Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Peter Joseph Serukamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami niwapongeze sana Mwenyekiti wa Bajeti na Mwenyekiti wa PIC kwa ripoti yao. Pia niipongeze Serikali kwa kazi kubwa wanayofanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri Mkuu wa Malaysia alivyoshinda uchaguzi juzi Mahathir akiwa na miaka zaidi ya 90 aliulizwa swali moja, utafanya nini ili kuendeleza maendeleo ya Malaysia. Alijibu jambo moja tu alisema kazi yangu ni kuhakikisha asilimia 24 zinaendelea kuwepo. Maana yake ni nini? Anasema kila biashara iliyoko hapa nchini kwetu Serikali inapata asilimia 24. Kwa hiyo maana yake sisi ni shareholder wa kila biashara. Nami ningetamani niwaombe wenzangu Serikalini tuseme kila biashara ya Tanzania, sisi tuna asilimia 30. Kwa hiyo tunalo jukumu la kulinda hii asilimia 30 iendelee kuwepo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu gani nasema haya, nasema biashara ikienda vizuri, kama kodi tumefika asilimia 88, tutafika asilimia 100 tutafika asilimia 180, hivi jambo likiongezeka ni mbaya? Kuna ziada mbaya kweli jamani. Mimi niwaombe wenzangu Serikalini tuanze kubadilika kwamba wafanyabiashara ni partners wetu. Wafanyabiashara ni partners wa Serikali hii. Ninayo mifano ya makampuni mengi sana ambayo ukiangalia kodi wanazolipa, ukiangalia wanavyoajiri watu, wanaleta fedha nyingi kwenye uchumi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, iko tabia imeanza kukua kwamba tunadhani wafanyabiashara ni wezi, ni wahuni, ni watu wabaya, maneno haya yanasemwa na viongozi, hili siyo sawa. Juzi Mheshimiwa Rais amesema tunawahitaji wafanyabiashara. Kwa hiyo ningeomba na wale wengine ambao mnamsaidia Mheshimiwa Rais muanze kuona umuhimu wa wafanyabiashara. Leo Kariakoo imekufa, nitasema sababu chache za Kariakoo kufa. Ya kwanza ni tariff, Serikali yetu wafanyabiashara wadogowadogo anaenda India, anaenda China analeta glass ya shilingi elfu moja na kuna glass ya shilingi elfu kumi, akija mtu wa kodi anasema glass zote hizi ni shilingi elfu kumi, lakini watu wengi wanatumia glass za shilingi elfu moja matokeo yake commoditie zinazokuja ni bei ghali na matokeo yake watu wanaondoka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili angalia, ni harassment tunayowapa, anakuja Mzambia anakuja na fedha zake, anafika Kariakoo anakutana na TAKUKURU, anakutaka na Polisi anakutana na TRA, huyu hawezi kurudi. Shughuli ya kodi inasomewa, watu wanakaa darasani wanapata degree ya kodi, hawa watu wanafanya TRA, tuwaombe Polisi na vyombo vyote vya ulinzi ya usalama wafanye kazi walizosomea. Yako madhara yako madhara ya kuwapa watu wakafanye kazi ambayo hawakusomea. Madhara haya ni makubwa, tunaharibu uchumi wetu wenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Kariakoo mabenki yote yanafungwa, mnajua kwa sababu gani? Kila branch ya Kariakoo inafungwa, kwa sababu hakuna biashara tena, biashara yote imehamia wapi, Zambia, Kenya na Uganda. Hii siyo sawa, Mungu alituweka Tanzania geographically, Tanzania tuko mpakani ni kwa nia njema, tuutumie mpaka huu kwa maendeleo yetu lakini tunafanya nini. Tuangalie trade angalia transit trade, angalia vizingiti vya barabarani, lori mpaka lifike Zambia limesimamishwa zaidi ya mara 30, polisi wako everywhere, watu wa mizani wapo, sasa hizi tunaambiwa lazima tufuate sharia, lakini hii sheria ametunga nani, si sisi leteni tuibadilishe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ni suala la Afrika