Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

Hon. Godbless Jonathan Lema

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arusha Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Nitaongea mambo serious, naomba wale watu wenu ambao mmewapanga kwa taarifa waniache nisikilizwe na Serikali ili muweze kulisaidia Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kwamba mazingira ya kibiashara Tanzania yamekuwa magumu sana. Mfanyabiashara yeyote ili aweze kuwekeza anahitaji kitu kinachoitwa confidence. Katika Taifa hili na nimekuwa nikisema mara nyingi na nimemwambia hata personal Mheshimiwa Mpango, mitaji inayohama na watu ambao wana-reallocate biashara zao katika mataifa mengine ya jirani, ukiniambia nikutajie kwa namba makampuni ambayo yanaondoka ni mengi sana. Huwezi kujenga uchumi wa taifa bila kuimarisha private sector. Kiungo muhimu kabisa katika taifa ni private sector. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo katika Jimbo langu la Arusha Mjini kwenye kikao cha kodi ambacho tulikaa mwezi huu ulioisha, watu walio-register kufunga biashara walikuwa ni 650. Ukifanya utafiti wote hawa kitu kinachowasabishia wafunge biashara ni ujasiri katika kuwekeza katika taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hapa zinakuja takwimu za uongo juu ya ukuaji wa uchumi lakini wote ni mashuhuda na wewe ni shuhuda kwa sababu ni Mbunge wa Jimbo la Mjini kabisa Dar es Salaam ya kwamba purchasing power ya Watanzania ime-decline katika kiwango cha hali ya juu. Kwa bahati mbaya sana mnapokuja humu ndani kuongelea inflation kwamba imeshuka mnashindwa kutofautisha inflation na kuanguka kwa soko. Kinachoendelea mitaani ama kinachoendelea katika biashara za bidhaa ni kwamba nguvu ya manunuzi imeshuka na kwa sababu nguvu ya manunuzi imeshuka maana yake ni kwamba watu wanashusha bei bidhaa ili angalau waweze kuuza vitu vyao waepuke hasara ya moja kwa moja sasa huku mkija mnasema ni inflation imeshuka. (Makofi)

T A A R I F A

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, twende kwenye Sera ya Viwanda. Bunge lililopita nilisema hapa kwamba viwanda havijengwi kwa kauli mbiu vinajengwa kwa mazingira wezeshi na mazingira hayo wezeshi wanafanywa na Serikali kwa watu. Leo Sera yenu ya Viwanda 100 kila Mkoa nikiomba Bunge hili Mheshimiwa Waziri aoneshe viwanda viwili, hamuwezi kuonesha. Unajiuliza Serikali hii ambayo inapigia kelele viwanda, inakwenda kupunguza bajeti ya kilimo na wakati kilimo ndiyo malighafi ya viwanda, unajiuliza hawa watu wako serious na viwanda ama ni kelele tu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini viwanda vinasababishwa na demand, hakuna Mtanzania aliyepiga kelele spirit zitengenezwe, pombe aina za spirit zimetengenewa kwa sababu ya demand. Kwa hiyo, ili viwanda viweze kutengenezwa, ili traders waweze kufika kwenye hatua ya kuona viwanda ni vitu muhimu kinachopaswa kufanyika ni watu wawe na mazingira mazuri, uchumi ukue, mishahara bora, kuwepo na purchasing power ili nguvu ya manunuzi ikawaambie wafanyabiashara kwamba kwa hali hii sasa mimi naona sihitaji kuagiza tomato kutoka India nahitaji kuwa na kiwanda cha tomato Iringa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mazingira ya biashara yanatengenezwa na hali nzuri (harmonization) pamoja na demand na hiyo demand wa kwanza kuitengeza ni Serikali. Sasa Serikali yenu imeua workshop, Serikali yenu inawatanzama wafanyabiashara kama maadui, ma-DC na Wakuu wa Mikoa wanaumiza wafanyabiashara, wafanyabiashara wanawekwa ndani. Mheshimiwa Lukuvi kila anapokwenda ananyang’anya watu mashamba, Sheria na Sera ya Ardhi ni mbovu, leo nani anakuja kuwekeza Tanzania mahali ambapo Sheria ya Ardhi inasema ardhi ni mali ya Serikali. Hivi ni nani leo atakuja kufanya investment ya dola bilioni 50 …

WABUNGE FULANI: Aaaaaa.

