Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

Hon. Dr. Philip Isdor Mpango

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nikushukuru sana kwa kunipa fursa hii nami nichangie hoja hizi zilizoko mbele yetu na hasa kwa kuzingatia kwamba mimi ni mdau wa kila Kamati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, na ninawapongeza Wajumbe na Wenyeviti wa Kamati zote mbili kwa uchambuzi wao mzuri sana, naamini kabisa utatusaidia Serikalini. Labda nianze na moja, lile linalohusu Shirika letu la Posta na hususan fedha zile ambazo walizitumia kulipa pensheni kwa wafanyakazi ambao walikuwa wameajiriwa East African Post and Telecommunications.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kufikia Septemba tarehe 30, 2016, tulikuwa tumepokea maombi ya kurejesha takribani shilingi bilioni 5.1 ambazo zilitumika kuwalipa pensheni wastaafu. Kati ya fedha hizo, ilipofika Februari 28, 2017 tulikuwa tumerejesha shilingi bilioni 2.7. Kwa hiyo, napenda tu kusema kama Serikali, tutaendelea kupunguza hilo deni kadiri mapato yanavyoruhusu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu deni lile la shilingi bilioni 26 ambalo linadaiwa na TRA, naomba nilifahamishe Bunge lako Tukufu kwamba kupitia ule utaratibu wa Tax Amnesty, kiasi cha shilingi bilioni 12 ambacho kilitokana na riba kimesamehewa kupitia Mamlaka ya Mapato. Hivi
karibuni Shirika letu la Posta limeleta maombi ya kufutiwa kiasi cha shilingi bilioni 14.8. Naomba niseme tu hili tunaendelea kulifanyia kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la mwisho upande wa Shirika la Posta, ni ushauri kwamba sasa tuliondoe kwenye orodha ya mashirika ambayo yanasubiri kurekebishwa. Hili suala tunaendelea kulifanyia kazi; na kama ambavyo tumefanya hivi karibuni kwa Shirika la Bima la Taifa NIC, tunakamilisha utaratibu pia wa kuliondoa Shirika la Posta kwenye orodha ya mashirika ambayo yanatakiwa kurekebishwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme pia kwamba tayari nimetekeleza agizo lako na natumaini utaendelea kuruhusu tuendelee na mawasiliano na Mheshimiwa Hawa. Tayari tumezungumza na nimemwonyesha hapa, Government Notice ambayo tulishaitoa kwa ajili ya kutoa hati ya msamaha kwa bidhaa ambazo zinatumika kwa ajili ya kujenga Terminal Three ambapo items takribani 277 zimepata msamaha kuanzia Januari tarehe 3. Kwa hiyo, nafikiri hilo limekwisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda lingine liseme kidogo alilisema Mheshimiwa Kishimba, kodi kwenye madini na hasa dhahabu, nimwombe tu, nakumbuka alichangia vizuri sana kwenye Mkutano wa Mheshimiwa Rais na Wachimbaji Wadogo wa Madini, kile kikao tulichofanya kwa siku mbili, tarehe 22 mpaka 23 Januari, 2019. Kama Serikali, tulipata mapendekezo mengi na namwomba tu avute subira kidogo tu, atapata majibu muda siyo mrefu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo ambalo limesemwa sana ni marejesho ya ile asilimia 15 ya import duty kwa importation ya sukari ya viwandani. Niseme tu kwamba Serikali imeanza kulipa; na mpaka kufikia Desemba, Serikali imerejesha shilingi bilioni 11.84 kwa Makampuni, SBC tumepeleka shilingi bilioni 3.5, BONITE shilingi bilioni 1.7, Nyanza Bottling shilingi bilioni 1.5, Coca Cola Kwanza shilingi bilioni 1.9, Bakhresa shilingi bilioni 2.3 na Jambo Food Products nusu bilioni. Kwa hiyo tumeanza kulipa na tunaendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme pia kuhusu GN ambayo nimeshaieleza lakini niliseme tu kwa ujumla. GN, Sheria zile za Kodi pale ambapo sheria zinaniruhusu kusamehe kodi, zinanitaka kama Waziri wa Fedha, nijiridhishe kwanza na bidhaa ambazo zinahusika, kama zinakidhi, lazima nijiridhishe kwamba bidhaa hizo, au msamaha huo unazingatia maslahi ya Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kubwa ni kwamba, tunajitahidi ili misamaha hiyo, isitumike vibaya. Kwa hiyo, kwa miradi mingi, kwa siku za karibuni tunatoa tunaita Global GN ambayo inarahisisha, lakini tumewabana Mawaziri wasimamizi wa Sekta husika, waji-committ kwa maandishi na kuhakikisha kwamba bidhaa zile zinazoombewa msamaha basi zinakidhi matakwa ya Sheria ya Kodi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu maduka ya fedha za kigeni, niseme kwamba zoezi tulilofanya hivi karibuni kupitia Benki Kuu, lilituonyesha mambo mengi ambayo siyo mazuri; kwanza maduka haya yalikuwa ni mengi mno bila sababu, mengine yalikuwa hayakidhi vigezo na mengine yalijihusisha katika utakatishaji wa fedha haramu na mbaya zaidi, ni kwamba Benki Kuu iliona kuna hatari ya kuhatarisha Financial Stability katika Taifa letu. Hili hatutalikubali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunaendelea kufuatilia kwa karibu, nasi tunaamini kabisa kwamba mabenki yaliyopo yanatosha kabisa kutoa huduma ya kuuza fedha za kigeni. Kwa hiyo, tunaendelea kufuata kwa karibu lakini la msingi sana ni kuhakikisha Financial Sector Stability katika Taifa letu inalindwa. Lingine lilisemwa hapa kwamba, hawaoni reforms kubwa ambazo tumefanya katika Taifa letu na hili linanishangaza kidogo. Kwa kipindi kifupi katika miaka mitatu, tumeongeza makusanyo ya mapato katika nchi yetu kutoka shilingi bilioni 850 kwa mwezi kwenda karibu trilioni 1.4. Jitihada za Mheshimiwa Rais, za kupiga vita Rushwa ni reforms za wazi kabisa ambazo ni transformative. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumefanya uwezaji mkubwa sana kwenye miundombinu na kwenye umeme. Zote hizo kama hazionekani ni transformative, basi kweli nashangaa. Tumeshughulikia sana suala la efficiency kwenye public service. Jamani vitu vingine tuwe honesty kidogo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu deni la ndani, in bottom line ni kwamba linaliopika, tumefanya uchambuzi, lakini ni muhimu kwamba tunahakikisha deni hili linakwenda kugharamia miradi ya maendeleo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, as long as tunaendelea kuhakikisha kwamba ni himilivu kwa vigezo vya ndani, halina tatizo, kaa na amani kabisa. Ukitumia BoT Monthly Economic Review ni muda mfupi sana. Nadhani na Mheshimiwa huyu alikuwa mmoja wa watu waliokuwa darasani kwangu miaka ile, ni vizuri akakumbuka kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kulihakikishia …

