Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Dr. Philip Isdor Mpango

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nakushukuru sana, kwa kunipa hii fursa niweze kuchangia kwenye hoja zilizotolewa, lakini nitangulize pongezi zangu za dhati kabisa kwa Kamati ya Bajeti na Mwenyekiti wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia PAC na Mwenyekiti wake, kwa kweli taarifa ni nzuri zina afya, na naamini kabisa zitatusaidia kuendelea na juhudi za kuboresha uchumi wa Taifa, lakini pia zitatuwezesha, kuimarisha utekelezaji wa bajeti kwa kipindi cha mwaka kilichobaki. Na naamini pia kwa upande wa PAC ushauri wao utatusaidia kusimamia utendaji wa Mashirika yetu na yale ambayo yametolewa kama ushauri na Waheshimiwa Wabunge waliochangia niwaahidi kwamba tutayafanyia kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa baada ya maneno hayo ya utangulizi, niseme kidogo, nikianza na lile ambalo alilieleza Mheshimiwa Balozi Kamala. Ni kweli kabisa kabisa, naungana naye, uchumi wetu umekuwa unakuwa kwa kasi na dunia yote inajua hivyo, sio tu kwamba ni jambo jema, lakini ni lazima tuhakikishe kwamba uchumi wa Taifa unaendelea kukuwa kwa kasi kubwa zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini naungana naye pia kusema ni muhimu tuelekeze pia nguvu kukuza sasa size ya keki yenyewe, ametoa takwimu nzuri. Lakini ni vyema tukumbushane tunakotoka nchi yetu tunatoka kwenye kauchumi kadogo sana, kwa mfano mwaka 2000 GDP ya Tanzania ilikuwa ni dola bilioni 10.1 tu, sasa ndani ya miaka 15 kufikia 2017 uchumi wa Taifa umefikia dola bilioni 52. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo unakuwa haitoshi kwa hakika, ukilinganisha na takwimu na zile alizokuwa anasema kwa nchi kadogo kama Ubelgiji ni kweli, lakini msingi wake ni lazima tubadilishe sasa structure ya uchumi wetu, ili twende zaidi kwenye viwanda, twende zaidi kupanua pia huduma ambazo kama Taifa tuna fursa kubwa au comparative and competitive advantages. Kwa hiyo, nilitaka tu niungane na Mheshimiwa Dkt. Kamala na njia aliyosema ni sahihi, sio tu tuwekeze kama tunavyofanya kwenye Standard Gauge Railway tuwekeze kwenye umeme mkubwa ambao ndio msingi wa kujenga viwanda, tuwekeze kwenye skills za Taifa letu, lakini pia twende kwenye maeneo kama tourism ambayo itatupatia nguvu zaidi ya kuendelea mbele kama Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la pili ambalo ningependa kulisemea kidogo ni baadhi ya maeneo ambayo aliyasema Mheshimiwa Silinde, nilidhani ametoka sasa namuona, kwanza tu nisisitize wazee wetu walitufundisha mtegemea cha nduguye anakufa fukara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ni muhimu sana kama Taifa, na hapa huwa siendi kwenye siasa za vyama, very seriously kama Taifa tusipofika mahali tukasimama, tukajitegemea, tukaendelea kutegemea hawa wajomba wa enzi zile, hatutakwenda, hatutakwenda kabisa. Kwa hiyo, kwa hili ningeomba sana Waheshimiwa Wabunge, tuungane kuhakikisha kwamba hatua zote ambazo Serikali inachukua hivi sasa, ili tujitegemee, kweli tunashikamana ili twende mbele kama Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sijui nisemeje, mimi ambaye nakwenda kuomba kwa niaba ya Taifa ninadhalilika mno, ninadhalilika mno, tumekaa na mradi wa Stiegler’s ili tupate umeme wa kutosha kwa muda mrefu mno. Lakini hivi sasa, wao ndio wanataka watufundishe darasa kwamba sisi ndio hatujui maana ya mradi ule, haiwezekani, haiwezekani hata kidogo, wala hatutakubali na wala hatutakubali,. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Mheshimiwa Silinde kupitia meza yako nataka tu nimkumbushe kwamba uandaaji wa takwimu za Pato la Taifa na ukuaji wake, unaenda kwa ngazi na inanishangaza kidogo kwa sababu Mtakwimu Mkuu wa Serikali alitoa mada kwa Kamati ya Bajeti namna ya kukokotoa takwimu za Pato la Taifa na mimi nilidhani si tulikuwa tumejitahidi kumuelewesha namna ambavyo tunafanya. Zipo zile za robo mwaka lakini, takwimu za robo mwaka zinakuwa zile ambazo baadhi ya vitu, havijapatikana sawasawa. Kwa hiyo, kwenye robo ya pili inayofuata unakuwa una takwimu nzuri zaidi, za robo iliyotangulia. Kwa hiyo, inawezekana kabisa