T A A R I F A

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ni tatizo kubwa sana kuwa na viongozi wanaokuja ndani ya Bunge wakiwa wamelewa, ni tatizo kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana unilindie muda wangu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nasema ukiangalia namna Taifa linavyoenda sasa, anzia ma-DC na ma-RC na wote ninyi Waheshimiwa viongozi hapa ni mashuhuda wa behavior za ma-DC na ma-RC kwa wafanyabiashara, hiyo sasa imesababisha watu na viwanda kuondoka. Nilisema katika Bunge hili utajiri ni prestige, kama mimi nakuwa na fedha halafu fedha yangu inakuwa ni adhabu maana yake nitatafuta mahali ambako nina amani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee General Tyre ambayo Kamati yetu imefanya conclusion vizuri sana. General Tyre toka imefungwa ni miaka mingi sana. Nimekuwa kwenye Kamati wakati wa Bunge la Mheshimiwa Makinda, tukaongelea kuhusu General Tyre, leo tunavyoongea General Tyre bado haijafunguliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, demand ya tairi nchi hii ni kubwa katika kiwango ambacho hatuhitaji kiwanda cha matairi Arusha peke yake, tunahitaji viwanda vya matairi zaidi ya viwanda hata kumi. Leo tairi nchi hii zinatoka China, Taiwan, Japan, Marekani na Ujerumani. Hii demand yote ya matairi ndani ya nchi, nchi hii ingekuwa serious, kiwanda cha matairi kisingekuwa mpaka leo hakipo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumetoa ushauri kwenye Kamati pale kilipo kiwanda cha General Tyre ni katikati ya makazi, ni elite area, ni karibu heka 70, ukiweza kuuza heka moja pale ni karibu shilingi milioni 300 ama shilingi milioni 400 kwa mnada kwa sababu ni eneo prime. Maana yake ni nini? General Tyre ukiithamanisha kuwa pesa leo pale katikati Arusha ni zaidi ya shilingi bilioni 28 mpaka bilioni 30. Kiwanda cha matairi hakihitaji dola milioni 15 au 20 kuanza. Maana yake ni nini? Mtaji ni eneo lile kuligeuza kuwa pesa, nendeni kwenye maeneo ya EPZ yaliyoko katika Mkoa wa Arusha chukue zaidi ya heka 500 au 100 tafuteni mwekezaji atawakuta na ardhi na pesa, kiwanda tayari kitafunguliwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa bahati mbaya huku watu mme-operate manual, watu huku mna-operate kwa woga, mkiingia kwenye vikao mnashindwa kuongea mmekuwa waoga, mmepandikizwa hofu, mnashindwa kuwaza kisasa, mnashindwa kuwaza kibiashara. Ndiyo maana leo hata maana ya broker kuwa katika biashara mmeshindwa kujua. Mnashindwa kuwawezesha ma-broker kwa kuwapa leseni, mnashindwa kuwarasimisha ma-broker kuwapa mizani, leo mnakwenda kutafuta broker Kenya! Ni kijana mmoja kutoka Kenya ana kampuni yake ya thamani ya dola 1,000 za Kimarekani, amevaa suti, amekuja na caravan na wapambe Mawaziri wote mmekimbilia Arusha kwenda kusaini mkataba na broker Kangombo. Kangombo kutoka Kenya amekuwa wa maana kweli kwa sababu tu amekuja suti na private jet, Mawaziri wote mkaacha kazi mnapigwa na style, kwa sababu hamuwazi kimkakati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Watanzania wanafikiria ninyi mnaweza mkawa solution ya nchi hii, waone mawazo yenu na waone michango yenu. Hata angalia dressing style tu ya Mheshimiwa Waziri wa Viwanda na Biashara utajua kabisa huyu hawezi kuleta transformation yoyote katika uchumi wa Taifa hili. (Makofi/Kicheko) [Maneno Haya Siyo Sehemu ya Taarifa Rasmi za Bunge]

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nachosema ni nini? Nachosema ni kwamba biashara haihitaji nguvu, biashara haimhitaji Sirro, uchumi haumuhitaji Sirro, uchumi hauhitaji nguvu. Maduka ya Forex Arusha yamefungwa mpaka leo. Hivi kweli ninyi mna Usalama wa Taifa unawambia...

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa
Mwenyekiti, kuhusu utaratibu.

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, leo...

KUHUSU UTARATIBU

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hata huyu anayemalizia kuongea ukiangalia koti lake linaweza likatoa suti za...

