Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuwapa pole Waheshimiwa Majaji na Mahakimu wote ambao wametajwa ndani ya Bunge hili ambao hawawezi kufika ndani ya Bunge hili kujitetea. Kanuni zetu za kilatini Mheshimiwa Tundu Lissu atakuwa mwenyeji kwenye hili right to be heard, rule of law ambazo zinatuongoza anazifahamu vizuri, lakini nitambue mchango Jaji Mkuu Mheshimiwa Mohamed Othmani Chande, amefanya kazi nzuri sana ya kuhakikisha kwamba mahakama zetu zinakwenda vizuri kupunguza kesi za mahakama ambazo zilikuwa msongamano kwa muda mrefu sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli naomba niwashukuru wapiga kura wangu wa Jimbo la Rufiji kwa kunielewa, wananifahamu kule Rufiji naitwa jembe, wengine wananiita sururu. Ninashindwa kutambua uwezo wa kisheria au uwezo wa kufahamu wa ndugu yangu Tundu Lissu, kwa muda mrefu sana nimekuwa nikifuatilia mchakato na namna ambavyo akiendesha Bunge kwa muda mrefu sana kwa zaidi ya miaka sita nimekuwa nikimfuatilia. Mheshimiwa Tundu Lissu namfananisha na mwandishi wa vitabu vya movie, aki-act mwaka 1940 ile movie ya Ndugu Charlie Champlin. Kuna movie moja, political satire, hii ukiifuatilia vizuri inaendelea kiundani, Mheshimiwa Tundu Lissu ni mtaalam mzuri wa kuiga kisiasa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nielezee uteuzi wa Mawaziri. Tunaongozwa hapa na Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 1977, kama ambavyo imekuwa ikirekebishwa mara kwa mara. Lakini katika Katiba hii, Ibara ya 54 na 55 inazungumzia kwa uwazi uteuzi wa Mawaziri. Ibara ya 56 inazungumzia mchakato mzima wa nani anaweza ku-qualify kuwa Waziri yaani kwamba mchakato huu, mtu atakuwa Waziri baada tu ya kuapishwa na Mheshimiwa Rais. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia tunaongozwa na Sheria Na. 15 ya mwaka 1984 kama ambavyo Mheshimiwa Tundu Lissu ameizungumzia. Katika instrument of appointment ya Mawaziri ambayo Mheshimiwa Tundu Lissu amekuwa akiikazania kwa muda mrefu, siyo yeye tu hata Mwenyekiti wa Chama chao amekuwa akizungumza sana kuhusiana na sheria hii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Bunge hili lipate fursa ya kutufundisha kizungu inaonekana kuna shida ya kufahamu kizungu. Kwa mujibu wa Sura ya 299 ya sheria inayompa mamlaka Mheshimiwa Rais ya kuwaapisha pamoja na kuunda instrument yaani sheria hii inaitwa The Minister‟s (Discharge of Ministerial Functions) Act, Sura ya 299. Ukisoma kifungu cha tano cha sheria hii kinasema hivi ninaomba wataalam wa linguistic watusaidie ili waweze kumuelewesha huyu bwana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kifungu cha tano cha sheria hii kinasema hivi; “The President may, may na shall ina maana kubwa sana kwa kizungu. Wataalam wa linguistic watusaidie kumfahamisha may ina maana gani na shall ina maana gani. Siyo hivyo tu kifungu hiki kimekwenda moja kwa moja kuzungumzia kwamba from time to time by notice published in the Gazette specify the departments, business and other matters responsibility for which he has retained himself or he has assigned under his direction to any Minister, and may in that notice specify the effective date of the assumption of that responsibility. (Makofi)
Sheria hii inasema wazi ni wakati gani. Mheshimiwa Rais wakati wowote anaweza kutengeneza instrument kwa sababu sheria hii haija-specify ni wakati Mheshimiwa Rais anapaswa kutoa gazette la Rais. Sheria hii haitoi muda. Kwa hiyo, Mheshimiwa Rais hajavunja Katiba yoyote kwa mujibu wa sheria hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, niende mbele zaidi, amezungumzia suala zima la ESCROW kuna Majaji walishutumiwa not kushtakiwa. Naomba nimkumbushe vifungu vya sharia vinasema allegation however strong it may it cannot convict the accused person, hata kama shutuma zitakuwa na uzito wa kiasi gani haziwezi kumtia hatiani mshitakiwa.
MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Katiba Ibara ya 112 inazungumzia Tume ya Utumishi wa Mahakama. Tume hizi zimepewa uwezo mkubwa wa kujadili nidhamu za Majaji na Mahakimu. Ibara ya 113 inakazania kwenye suala hili zima. Bunge halina mamlaka juu ya Mahakama, hali kadhalika Serikali haina mamlaka dhidi ya Bunge na Mahakama. Kilichofanyika baada ya mapendekezo ya Bunge, Mheshimiwa Rais alikabidhiwa mapendekezo ya Bunge, kwa mujibu wa Ibara hii ya 113 Mheshimiwa Jaji Mkuu aliunda Tume, Tume ya Utumishi wa Mahakama ipo kwa mujibu wa Katiba.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Tume Rais hana mamlaka ya kumfukuza Jaji isipokuwa tu Ibara ya 113 inampa mamlaka Mheshimiwa Rais iwapo itaonekana Jaji amefanya utovu wa nidhamu na maadali baada ya Tume ya Utumishi wa Mahakama kutoa mapendekezo yake. Jambo hili lilifanyika na Waheshimiwa Majaji hawa baada ya kupitia na jambo kubwa ambalo lilifanyika, Mheshimiwa Jaji Mkuu pamoja na Tume hii walitumia the Code of Ethics for Judicial Officers, pia kwa kuzingatia the independence of the judiciary walizingatia haya yote kimsingi na ilionekana kabisa wazi kwamba hakuna jambo lolote lililofanyika na taarifa hii ipo mbele ya Mheshimiwa Rais kwa tafiti zangu binafsi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nitaenda kwa haraka. Kuhusu Mahakama ya Mafisadi imekuwa ikipigiwa kelele sana, sasa sijui kwa nini ndugu zetu hawa wanakuwa waoga, wanaogopa nini? Kwa mujibu wa taratibu na sheria kinachoweza kufanyika ni kufanya mabadiliko ya Sheria hii ya Uhujumu Uchumi ambayo Mheshimiwa Tundu Lissu ameizungumza hapa, Sura ya 200 imezungumzia kiundani kabisa. Division hizi za Mahakama Kuu zipo nyingi Tundu Lissu anafahamu, tunayo Division ya Ardhi, tunayo Division ya Biashara, tunayo Division ya Kazi, kwa mujibu wa taratibu na sheria hii kwa kufanya mabadiliko Mheshimiwa Jaji Mkuu anaweza akaunda special court kwa kupitia muundo huu ambao nimeuzungumzia hapa ambao inakua division ya Mahakama Kuu hakuna tatizo lolote wala Katiba haijavunjwa kutokana na hili. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa haraka nizungumzie Muungano. Mheshimiwa Tundu Lissu anasahau kwamba Muungano wetu uliasisiwa na Waasisi hawa wawili, Mwenyezi Mungu azirehemu roho zao. Kupitia Sheria Na. 4 ya mwaka 1964 iliondoa haya matatizo yote ambayo anazungumzia Mheshimiwa Tundu Lissu. Hata Mwenyekiti wa Marais Afrika anatambua mchango wa Tanzania katika kukomboa Bara la Afrika, siyo kwenda kusababisha Mapinduzi ya Zanzibar, Tanzania ilifanya kazi kubwa Afrika nzima siyo huko. Mimi nilichotegemea ni kwamba kwa Wapinzani wanapaswa kuleta hoja ya kusaidia Wizara hii ya Katiba na Sheria. Siyo kuanza kuzungumza maneno ambayo ni ya uchochezi maneno ambayo hayafai. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nilitegemea Mheshimiwa Tundu Lissu hapa angekuja na akatuambia ni namna gani tutaweza kulizungumzia Fungu Na. 40 ambalo Mheshimiwa Waziri hajalizungumzia, ni namna gani Mahakama itaweza kupatiwa fedha zake kwa mujibu wa taratibu na suala hili halijazungumzwa na Mheshimiwa Waziri. Lakini pia nilitegemea watu wa Upinzani wangezungumzia kuhusu Fungu Na. 55 la Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ili tume hii iweze kuongezewa fedha.
Ninaishauri Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi kuweza kuona mchakato wa kuongezea fedha Tume hii ya Haki za Binadamu na Utawala Bora.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba pia niongelee suala la Mahakimu. Mahakimu wetu wanafanya kazi ngumu, nawapongeza sana kwa kuchapa kazi Mahakimu na Majaji wote Tanzania. Ninaomba Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi kuona uwezekano wa kuwaongezea mishahara Mahakimu wetu, pia kuangalia kuwapatia non- practicing allowance pamoja na rent assistance kwa ajili ya kuwapunguza ukali wa maisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, tofauti ya mishahara kati ya Mahakimu na Majaji ni kubwa sana, ninaomba Mheshimiwa Waziri Tume ya Utumishi wa Mahakama kuweza kufikiria uwezekano wa kupunguza ukubwa wa tofauti ya mshahara kati ya Hakimu na Jaji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa haraka haraka Tundu Lissu pia amezungumzia kuhusiana na Mkuu wa Wilaya kutoa maelekezo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante sana.