Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

Hon. Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia ripoti ya Kamati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nipende kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunisimamisha mbele ya Bunge lako tukufu, lakini pia nipende kuipongeza Serikali katika mwaka wake wa fedha 2018/2019 imeweza kutenga kiasi cha shilingi trilioni 4.2 kwa ajili ya sekta ya ujenzi, uchukuzi na mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwenendo huu wa bajeti unakwenda vizuri kwani katika sekta hii ya uchukuzi na mawasiliano ina miradi mikubwa na mingi sana hivyo nipende kuipongeza Serikali…

MWENYEKITI: Waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa Hawa Mchafu ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu, msikilizeni atoe vipande sasa. (Makofi)

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo nipende kuipongeza sana Serikali na niseme tu nipende kuishauri Serikali sambamba na ushauri tulioutoa kwenye Kamati kuhakikisha bajeti inatolewa kwa wakati ili miradi yote ya maendeleo iweze kutekelezeka kwa wakati ikiwa ni ishara ya kupunguza madeni lakini pia kuipeleka nchi yetu kwa kasi iliyokuwa kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kuchangia mchango wangu wa kwanza katika Shirika la Ndege la ATCL, nipende sana kumpongeza Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, ndani ya kipindi kifupi ameweza kununua ndege sita na ndege zingine ziko njiani zinakuja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niseme, hii imewezesha kurahisisha huduma ya usafiri wa anga lakini pia imeongeza idadi ya safari na miruko kitu ambacho kinakwenda kuchochea ongezeko la ajira, ongezeko la watalii nchini lakini pia mapato yanakwenda kuongezeka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nipende kutaarifu Bunge lako tukufu, mnamo mwaka jana mwezi wa nane, Shirika la ATCL lilizindua safari ya kwenda Entebbe - Uganda, lakini Bujumbura-Burundi. Niseme mwezi wa pili mwaka huu tunakwenda kuzindua safari ya kwenda Johannesburg -South Africa, Harare pamoja na Lusaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ni maendeleo makubwa, lakini nipende tu kuishauri Serikali, tumenunua Ndege zetu kwasababu ya safari za ndani, safari za kikanda na safari za kimataifa. Ushauri wangu kwa Serikali ni kwamba mharakishe mchakato uliokuwepo kati ya TCAA ya Tanzania na CAA ya nchini China ikiwezekana hata mtumie Balozi zetu watupe majibu sasa ni lini mchakato unakamilika ili tuanze safari za kwenda Bombay. Sambamba na hilo pia nipende kuitaka Serikali kuharakisha mchakato uliopo baina ya nchi ya China na Tanzania ili kuhakikisha safari ya Guangzhou inaanza haraka iwezekanavyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu mwingine upo katika kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Mwalimu Nyerere. Kumekuwa na changamoto kubwa ya ucheleweshaji kwa malipo ya treasury voucher, hii inapelekea mzigo kukaa muda mrefu bandarini. Hivyo itakumbukwa kwamba gharama za kuhifadhi mzigo bandarini wakati mwingine zinazidi hata ile gharama ya kilichonunuliwa zile bidhaa ama ile mizigo gharama yake inakuwa ni kubwa zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vitu vyote ambavyo vina exemption kutoka kwake ni lazima taratibu wa GN zikamilike. Huwezi kutoa vitu vyenye exemption ya VAT kama GN haijakamilika na ukisema unatoa kwa utaratibu huo unakuwa umevunja sheria. Sasa ninataka niwaombe TRA maana hatuna sababu leo hii tuliuliza kwa nini viti vya uwanja wa ndege vya terminal three mpaka leo havijafungwa? Lakini kwa nini lift ya uwanja wa ndege wa terminal three mpaka leo haijafungwa? Ni kwa sababu tunaambiwa masuala haya ya GN hayajakamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiri, kwa kuwa mnafahamu TRA ule mzigo uko exempted, lakini ule mzigo pia unatakiwa ufike katika terminal three, vyombo vya usalama vipo. Ushauri wetu tunashauri TRA sambamba na vyombo vyetu vya ulinzi na usalama ikibidi hata muwa-escort mfike mpaka eneo husika wakati vinafungwa mpo, mnashuhudia kwamba kweli huu mzigo ama hizi bidhaa ni kwa sababu ya terminal three. Hatuna sababu ya kuchelewa kwa sababu ya masuala ya GN, wakati sisi huku tunaendelea na hizo process za GN huku zinaendelea. Kwa kufanya hivi tutaharakisha ama tunahatarisha process ya mkandarasi kuongezeka anapata muda, muda wa mradi unakuwa ni muda mrefu zaidi muda ule wa kukamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu mwingine uko kwa Shirika la Posta Tanzania, Shirika la Posta lina changamoto kubwa ya kulipa pension ya wafanyakazi. Mpaka mwezi Juni, 2018 imelipa tayari shilingi bilioni 4.9 pasipo Serikali kuwarejeshea lakini wakati huo huo TRA inawadai Shirika la Posta deni la shilingi bilioni sita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, deni hili limetokana na kipindi kile Posta inashindwa kujiendesha ama inashindwa kufanya biashara vizuri. Kilichopo hapa baba anamdai mtoto na mtoto anamdai baba. Kwa kuwa Shirika letu la Posta limeanza kuimarika na kwa kuwa Shirika letu la Posta liko kwa ajili ya kufanya biashara kushindana na akina DHL, kushindana na wakina Forex, ushauri hapa tunaoutoaWizara ya Fedha na Mipango ikae chini na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Miundombinu waangalie namna bora aidha ya kuwaondoshea hili deni ama kama siyo kuwaondoshea hili kuwapounguzia hili deni kwa sababu Shirika la Posta linaidai Serikali na Serikali inaidai Shirika la Posta. Kwa hiyo, naomba sana Serikali iliangalie hilo ili tuweze kusaidia Shirika la Posta lisimame vizuri na liweze ku-compete na Mashirika mengine ya Kimataifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu mwingine utakuwa kwa Shirika la Kampuni ya Meli (MSCL), nipende kuipongeza sana Serikali katika mwaka wake wa fedha 2017/ 2018 ilitenga takribani shilingi 24,496,000,000 kwa ajili ya ununuzi wa meli mbili mpya. Tuna kila sababu ya kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa jinsi anavyoikimbiza nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, shilingi bilioni 24 tayari zimeshatolewa na kilichokwenda kufanyika mpaka sasa tumeshalipia ama imeshalipiwa advance payment kwa sababu ya chelezo. Lakini pia nyingine niseme wamelipa advance payment ya kuanza kujenga meli mpya na advance payment nyingine imetolewa kwa ajili ya ukarabati wa MV Victoria na MV Butiama kwa ajili ya Ziwa Victoria. Kwa hiyo, haya ni mapinduzi makubwa sana tuna kila sababu ya kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kikubwa kile anachokifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru sana, naunga mkono hoja.