Mashariki, Kenya wanatudanganya, kwa sababu Kenya biashara yao haiko Zambia, haiko Kongo. Tanzania sisi wanaotuletea fedha ni Zambia, ni Malawi, ni Kongo, ndio watafuata Burundi kidogo, watafuata na Rwanda. Niwaombe sana Serikalini biashara hii isipokua, maana leo Waziri wa Fedha tutampiga maneno tu hapa, lakini Waziri wa Fedha tusipomsaidia biashara ikakua, hawezi kukusanya, hawezi kuleta hela ya maendeleo, tutaaanza kulalamika hapa. Kwa hiyo niwaombe wenzetu wazingatie hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi kwenye World Economic Forum bosi wa IMF ameulizwa anasema ili nchi ifanye vizuri mambo machache sana, moja kubwa lililosemwa ni growth, kwamba lazima tulete fedha za kukuza uchumi, tukuze kilimo, tukuze biashara, tukuze kila jambo. La mwisho akasema ni suala la private sector, ndugu zangu tukidhani Serikali inaweza ikafanya kila kitu, kuna mtu tunamdanganya sio kweli. Nenda kuanzia China, nenda kote unakokujua ambako wameendelea juzi kilichofanya waendelee ni private sector.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi niwaombe sana, unajua niwaambieni hakuna nchi iliyoendelea kwa kuwa na maskini peke yake, haipo, no single country imeendelea kwa kuwa na maskini peke yake. Tufanye jukumu la kupunguza umaskini, tufanye jukumu la kuondoa wanyonge kwenye uchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtu mmoja akiwa na pesa, leo Mbunge mmoja akiwa amepata Ubunge na niwaulize Wabunge wenzangu kuna watu wamepata Ubunge ndio ameajiri dereva, ameajiri Katibu na kadhalika kwa sababu ya nini tuna income zaidi. Uchumi pia unafanya kazi hivyo hivyo, akitokea mtu akawa tajiri, huyu mtu ataajiri watu wengi. Bakhresa hajasoma, lakini ameajiri wenye PhD ni kwa sababu ana uwezo wa kifedha. Kwa hiyo, kudhani wafanyabiashara ni watu wabaya siyo sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, liko suala hapa limesemwa na naomba sana amesema Mwenyekiti wa PIC tunayo mashirika zaidi ya 11 yametupa dividend bilioni 35. Nasema hizi hazitoshi, tuyasaidie mashirika haya yafanye vizuri zaidi. Nami ningemwomba Mwenyekiti atakapokuja mwaka kesho asiishie kwenye dividend, nataka atuonyeshe mashirika haya yamechangia shilingi ngapi kwenye uchumi. Watuoneshe maana kuna watu wanadhani ile Kampuni naweza nikaifuta tu, wewe unafuta kampuni assume leo watu wamesema hapa habari PUMA, tukiamua hapa leo kuifuta PUMA unajua maana yake ni nini? Unapoteza zaidi ya bilioni 400 kwenye uchumi wako, sasa unapata nini ukiifuta. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimalizie kusema jambo moja la ATC. Nataka nichukue nafasi hii kabisa kupongeza uamuzi wa kuwa na Shirika letu la ndege na niwaombe wenzangu tusiwe na haraka ya kupata faida, tunachotakiwa ni kuangalia multiplier effect ya kuwa na airline. Ukishakuwa na airline yako muuza mafuta atakupa dividend, muuza mafuta ya ndege utapata corporate tax utapata tax faida, lakini ameuza mafuta mengi kwa sababu una ndege, utapata ajira kwa sababu una ndege, utapata kodi kwa sababu una ndege, lakini utafanya biashara ichanganye Dodoma hukai masaa manane barabarani utawahi, uje ufanye biashara urudi. Hii ndio faida ya kuwa na airline in the country.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda pale Airport mtu akipita pale atanunua kitu yule mwenye duty free utapata kodi kule, matokeo yake ndio faida ya kuwa na Airline.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nakushukuru na naomba niwashukuru Wenyeviti kwa kazi nzuri waliyofanya. (Makofi)