Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi, kwanza naomba nipongeze Wajumbe wenzangu wa Kamati ya PIC kwa kazi nzuri ambayo wameifanya ya kuweza kuishauri Serikali katika utendaji kiujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze na jambo la kwanza ya masuala machache ambayo yamejitokeza hapa ndani; kwanza kuna mchangiaji mmoja ameeleza hajui tofauti ya revenue na tozo, lakini naomba tutambue kwamba tuna mapato ya aina mbili katika bajeti yetu ya Serikali. Tuna mapato yanayotokana na kodi na tuna mapato ambayo hayatokani na kodi. Kwa hiyo, unavyotuambui revenue na utambui tozo nazo ni revenue ni mapato kwa hiyo tusiwe tunachanganya kidogo masuala haya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine limejitokeza suala la kwamba faida kutoka Serikali inayopata katika uwekezaji kwenye taasisi na baadhi ya mashirika ya umma imepungua kutoka bilioni 800 na ushehe mpaka bilioni 600. Serikali katika hizi taasisi na mashirika ya umma ambapo imewekeza inapata aina mbili za mapato; kuna mapato ghafi ambayo ni 15% kutoka kwenye mauzo na pia kuna mapato yanayotokana na gawio baada gawio la kwenye faida yaani dividend. (Makofi)

Sasa baada ya kutoa haya unakuta bado kuna masalia ya ziada yamebaki, kwa hiyo kwa mujibu wa Sheria ya Bajeti ambayo ni 70% inachukuliwa na Hazina na 30% inabaki inaendelea kwa ajili ya kuendelea hayo mashirika kufanya uwekezaji. kwa hiyo kushuka kutoka bilioni 800 mpaka bilioni 600 ilitokana na kwamba kulikuwa na malimbikizo ya miaka ya nyuma kulikuwa na cummulative figure retained earnings ndiyo ambayo ilichukuliwa na Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo alilisemea rafiki yangu Mheshimiwa Silinde ni kuhusiana na miradi ya maji. Mwaka jana tumepitisha bajeti ya maji takribani bilioni 673 ambayo ni ya miradi ya maendeleo katika hizi bilioni 673; shilingi bilioni 443 zinatokana na mapato ya ndani na zinazobaki zinatokana na mikopo pamoja na ruzuku za wafadhili mbalimbali yaani fedha za nje. Sasa kwenye hizo shilingi bilioni 443 hapo ndani pia tuna mfuko wa maji ambapo una bilioni 158 na siyo ile bilioni 249 aliyoisema na katika hiyo bilioni 158 Serikali imeshatoa bilioni 67 ambayo ni sawasawa na 43% ambayo imeshapatikana. Na wengi katika Halmashauri zetu tunajua kabisa miradi ya maji inatekelezwa na Halmashauri zinatuma certificate Wizarani ikishatuma certificate Wizarani ndipo Serikali inapeleka pesa na hatua hii ilichukuliwa kwa sababu fedha zilikuwa zinaliwa na miradi haitekelezwi kwa wakati, ndiyo maana Serikali ilibadilisha utaratibu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala lingine ambalo limeweza kuzungumziwa ni kuhusiana na masuala ya madeni. Ndugu zangu tunajua taasisi ya kufanya kazi kuna madeni na sisi kwenye Kamati yetu tumekuwa tukisisitiza sana ulipaji wa madeni na pia katika kuongeza mitaji baadhi ya taasisi na mojawapo ambapo tunaiona katika ulipaji wa madeni yasipolipwa kwa wakati kulingana na kanuni za kiuhasibu zinavyohitaji lazima ufanye provision for doubtful debts yaani unafanya in payment ya receivable kwamba endapo isipokusanywa tutakuwa na gharama ya hasara kiasi gani, kwa hiyo, tumekuwa tukisisitiza kwenye jambo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuzungumzia hapo naomba nirudi kwenye usimamizi Ofisi ya Treasury Register (TR). Serikali kama tulivyosema awali kuna mapato