MWENYEKITI: Mheshimiwa nakuongezea dakika tano. (Makofi)

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Napenda tu kulihakikishia Bunge lako Tukufu, vipo vigezo sasa; tumemaliza Household Budget Survey ya mwaka 2017, tumehakiki kwa kushirikiana na baadhi ya wadau wetu na tutaleta taarifa rasmi katika Bunge ili kulieleza Taifa Household Budget Survey imeonyesha nini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kifupi tu, kwa mfano, basic need poverty imepungua kutoka asilimia 28.2 sasa imefikia asilimia 26.4. Vile vile umiliki wa rasilimali walizonazo wananchi wetu imeongezeka, lakini vilevile ajira katika sekta ambazo zinakua haraka, nayo imeongezeka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwa vigezo tu hivi vichache, ujue kwamba hii ni uhalisi, siyo namba tu. Nilisema suala juu ya vikwazo na usumbufu wakati wa kuingiza mizigo. Serikali inapokea ushauri, tutakaa na Wizara ya Viwanda na Biashara kama ilivyoshauriwa, tutazungumza na waagizaji wa bidhaa nchini; na ipo fursa na hasa baada ya Bunge hili, tutakutana nao ili tuweze kuona shida iliyopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa tunafanya hivi kama Serikali, lakini kwa sababu ya wingi wa makundi na mgawanyiko ndani ya sekta binafsi, tumekuwa tunakutana na Apex organizations. Kwa kikao kile cha Sekta ya Madini tuligundua kwamba unapata zaidi kwa kuzungumza na makundi maalum badala ya kuzungumza na haya makundi Wakilishi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tutakutana nao ili tuweze kuona namna nzuri zaidi ya kushughulikia upungufu. Kwa hiyo, ni jambo jema halina tatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi hii, naunga mkono hoja. (Makofi)