Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

Hon. James Kinyasi Millya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Simanjiro

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

MHE. JAMES K. MILLYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze kwa kunukuu kitabu ambacho asubuhi tumeambiwa kinauzwa pale nje na Mheshimiwa Spika kwa sababu wengine wanapenda sana kunukuu vitabu vya nje, lakini hapa ndani wanaviacha wakijidai kama hawaoni, naomba nianze kunukuu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitabu chenyewe kinaitwa Corruption in Agony, Contemporary Nyerere of our time, by Jacob Roman Lubuva. Kinaanza hivi naomba niendelee; “many people in Africa in beyond consider the President’s personal character, attitude and leadership style peculiar to his predecessors. Some equate his leadership qualities to leadership ethos of the founding father of Tanzanian Nation, his excellent, the late Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Some commentators have yet compared President Magufuli to some known architects of African Nations like Kwame Nkurumah and Nelson Mandela with reference to his hate of corruption, a sense of self-reliance and pro-poor attitude.” (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini anaendelea, “The President remarkable achievement immediate and radical pro-citizen’s socio-economic transformations and unprecedented fast truck of political campaigns. Consequently, the President has been and presence of pre- electric and social media global being committed.”Mwisho wa kunukuu.

Mheshimiwa Zitto…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Zitto…

MHE. JAMES K. MILLYA: …mimi najua Kimasai vizuri na unajua hilo, lakini Mheshimiwa Zitto wakati fulani nilipokuwa Rais wa Chuo Kikuu cha Tumaini ulikuwa mtu wa kawaida/ Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kwa hiyo, unajua kwamba najua kiingereza vizuri, najua kimasai na kiswahili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee kwa kuanza hili, Mheshimiwa Rais amefanya mikutano miwili; mmoja, Ikulu kuhusu wafanyabiashara Tanzania nzima, lakini bado Mheshimiwa Rais juzi alifanya mkutano na wachimbaji wa nchi nzima wadogo wadogo kuhusu biashara ya madini. Lakini wenzetu hawa kwa sababu hawaoni na hawataki kutambua, bado wanaponda nguvu za Mheshimiwa Rais. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nimetaja rushwa? Kampeni za wenzetu mwaka 2002, 2005, 2010 walisimamia ajenda ya rushwa, rushwa, rushwa! Ametokea mtu ambaye anapigana dhahiri kwa ajili ya rushwa kwa sababu hawa wafanyabiashara siyo wengi wazuri. Ukiona mtu anatoa mapovu kuwatetea ujue inawezekana amerambishwa kidogo, lakini ukweli ni kwamba wengine na naomba nieleweke vizuri, siyo wafanyabiashara wote wabaya, lakini kuna wafanyabiashara kweli imedhihirika pale mfano, madini pale airport, Tanzanite wameshakamata zaidi ya watu wengi wanaiba madini, na hao unawatetea? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni Mbunge wa Jimbo la Simanjiro, naomba nitoe takwimu za Tanzanite tangu ukuta huu uwekwe mambo ambayo yalikubalika kuhusu Marekani miaka hata kabla ya mimi kuanza shule ya msingi. Ukuta huu Mheshimiwa Dkt. Magufuli baada ya kuona kwamba madini yetu yanaibiwa sana akaamua kuweka ukuta. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa kwenye Kamati Teule ya Bunge leo hii watu wa Mererani na hii kauli ichukueni, watu wa Mererani wanapendelea ukuta, wanafurahia ukuta, madini yameongezeka bei. Mimi ni Mbunge, kauli hii inaweza ikanihukumu mwaka 2020 lakini uhakika watu wangu wanafurahia ukuta. Ukuta hauna shida na ukuta nauunga mkono sana, kwa hiyo, watu wengine wanaokuja kuongea kuhusu ukuta hiyo waache kabisa kwa sababu ukuta uko sawa sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna kitengo kinaitwa TANTRADE kwenye Wizara ya Biashara. Mheshimiwa Rais juzi juzi hapo aliwaambia watu hawa hawasaidii Serikali yetu vizuri kabisa. TANTRADE inaongozwa na mtu anaitwa Edwin, naomba nitoe ushuhuda, kuna EXCO itafanyika China mwaka huu. Kuna vijana wa Arusha wameomba kuhudhuria na wanasema Serikali hatutaki hata shilingi moja kwenu. Wameomba tangu mwezi wa Oktoba, 2018 mpaka leo isingekuwa Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje juzi Arusha, isingekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara huyu kijana asingesaidiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe, watu wetu hawa ambao wamepewa dhamana ya kuwasaidia Watanzania kukuza biashara zao wawasaidie kweli kweli. Niombe kitengo hiki cha TANTRADE kiangaliwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwani vita ambayo saa nyingine Mheshimiwa Dkt. Magufuli anapigwa ni ya nini? Ni kwa sababau kama Mheshimiwa Dkt. Magufuli anaingilai interest ya Wamarekani, interest ya Wabelgiji, interest ya Wajerumani kwa sababu wafanyabiashara wao wamesimamishwa na Canada na wengine ndiyo maana wanasukuma. Ninaomba Serikali yangu tuwaangalie wafanyabiashara tuwasaidie haswa, tuwasaidie, tuweke mifumo rafiki ya kusaidia wafanyabiashara kwa sababu nchi hii kiuchumi tutafahamika tu kama ni wazuri kama tuki- compete mfano na Kenya na nchi nyingine kiuchumi. Ninaomba nia njema ya Mheshimiwa Rais kwa kuita ile mikutano miwili ipo, ninaomba watu ambao wanasaidia kwenye kitengo cha biashara wasaidie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilisikitika asubuhi sana, kama mtu anataka maamuzi ambayo yanafanywa kwenye nchi na yanufaishe na watu wa Msumbiji nilisikitika kidogo. Mheshimiwa Zitto nikikosea ni faida yako wewe mpinzani kwa hiyo wewe ninaomba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, issue ni moja, kama Serikali imepitisha bei elekezi kwa ajili ya korosho kuwaokoa watu wetu wa kawaida, kwa nini mtu mmoja ambaye anajua…

Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wa kangomba utawafahamu tu. Na ni kweli wangependa korosho ya Mozambique inunuliwe ili ya watu wetu isinunuliwe waanze kupiga kelele ndiyo nia yao. Lakini hujuma hiyo imeshafahamika na hakika hamtaweza kufanikiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe Wizara husika, biashara ni muhimu sana na Mheshimiwa Rais ana nia njema sana. Niombe kama ikiwezekana Bunge hili liweze kuunda Kamati Maalum ya Wafanyabiashara ambayo inaweza ikasaidia kumuongoza Mheshimiwa Rais na Mheshimiwa Waziri kutanzua matatizo ya kwenye sekta hii ya biashara, ningeomba sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaona, naomba niwasilishe, ahsante sana. (Makofi)