Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Sonia Jumaa Magogo

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. SONIA J. MAGOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijaalia afya njema na leo tena nimeweza kusimama mbele ya Bunge lako tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni mmoja wa Wajumbe wa Kamati ya PAC na ningependa kuchukuwa fursa hii kumpongeza Mwenyekiti wangu na Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti kwa kuwasilisha vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuanza, nilikuwa na ushauri kidogo kwenye haya Mashirikia na Taasisi ambazo Serikali inawekeza fedha zake. Ninachoona hapa kwanza haya Mashirika yenyewe kwa yenyewe wanatakiwa yawe na mahusiano mazuri. Ikiwa haya mashirikia yatajitangaza vizuri na ikajulikana yanafanya nini na wenyewe kwa wenyewe wakawa wanapeana huduma, kwa mfano SUMA JKT, wanatengeneza furniture nzuri sana, wanatengeneza product ya maji ambayo walileta kwenye Kamati yetu na tuliyaona ni mazuri na bei yake ni nzuri. Hivyo kama Serikali itaunga mkono na wenyewe kwa wenyewe wakasaidiana, kwa mfano, kukawa kuna maelekezo kwamba furniture zote zinunuliwe kutoka SUMA JKT, ama sehemu kubwa furniture za Serikali ziwe zinatoka SUMA JKT, itawasaidia kutengeneza faida zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa bandari, tukiangalia bandari yetu ya Dar es Salaam, ina mlundikano wa mizigo mingi sana; lakini kuna bandari ya Tanga na bandari ya Mtwara. Kama kutakuwa na categorization ya mizigo mingine inakwenda Tanga, mingine inakwenda Mtwara, itasaidia na zile bandari nyingine kuweza kujiendesha vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile tunaona Serikali yetu inavyotumia fedha nyingi katika kutengeneza miundombinu ya barabara. Bandari wanaweza wakawatumia zaidi TRC kusafirisha mizigo kuliko kutumia malori ambayo yanapita na mizigo mikubwa kwenye barabara na kuharibu miundombinu ya barabara zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni bajeti ya Ofisi ya Msajili wa Hazina. Kama tulivyoona, hii Ofisi ina mashirika mengi sana ya kusimamia. Kama watapewa bajeti nzuri ya kutosha na ikaenda kwa wakati na wakawa wanafanya performance contract na zile Taasisi, pia wakawa na ufuatiliaji wa expenditure kwenye zile taasisi mara kwa mara, itasaidia kufanya zile taasisi ziwe na uwoga na kutengeneza faida kwa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati huo huo tunaona kuna madeni mengi sana hizi taasisi zinadai. Serikali ingeweza kuwasaidia ili waweze kukusanya yale madeni yao pale ambapo wao wamefikia ukomo. Kwa mfano, tunaona wengine ni waajiriwa Serikali na wengine wanajulikana wako wapi, wanaweza kutaifishiwa mali zao. Serikali iwasaidie kama vile ilivyowezekana kwenye Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu na wenyewe wasaidiwe ili hizi fedha zirudi ziwadaidie kuendesha shughuli zao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine ni suala la kukaimu. Mtu anapokuwa anakaimu, anakuwa na hali ya uwoga. Yaani anakuwa hana ile full mandate, anakuwa na wasi wasi kwenye kile kitu anachokifanya, hasa kwenye zile level za Management. Kwa hiyo, kama watasaidiwa kuondoa hili tatizo la kukaimu na wakawa wanawapa wale watu wanaokaimu madaraka au kuziba zile nafasi kwa wakati, itasaidia sana kuchochea maendeleo katika zile taasisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.