Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

Hon. Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa mwaka 2018

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza nataka kusema kwamba sisi wapinzani hatuna ugomvi na ATCL, hatuna ugomvi na ndege; ndege ni zetu na ATCL ni yetu, tunapokosoa, tunaposema ni kwa ajili ya kulifanya shirika liwe na nguvu zaidi kiuchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mambo yangu matatu nitakayozungumza, nianze kuondosha dhana ambayo inazidi kukua kwamba kukiwa na shirika la ndege ni huduma, hii sio sahihi na kwa bahati mbaya tunapandikiza fikra kwa Watanzania ambao baadaye shirika likifa itabidi tuwajibu kwa sababu kama ambavyo tulikuwa tunasema viwanda vingine ni huduma, viwanda kwa maelfu au kwa mamia vimekufa na faida yake hatukuiona.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili ni kwamba, tunapandikiza fikra mbaya kwa watendaji wa shirika letu, kwamba wao hawalazimiki kuliendesha shirika kibiashara, hiyo ni wrong concept. Shirika ni sustainability na profitability, kama hamkufuata hivyo shirika linakufa, pesa ya umma inapotea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ethiopian Airlines – moja ya mashirika ya mfano hapa mitaani kwetu; Ethiopian Airlines mwaka wa fedha 2016/2017, walitengeneza faida ya Dola bilioni 233, mwaka uliofuata yaani 2017/2018, wakatengeneza faida ya dola bilioni 229, wakajiuliza wameshuka kwa bilioni nne, wamefanya inquiry kwa nini wameshuka kwa bilioni nne, sio kwamba wamejiachia tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tusijenge dhana ya kujiachia kwamba ni service, kwa sababu hatimaye shirika likifa tutakuwa na tatizo, kwa hiyo tuiwekee target management ya ATCL kwamba lazima katika muda fulani mfikie lengo fulani. Hilo la kwanza. La pili ni kwamba, lazima wawe na business program ambayo inaonesha wanatoka hapa watafika hapa na growth iwe inaonekana mwaka hadi mwaka, tukiwaachia na kuwajengea dhana kwamba ni huduma tu, basi tutafika pabaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili nimelisikia leo na nimefurahi, juu ya Uwanja wa Ndege wa Songwe. Siku zote nasema kwamba nchi nzuri haiwezi kuwa na gateway moja tu katika nchi yao, inabidi watengeneze gateways nyingi kwa suala la ndege. Uwanja wa Ndege wa Songwe ni gateway yetu ya kusini, tunaweza tukatawala na tukatengeneza biashara kusini ikiwa tutajipanga vizuri kwa uwanja ule, lakini leo nimesikia kwamba angalau sasa tenda imetangazwa ili kuweka taa katika Uwanja wa Songwe ili iwe getaway yetu ya kusini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Mwanza ni gateway yetu ya Maziwa Makuu, Mwanza ikitumika vizuri ni mahali pazuri sana pa kuweza kutumia kuingia Maziwa Makuu, lakini sioni athari ya kiuchumi ya kujengwa uwanja mkubwa Chato. Nimekuwa najiuliza; hivi Chato ni gateway ya kwenda wapi kwetu sisi? Unaweka kiwanja pembeni ya nchi, hakuna utalii, hakuna biashara ya hivyo, halafu unatumia pesa nyingi badala ya kuimarisha viwanja ambavyo ni gateway…

T A A R I F A

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, siipokei taarifa yake kwa sababu ni ndoto tu anayoyasema.

MWENYEKITI: Endelea na mchango wako.

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nafikiri kwamba tungeweza kuwekeza zaidi katika maeneo ambayo yangeweza kuwa na maana kwetu sisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ninalotaka kuzungumza ni kujaribu kui-turn…

T A A R I F A

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubali taarifa hiyo na Mji alioujengea unaitwa Gbadolite na ni kweli kwamba kumekuwa na makazi ya popo na njiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine linaloifanya Dar es Salaam Airport…

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Musukuma.

T A A R I F A

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa imekataliwa kwa sababu udhahiri umejengwa kwa ajili ya upendeleo tu, hakuna kingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kusema kingine ni kuutengeza Uwanja wa Ndege Dar es Salaam uwe ni hub. Sasa hivi utakuta mtu akitaka kwenda Moroni, akitaka kwenda Seychelles, akitaka kwenda Mauritius…

MHE. JAMES K. MILLYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Millya, kaa chini.

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo naishauri Serikali…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)