Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

Hon. Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kutoa maoni yangu katika mawasilisho ya Kamati za Kudumu za Bunge zote mbili. Nianze kwa kuwashukuru Wenyeviti na Kamati zao kwa kufanya kazi nzuri na hasa Kamati yangu ya Bunge ya Kudumu ya Miundombinu kwa jinsi ambavyo imeonesha weledi mkubwa sana kwenye Wizara yangu. Maeneo mengi sasa wanayafahamu vizuri na imekuwa ni bahati tu kwa sababu ajira yangu yote ilikuwa kule ndio maana naweza nikaenda nao vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niwashukuru sana kwa michango yao ambayo ni michango ya kujenga. Wamezungumza vizuri sana na kila wakati wananipa maoni na hayo maoni Serikali inayafanyia kazi. Kwa hiyo, nawashukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati yangu ya Kudumu ya Bunge, imeshauri katika maeneo mbalimbali, wameelekeza kwamba fedha za miradi ya maendeleo zitolewe kwa haraka. Nitoe taarifa kwamba nimshukuru sana Waziri wa Fedha hata mwezi wa 12 alitoa shilingi bilioni 200 na tumelipa tayari kwa ajili ya miradi ya barabara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuhusiana na bandari, kwa sababu bandari ndio lango kuu la uchumi katika nchi yetu. Waheshimiwa Wabunge wamependekeza kwamba asilimia 40 ya makusanyo ya bandari, basi yabakie kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya bandari. Baada ya tamko hilo niliwasiliana na Waziri wa Fedha lakini kwa mujibu wa sheria kwa sasa, hela zote za retention, hiyo Sheria ya Retention imeshafutwa ili ziweze kubakizwa kwenye taasisi za Serikali. Kwa hiyo hela yote inakusanywa na kupelekwa Hazina, lakini sisi tutaomba na kwa sababu bandari, inakarabatiwa sasa hivi kwa kuongeza kina, tunajenga magati nane kutoka sifuri mpaka saba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mradi ule tayari tumeshakamilisha gati namba moja na ndio lenye kina kirefu lina mita 15 kwenye low tide, kwa hiyo meli kubwa inaweza ikakaa pale na sasa hivi tunaendelea na study kwa ajili ya kuongeza pia kina cha ule mlango wa kuingilia meli kubwa. Kazi inaendelea vizuri na kwa kusimamiwa pia pamoja na hii Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na ununuzi wa flow meter ili tuwe na flow meter zenye uhakika na mpango wetu ni kuhakikisha kwamba tunakuwa na maeneo matatu ya flow meter. Kwa sababu wakati mwingine tunakuwa na meli zaidi ya sita za mafuta, sasa zikichelewa sana zinasababisha gharama kwa watumiaji. Kwa hiyo, tayari Serikali mwaka ujao wa fedha study zimeshafanyika, tutaomba fedha ili tuweze kuongeza flow meter.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati ya Kudumu ya Bunge imezungumzia kuongeza gati namba 13 na namba 14, tayari tumeshafanya mazungumzo na Benki ya Dunia baada ya kukamilisha huu mradi unaoendelea unaojenga magati nane, tutakwenda tena tukaongeze hayo magati namba 13 na namba 14.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika michango ya wabunge wamechangia kuhusiana na hii sheria mpya, Sheria mpya ya Kudhibiti Uzito wa Magari ambayo ni ya East Africa. Chanzo cha sheria hii ni usikivu wa Serikali, lakini pia ni usikivu wa Serikali kutoka kwenye Bunge na Wabunge walikuwa na haki kwa sababu miradi mingi tulikuwa tunatekeleza, lakini baada ya muda mfupi, barabara zinaharibika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kupokea maoni ya bunge lako Tukufu, Serikali ilii-engage consultant, ilitoa fedha, wakafanya study, ile study ndio iliyotuelekeza kwamba haya magari ya super single ndio yanayoongoza kuharibu barabara, kwa nini? Kwa sababu wanatumia size ya matairi ambayo ni 385/85 lakini kama size ya matairi itakwenda kwenye 465/67, basi hiyo effect haiwezi kuwepo. Sasa kwa sababu tayari tunayo sharia, niwaombe tu wasafirishaji waendelee kutumia sheria hiyo, lakini kama itabidi, itabidi tena tuite consultant ili tuweze kufanya study nyingine kwa ajili ya kuboresha. Serikali ni wasikivu na bandari haiwezi kufanya kazi bila reli, lakini bandari haiwezi kufanya kazi bila barabara pia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge wametoa mfano mzigo wa Zambia, ni kweli kabisa Zambia wana mzigo wa tani zaidi ya milioni 10 wanasafirisha kwa mwaka. Hata hivyo, mzigo unaopitia bandari ya Dar es Salaam ni tani milioni 2.2, ni malengo yetu sisi kwamba tuweze kuchukua mzigo mkubwa zaidi. Ndio maana nishukuru Waheshimiwa Wabunge ambao wamezungumzia pia Reli ya TAZARA, reli ile inatakiwa kubeba tani milioni tano kwa mwaka, lakini sasa hivi inabeba chini ya tani laki tatu kwa mwaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi Serikali ilitoa shilingi bilioni 10 tunakarabati vichwa saba ambavyo vitakamilika kabla ya mwezi wa Saba ili tuendelee kuongeza sasa uwezo wa ile reli kubeba mzigo zaidi. Malengo yetu kama walivyoshauri Waheshimiwa Wabunge kwenye Kamati ya Miundombinu, tutakaa pamoja na wenzetu wa Zambia, kwa sababu reli ile tunaichangia mali kwa asilimia 50 kwa 50. Tutakaa nao ili tuweze kuboresha zile sheria za zamani, tuboreshe ili sasa tuweze kuona ni namna gani kwamba tuta- improve matumizi ya ile reli ili iweze kutumika vizuri zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tulikaa tumekodisha kampuni moja ya wa South Africa ambayo inaitwa Calabash. Calabash ni kampuni ya wastaafu waliokuwa wanafanya kazi kwenye reli ya South Africa kule. Baada ya kustaafu wamenunua vichwa na mabehewa kwa hiyo tumewakodisha ndio wanaobeba mzigo kupitia ile reli, tunawalipa kwa kila trip, kila trip moja wanalipa milioni 20 na bado nafasi hiyo ipo hata Watanzania wengine wanaweza wakafanya hivyo na Calabash wameongeza uwezo wa kubeba mzigo, wanabeba tani 150,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yako mengi ya kuzungumza, lakini nikushukuru kwa kunipa hii nafasi na niwapongeze sana Waheshimiwa Wabunge kwa michango yao. Nawashukuru sana. (Makofi)