Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

Hon. Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Niende moja kwa moja katika kuchangia kwenye Kamati ya Miundombinu, nianze nayo kwanza. Naipongeza sana Serikali kwa jitihada kubwa ambazo imefanya na hasa Mheshimiwa Rais katika kulifufua na kuiendeleza TTCL. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa TTCL ilikwishakufa lakini kwa jitihada na weledi mkubwa wa Rais wetu tumeona sasa shirika hili tayari limekwishafufuka. Ni matarajio yangu kwamba sasa litakwenda kujiendesha kwa faida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili shirika hili liweze kujiendesha kwa faida naishauri Serikali kuona ni namna gani Wizara na Taasisi zinaweza kulipa yale madeni ili pia liweze kuendelea kutoa gawio kama walivyoweza kufanya kwa mwaka jana. Pasipo kulipa haya madeni bado itakuwa ni tatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije katika viwanja vya ndege. Naipongeza pia Serikali na Kamati kwa jinsi ambavyo wametuletea ripoti inayoonyesha jitihada za Serikali katika ujenzi huu wa uwanja wa ndege na hasa Terminal III. Uwanja huu utakapokamilika utapokea kwa siku watu zaidi ya 2,000, hili pia litasaidia kuleta watalii na wageni wengi kutoka nje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nina ushauri kwa Serikali kwa sababu pamoja na jitihada hizi nzuri lakini suala la miundombinu hasa kwa watu wenye ulemavu bado ni tatizo. Katika viwanja vyetu vya ndege hakuna lift ambazo zinaweza kuwasaidia watu wenye ulemavu. Mara nyingi ukienda katika uwanja wa ndege hata ile lift iliyopo wakati mwingine unakuta haifanyi kazi. Kwa hiyo, watu wenye ulemavu, wagonjwa inakuwa shida kufika katika viwanja vya ndege. (Makofi)

Mheshimwa Mwenyekiti, wakati mwingine tumeona kwamba wengine wanalazimika kuwabeba, siyo kila mtu atapenda kushikwashikwa kubebwa kupandishwa kwenye ndege kutokana na ule umbali. Kwa hiyo, niwaombe sana Serikali na hasa Wizara husika kuona ni jinsi gani tunaweka hii miundombinu ili angalau basi na watu wenye ulemavu waweze kufurahia mazingira hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafurahi sana ukifika maeneo mengine kama Dubai unapotua tu kwenye uwanja tayari unakuta kwa mtu mwenye ulemavu miundombinu imeandaliwa na mtu huyu inakuwa ni rahisi kufika eneo ambalo anataka. Kwa hiyo, naishauri Serikali kuona ni kwa jinsi gani wataboresha miundombinu na kwa watu wenye ulemavu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa miundombinu. Naipongeza sana Serikali kwa ujenzi wa miundombinu ambayo tumeona sasa Tanzania yetu ni kwa jinsi gani tunaunganishwa na barabara ambazo zimejengwa. Barabara hizi zitaweza kukuza uchumi, kipato kwa mtu mmoja mmoja lakini kwa maeneo mengi wananchi wataweza kusafirisha bidhaa zao kutoka eneo moja kwenda eneo lingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii itawasaidia wao badala ya kuuza bidhaa zao katika maeneo yale ambayo kwa namna moja au nyingine hawezi kupata fedha ambazo wanatarajia wao lakini wakitoka pale na kwa sababu kwa hivi sasa miundombinu tayari ipo itasaidia sasa kukuza uchumi wa mwananchi mmoja mmoja lakini pia kuongeza pato kwa kwa Serikali yetu kwa sababu itapata kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapo hapo kwenye barabara, naomba tu Serikali kwa sababu nimechunguza na kuona wamejitahidi kuweka alama za barabarani na alama hizi zipo kuhakikisha kwamba hapa kuna watu wenye mahitaji maalum wanataka kuvuka, tumeona sasa hivi zebra zinaheshimika sana. Hata hivyo, maeneo mengi ambapo kuna alama zinazowawezesha watu wenye ulemavu waweze kuvuka bado ni tatizo Watanzania hawaheshimu alama hizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kwa kusema…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)