Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuongea. Ni dakika ngapi Mheshimiwa?

SPIKA: Dakika kumi.

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa hizo dakika kumi.

Mheshimiwa Spika, nchi zetu za Afrika zilikuwa zinatawaliwa na wakoloni kwa miaka mingi tu ikiwemo Tanzania nayo ilitawaliwa na Waingereza lakini kwa sasa wakoloni hawawezi kutawala nchi za Kiafrika, kilichobaki ni kuwatawala katika fikra zao yaani fikra za Waafrika wengi viongozi wengi na hasa wasio kwenye chama tawala wamekuwa colonized na Wazungu. Ndiyo maana utawakuta wapo maeneo mbalimbali wanazungumza mambo mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nasema hivyo kwa sababu gani? Nilikuwa naangalia hapa kwenye takwimu mbalimbali wanasema top ten best performing President in Africa, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli yumo. Ana miaka mitatu tu toka ametawala nchi hii lakini ameingia ni wa nane, amemzidi mpaka wa Rwanda miaka mingapi ametawala? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilikuwa natazama mtu anazungumza mambo ya Stiergler’s Gorge namshangaa. Nataka ni-declare interest kwamba mimi nimesoma diploma, certificate na degree ya mazingira. Sheria ya Mazingira inasema hivi utawale mazingira na mazingira yakutawale. Ukiangalia nchi zote duniani zilizoendelea zina mabwawa ya hydroelectric power; Marekani, China, Uingereza zote wanayo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitoe mfano mmoja tu, China sasa ina mahali panaitwa Gorges Dam capacity yake ni MW 22,500. China imechukua mito kama mitatu imekusanya yote, ina watu bilioni sijui 3 leo tunazungumza Tanzania MW 2,400 watu ng’e, ng’e, ng’e, hivi wamekuwaje? (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Spika, Marekani wana bwawa linaitwa Grand Coulee Dam, capacity yake ni 6,809. Sasa Marekani wametengeneza mto unaitwa Colombia, ule China unaitwa Yangtze, leo wale waliokuwa-colonized kwenye akili they are talking about mambo ya wazungu, sasa akili gani hizi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nitoe tu angalizo, nampenda sana rafiki yangu Msigwa na tupo Kamati moja, mimi Mungu alinisaidia kuwa mkweli, ni vizuri tuwe wakweli. Kwanza amezungumza kwamba kwenye Kamati yetu hakuna taarifa lakini taarifa hiyo imo. Kamati imempongeza Rais kwa kutatua migogoro mbalimbali ya ardhi nchini. Wewe ulitaka tuseme kwamba wamenyang’anya mashamba ya Sumaye? Rais anapofanya kazi nzuri ni kumpongeza. Naishukuru Kamati yangu ya Ardhi imefanya kazi nzuri sana. Kwa hiyo, tumempongeza Rais kwa kufanya kazi nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini Rais hanyang’anyi watu mashamba na Rais yeye hafuti umiliki. Nataka nitoe mfano, Bunge lako ndiyo linatunga sheria, leo mwanafunzi wa darasa la kwanza, la pili au la tano akiulizwa nani anatunga sheria za Tanzania watasema Bunge la Tanzania lakini hizo sheria haziwezi kwenda kufanya kazi bila Rais kupitisha. Kwa hiyo, Rais akipitisha ndiyo inakuwa sheria. (Makofi)

T A A R I F A

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, matatizo ya hawa jamaa ndiyo hayo hayo, yaani wao ni kukuza maneno, Mwenyekiti wetu sisi anafanya kazi nzuri, kama amejiuzulu, amejiuzulu kwa utaratibu wa kawaida wa watu kujiuzulu. Mimi nampongeza Mwenyekiti kama amejiuzulu kwa utaratibu wa kawaida basi sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niendelee, hakuna siku kwenye Kamati yetu na Mwenyekiti wangu yupo hapa tumewahi kuita watu wenye mashamba walionyang’anywa wakalalamika, tumeita watu wa porini, tourism na watu wa kila mahali, Kamati tuna majina.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

MHE. BONIFACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, tuna orodha ya mashamba mengi nchi hii yanayotegemea kufutwa na mengine yamefutwa na sheria iko wazi…

T A A R I F A

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nadhani huyu ana jambo analo kichwani ndiyo linalomsumbua, kwa hiyo, tuendelee na utaratibu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuja na orodha ya mashamba yanayopendekezwa kunyang’anywa au kufuta miliki siyo kuleta wadau waliolalamika. Ni kweli kwamba Kamati ilikuja na mashamba mengi tu ya wakulima wadogo na wakulima wakubwa. Sheria ya Ardhi iko wazi inakutaka ukipewa uwekezaji miaka mitatu uwe umeendeleza.

MBUNGE FULANI: Ndiyo.

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Sheria hiyo inasema tukitaka kunyang’anya shamba tutakupa siku 90 za kujitetea. Nani aliwahi kuleta hiyo barua wewe ukaiona? (Makofi)

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, niombe nchi yetu tufanye kazi moja kuwaelimisha Watanzania waelewe nini maana ya kuwa mzalendo.