MWENYEKITI: Mheshimiwa Lema, endelea na hoja yako.

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niongelee suala la Benki Kuu na maduka ya kubalisha fedha Arusha. Leo navyoongea hapa hakuna duka la kubadilisha fedha za kigeni Arusha linalofanya kazi na Arusha ndiyo center ya utalii katika Taifa hili. Ukitaka kubalisha fedha ya kigeni Arusha Mjini ni lazima uende Kilimanjaro Moshi. Sasa hawa watalii wanaokuja Arusha wanataka kununua bidhaa ndani, wanataka ku-spend unampeleka benki ya NMB, CRDB akapange foleni, anasubiri kubadilisha fedha, mazingira magumu kama haya yanasababisha wale wanaotafuta watalii yaani tourist operator wa-shift destination kutoka Arusha na Tanzania kwenda Kenya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, utakuja kuniambia katika Bunge la bajeti high season ya kipindi hiki watalii watapungua wengi sana kwa sababu ya matatizo mengine lakini hata hili la kubadilisha fedha. Unajiuliza, hivi inachukuaje miezi miwili kupata solution ya kurudisha maduka ya kubadilisha fedha yaanze kufanya kazi kama kawaida? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo wamenyang’anywa fedha na wakienda kudai anaambiwa ukiendelea kudai tutakupa money laundry. Kwa sababu kuna ushuhuda wa watu wameteseka na kesi hizi watu wanaamua kuacha kudai fedha zao. Maduka haya kuna Sheria za BoT, sheria hizo zina faini pengine na vifungo, hatujasikia mtu mmoja anapelekwa Mahakamani leo ni mwezi wa pili maduka Arusha yamefungwa. Maduka mengine mmefunga mnasema eti Lema ana Bureau de Change kumi namwomba Mungu anisaidie niwe nazo yaani kama mna Usalama unawaambia mimi Bureau de Change kumi, mnakuja kufunga maduka ya kubalisha fedha eti mimi nina maduka, huo Usalama unawaingiza chaka sana maana yake haujui kitu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tanzanite hapa inakufa, mmem-mislead Mheshimiwa Rais tanzanite haichungwi na ukuta, rushwa ni attitude, mtaweka ukuta na kamera wale askari mnaowalipa 700,000 kwa mwezi tutawapa milioni 50 yatapita mawe bilioni moja, fikirieni vizuri. Leo mnasema mnaweka na kamera, tena mmesema kamera ziwekwe bila tenda. Kila mgodi Mererani una fensi, akili ilikuwa ni nini, kama mngekuwa hamuwazi manual, ni kila mgodi mnatoa standard ya kamera, mnaweka internet ninyi, mna monitor migodi yote kutoka Dar es Salam na kutoka Arusha bila ninyi kuweka kamera. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niko hapa naangalia nyumbani nikiwa Dodoma, usiku naamka naangalia nyumbani kwangu, namwambia mke wangu nje kuna watu ponyeza alarm, ita mlinzi, sasa ninyi mnashindwa kuwaza hivyo tu, leo mmepiga ukuta hakuna mawe, sasa hapa itakuwaje, Mheshimiwa watakuwa wanaiba, weka kamera bila tenda, mnaweka kamera bila tenda! Kila mgodi una ukuta, weka kamera, weka mtu pale, TRA wako pale, mgodi ukitoa mawe siyo siri kila mtu huwa anajua, Arusha nzima huwa inajua, maana yake ni kwamba TRA watakwenda pale sasa leo mmeweka ukuta hausaidii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mgodi siyo duka la mkate, mawe hayatoki kila siku. Mwanzo mgodi ulitoa mawe mkakusanya shilingi milioni 800 mwezi unaokuja migodi haikutoa mawe mkamfukuza na Mheshimiwa Angellah, mkakusanya sijui 500,000. Mikataba tunaibiwa, lile siyo duka la mkate ama la colgate kwamba mawe yanatoka kila siku. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nilivyokuwa mdogo kaka yangu alikuwa anahudumia mgodi. Nikawa mkubwa, nikawa Mbunge nikahudumia mgodi, nikawa Mbunge kipindi cha pili mgodi ukahujumiwa hatukuwahi kupata hata chembe moja ya mawe. Sasa ninyi mkikaa kule…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa mzungumzaji)

MHE. GODBLESS J. LEMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)