yanayotokana na kodi na mapato ambayo hayatokani na kodi katika moja ya mapato ambayo hayatokani na kodi ni kutoka Ofisi ya TR. Sasa ili aweze tuweze kuongeza mapato ambayo hayatokani na kodi maana yake tukaboreshe usimamizi wa hiyo Ofisi ya TR na katika kuboresha ofisi hii kimsingi haya makampuni/taasisi zote ziko nchi nzima na watumishi wako kwenye kama 105 maana yake ni kada mbalimbali wa chini mpaka wa juu. Sasa niombe Serikali ikaweze kumwezesha TR kibajeti ili akawekeze kwenye TEHAMA na kwamba kila mwezi mashirika yote haya report zao za mahesabu za kila mwezi wanaziingiza katika mfumo ambapo mtu amekaa ofisini kwake kama ni Mwanza kama ni Mbeya anaingizwa kwenye mfumo ofisi ya TR kutokea Dodoma Makao hapa wana monitor. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna reporting system inaitwa work based reporting kwa hiyo inatumika ile na mna- control mashirika yetu na makampuni ya nje yana-control dunia nzima kwa kupitia mfumo na hii itamsaidia TR.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na sisi kama Kamati ya PIC ili tuweze tukasimamie vizuri haya mashirika tunahitaji kufanya kazi kwa ukaribu vizuri kabisa na Ofisi ya TR. Sasa ni vyema tukaboresha namna ya kiutawala Ofisi ya TR kuwasiliana na Bunge, TR awasiliane moja kwa moja na Bunge maana mlolongo wa kupitia kwa Katibu Mkuu halafu ndiyo ije kwa Mheshimiwa Waziri halafu ndiyo ije sasa Ofisi ya Bunge tumekuwa na mawasiliano yanachelewa na maamuzi pengine yanachelewa. Wajumbe wanahitaji kuchangia uwezo semina hazifanyiki, Wajumbe wanahitaji kwenye kukagua miradi tumealikwa hatujaenda kwa sababu ya mawasiliano. Kwa hiyo, tunaomba TR apewe madaraka ya moja kwa moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na ili tuweze kuongeza ufanisi katika taasisi na mashirika yote haya tunahitaji TR akazingatie sheria; 60% ya gharama ikaende kuzingatiwa na kuweza kusimamia na tukifanya hivyo tutaondoa uwalakini wa mashirika ambayo yatakuwa yanafanya biashara au kazi kwa hasara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Kamati yetu tumesisitiza uongezaji wa mitaji na tunapongeza sana Serikali kwa kufufua Shirika la Air Tanzania. Nina imani kabisa miaka mitanomitatu ijayo au minne Air Tanzania itaanza kufanya kazi kwa faida kwa sababu uwekezaji huu ambao umefanywa na Serikali tutaenda kuongeza biashara, abiria wengi watabebwa na ndipo ambapo gharama zitaenda zinashuka ukilinganisha na mapato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na pia kama wachangiaji wengine walivyosema kwamba kwa kufufua Air Tanzania tutaenda na kuboresha sekta zingine ambazo ni sekta kubwa sana ya utalii, tutaenda kuongeza ajira na maeneo mengine ya Tanzania yatafikika. Kwa mfano Mkoa wetu wa Katavi tuna Mbuga ya Katavi ambayo ni nzuri sana na wanyama wakubwa wazuri sana, lakini ni kwamba Air Tanzania ikifika kule na uwanja wa ndege upo tutaongeza watalii wakuja kutalii kwenye nchi yetu na mapato ya Serikali yataongezeka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile shirika letu la Air Tanzania hebu kwenye kulinyanyua tulipe discount kwenye baadhi ya charge Serikali kwa mfano charge za airport, landing fee, kwenye charge cha TCIAA tuwape discount. Na pia TTCL wanahitaji mtaji wa dola kama 230,000 kama mchango wa Serikali ili iweze kushindana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru naunga mkono hoja. (Makofi)