kwamba takwimu ambazo tumetoa robo iiyotangulia tunapokuja robo ya pili, tukawa tumepata taarifa nzuri na kuzipitia zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sio kitu cha ajabu kabisa ukokotoaji wa pato Taifa, na kama utapenda tena turudie tuko tayari kurudie tukupeleke polepole polepole ili uweze kuelewa pato la Taifa linavyokokotolewa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ila alinishangaza kidogo kama mwanafunzi wangu wa uchumi aliposema kwamba kama mfumuko wa bei, unateremka kwa nini bei hazipandi, ilinishangaza kidogo, sijui labda nikirudia kwa lugha nyepesi, mfumuko wa bei, ni kama gari linalotembea unaweza ukaamua kutembea kwa speed 100, unaweza ukaamua kutembea kwa speed 40 kwa hiyo tunaposema mfumuko wa bei, umeteremka, hatusemi kwamba bei nazo zimeshuka, tunachosema ni kwamba kasi ya ongezeko la bei limepungua, ndio maana yake, sasa sijui nitalieleza kwa lugha ipi zaidi ili lieleweke. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme kidogo juu ya mchango wa Mheshimiwa Bashe, nafikiri saa nyingine anakuwa anatumia macho ambayo ni-bit pessimistic. Kwa sababu ni kweli, ukiziangalia zile takwimu, kwa nusu mwaka ambao tulikuwa tumetazama, export nyingi hasa zile za tradition zimepungua. Lakini sababu moja kubwa kwa mwaka huu ni kwa sababu ya tatizo la korosho tulilokuwa nalo na mimi naamini kabisa kwamba tutapata matokeo chanya baada ya muda si mrefu, kutokana na hatua ambazo zinaenda kuchukuliwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini namshangaa pia kwamba baadhi ya mauzo yetu nje kuna component zinaongezeka upande wa bidhaa za viwandani ni wazi kabisa zimeongezeka. Lakini pia baadhi ya bidhaa ambazo sizo za mauzo yetu ya asili nazo zimeongezeka, lakini la msingi ambalo nilitaka kusisitiza hapa, tumefanya mabadiliko makubwa katika uendeshaji wa biashara nchini ili kuirejesha nchi kwenye misingi halali na ya haki ya kufanya biashara. Sasa ni lazim utarajie kwa sababu biashara ni cyclical biashara sio kwamba kila saa, basi wewe utakwenda tu biashara mauzo yanaongezeka hayapungui hata kidogo, haiwezekani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo pamoja na kuwa tunaendelea kulitazama, niliiambia Kamati ya Bajeti kwamba tayari tumeunda timu pale Wizarani ili tuangalie mwenendo wa mauzo yetu nje kwa kipindi kirefu zaidi ili pale ambapo kama kuna structural problems tuweze kuzishughulikia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ulitolewa ushauri kwamba Kariakoo ilikuwa ndicho kituo kikubwa cha biashara na hususan tumeshauriwa tutazame sana soko la Congo na Zambia. Ni kweli kabisa na pengine labda hoja iwe kwamba tuongeze kasi katika kulitazama. Lakini kwa mfano dhamira ya Serikali ya kujenga Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa Songwe maana yake ilikuwa ni hiyo, kwamba tuweze kupata wasafiri kutoka Congo, Zambia, Malawi na nchi nyingine zinazozunguka mpaka Zimbabwe, kwa hiyo sio kwamba tumefumbia macho soko hili hata kidogo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jitihada ambazo zinafanyika kujenga Bandari ya Karema zinaelekea huko huko, lakini pia hata hatua ambazo tumefanya kujaribu kuimarisha management ya TAZARA, lakini pia TRA na bandari wamekuwa wanafanya ziara Congo na Zambia ili kuweza kuhakikisha kwamba tunashughulikia zile changamoto ambazo wafanyabiashara kutoka nchi hizo wanakumbana nazo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Bashe pia nadhani nilimsikia akisema ni muhimu kwamba hatua zetu za kibajeti zijielekeze pia kwenye uzalishaji. Nakubaliana naye na nafikiri ndiyo sababu tumekuwa tunaelekeza zaidi fedha kwenye miundombinu ambayo itatuwezesha kuchangamsha uchumi wa Taifa zaidi kuliko ilivyokuwa hapo nyuma. Lakini hata kwa upande wa mabadiliko ya Sheria za Kodi ni wazi kabisa kwamba kupitia bajeti iliyopita, ndiko tulipojielekeza huko kuhakikisha kwa mfano kwamba tunapunguza kodi ya mapato (income tax) kwa ajili ya viwanda vipya mfano upande wa ngozi, lakini pia kupunguza ushuru wa bidhaa kwenye baadhi ya viwanda ambavyo vinazalisha kwa kutumia raw materials za hapa ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)