardhi na Mheshimiwa Waziri wa Fedha tubadilike sasa tu-invest kwenye grove, bila grove ndugu tutabakia hapa hapa, tunatafutana kwa nini hatuendi mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, palm oil Tanzania tuna import asilimia 55.5 ya edible oil karibia dola milioni 300 zikaenda kwenye ku-import mafuta ya kula, lakini tuna eneo zuri la palm oil Kigoma pamoja na Kyela, tuna eneo mikoa yote ya katikati kulima alizeti na siyo kwamba tumejitosheleza kwenye edible oil lakini na Tanzania tungeanza ku- export edible oil. Balance of employment, export tusipo-invest kwenye ukuzaji na uzalishaji, bado tutabaki tunahangaika ku-solve matatizo ya siku inayofuata. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tuna suala la ng’ombe, suala la maziwa Uganda pekee yake wanazalisha lita 1,000 000 ya maziwa, sisi wenye ng’ombe wengi, wenye ardhi kubwa lita 100,000 na angalia tunachohangaika nacho, hata wale watu ambao wana vi-ranch badala ya kusema tuwasaidie wazalishe zaidi tunakwenda kuongeza kodi za per square meter maana yake waondoke, maana yake wao hawana malisho, na hiyo kodi unayoitaka mwisho wa siku hutoipata, lakini ungeunganisha wale wafugaji wakazalisha maziwa mengi ukaja na viwanda, leo tungekuwa mbali sana.

Mheshimiwa Spika, juzi Uganda mtoto wa Museveni wa kike amefungua kiwanda kimoja tu anazalisha lita 100,000 za maziwa kwa siku, wala hawatuzidi ng’ombe wengi, hawatuzidi maarifa, hawatuzidi land, tatizo letu ni nini? Lazima tubadilike kama Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimalizie kwa kusema tatizo la maji; kama dunia itakuja kupigana vita ya tatu ya dunia italetwa na maji, lakini kwa bahati nzuri Tanzania Mungu katupa baraka ya maji, moja ya 16 ya maji yote safi ya kunywa duniani yako Lake Tanganyika, lakini watu wa kilometa tano kutoka Lake Tanganyika hawana maji, ukienda Mwandiga hakuna maji, ukinda vijiji vyote vya Simbo hakuna maji, ukienda Kalinzi, Mkiva, Nyarubanda hakuna maji lakini tunazungukwa na Lake Tanganyika. Niombe sana tuhangaike na suala la maji.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, naunga mkono hotuba zote za Kamati zote. (Makofi)