Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuchangia. Jambo la kwanza ambalo nataka niseme, Taifa letu kama alivyosema Dkt. Kamala linafanya radical changes katika baadhi ya maeneo, lakini radical changes zozote ambazo tunazifanya kama Taifa, bila kuwa na inclusive plan ya sehemu kubwa ya population, hazitoweza kutuletea matokeo mazuri huko mbele tunakokwenda. Tumekuwa na Wizara ya Fedha katika Kamati yetu ya Bajeti na nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Wataalam waliotoka Wizara ya Fedha na naweza nikasema honestly kabisa kutoka moyoni for the first time nimemwona Mheshimiwa wa Fedha amekuwa very accommodative na anafungua milango ya ushauri na hapa ni lazima tuishauri Serikali kwa ukweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitatumia takwimu za BOT za mwezi Novemba. Ukiangalia takwimu za Benki Kuu kati ya mwezi wa nane, mpaka mwezi wa 11 our forex zimeshuka kwa zaidi ya dola milioni 500, fedha zetu za kigeni zimeshuka kwa kiwango hicho. Pia ukiangalia pressure kwenye shilingi yetu, leo dola kwenye soko inakwenda karibu Sh.2400, maana yake the cost of imports zinakwenda juu, shilingi inakuwa dhaifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia forex tunapata kutoka wapi? Ukiangalia mazao yote yanayotuingia fedha za kigeni, our exports zimeshuka,. Kwa hiyo, tafsiri yake ni kwamba, fedha za kigeni kuingia kwenye soko letu kuna upungufu na trend hii imeendelea kuwepo toka mwaka 2016. Hata hivyo, lakini ukiangalia taarifa ya TRA juu ya makusanyo ya kodi waliyoileta kwenye Kamati, malengo ilikuwa ni kwamba ukuaji wa makusanyo ya mapato yalikuwa ni asilimia 18.5, ndiyo yaliyokuwa malengo yetu, kwa miezi sita makusanyo yetu yamekuwa kwa asilimia mbili tu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la tatu ambalo kwa mtazamo wangu naliona ni challenge, mapato ya kodi ya customs yamekuwa kwa negative one percent maana yake yameshuka kwa asilimia moja, tafsiri yake ni kwamba component inayotuingizia asilimia 30 ya mapato, haiendi vizuri. Haya ni indication. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda kwenye landing, amesema Dkt, Kamala, segment pekee inayokua ya kukopesha katika commercial banks ni personal landing, mikopo ya wafanyakazi na Waheshimiwa Wabunge tunayokopa ambayo ni one hundred percent haiendi kwenye production. Ukiangalia commercial landing kwenye Agro sector imeshuka, ukiangalia landing kwenye manufacturing imeshuka. Sasa nini ushauri wangu, radical change tuliyofanya kama nchi, tumewekeza kwenye airline, tunajenga barabara, tunajenga viwanja vya ndege katika hifadhi zetu na tourist destination. Ushauri wangu, Wizara ya Fedha, Wizara ya Miundombinu, Wizara ya Tourism, kwa sababu GDP contribution ya Sekta ya Utalii ni asilimia 17, ni lazima Wizara hizi tatu zikae pamoja zije na mkakati wa growth, kwa sababu ukisoma taarifa zote za Wizara ya Fedha hakuna mpango wa kukuza biashara ni mipango ya administrative tu and this is counterproductive. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili tuweze ku-yield mapato kutokana na kwanza nawashangaa watu wote wanaofikiri kwamba tutapata faida kwenye ATC, leo Airline Business kwa Afrika inakuwa projected itapata hasara ya three million US Dola, Sekta ya Airline. Kwa nini nchi zinawekeza kwenye airline, zinawekeza kwa sababu it is means to stimulate growth kwenye sekta zingine. Kwa hiyo ushauri wangu, Wizara ya Fedha na end of the day anayeandika cheque ya kulipa ndege na kulipa cost zote ni Wizara ya Fedha, nimemwambia kwenye Kamati Mheshimiwa Waziri wa Fedha na narudia ndani ya Bunge, its time awe kaka mkuu ni lazima tuone tourism ina-grow kwa zaidi ya asilimia 22 ili iweze kuchangia kwenye GDP ya Taifa letu tuweze kurudisha investment tuliyowekeza kwenye ndege. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo ambalo ni muhimu sana tuelewe na mimi nataka niwaombe Serikali kwa heshima, Tanzania Kariakoo ilikuwa ni trading center ya nchi za SADC. Leo tuna advantage kubwa sana na nataka niwaombe Serikali, tunapokuwa kwenye hizi Jumuiya blocks mfano hii EAC, the most important question ya kujiuliza, who is our cash carry? Cash carry yetu ni Kenya the trading partner, cash carry yetu ni Uganda au ni Rwanda? Our cash carry ni Kongo na Zambia. Kwa hiyo all our economic policies ni lazima tutazame soko hilo. Tusipofanya namna hiyo hatutoweza kupata benefit ya kuwepo kwa eneo la Bandari ya Dar es Salam. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni jambo ambalo ni muhimu sana tulitazame, Eastern part ya Congo kuna zaidi ya watu milioni 25, how we are taking advantage of that? Leo amesema Mheshimiwa Mwijage, tunapitisha hii Sheria mnaita sijui axle, kwamba malori ya uzito, atakayekuwa disadvantaged ni sisi kwa sababu our trading partner ni Zambia, watahama wataenda Beila.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nitolee mfano kampuni kama PUMA. PUMA Serikali ina-own fifty percent, PUMA kwa mwaka 2011 mpaka 2017 wamelipa dividend Serikalini sixty billion shilling. Naomba msikilize, PUMA wamelipa tozo na kodi kwa miaka miwili for hundred and eighty billion shilling, halafu huyu anaomba leseni ya aviation industry mnamnyima, jamani what is this? Yaani PUMA ambaye tuna asilimia 50, ametulipa kwa miaka miwili bilioni 480 kodi, anaomba leseni ya aviation hapewi, why? Nashindwa kuelewa kwamba tunatafakari namna gani! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Kariakoo is dying...

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Taarifa.

T A A R I F A

MWENYEKITI: Mheshimiwa Bashe, taarifa hiyo.

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipokea, narekebisha siyo 2011 ni 2009. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachotaka nishauri ni nini? Ni lazima Wizara ya Fedha, fiscal measures zinazotengenezwa na Wizara ya Fedha ziwe production oriented badala ya kuwa more control measures. Mimi ni muumini wa aina moja ya ajabu sana ya falsafa. Naamini kwamba Mchaga wa Kariakoo akikwepa kodi haipeleki Ulaya, hafungui akaunti Uswiss, atakwenda kununua mfuko wa cement upata indirect. Kwa hiyo, why are we controlling these small businesses, tunazi-suffocate? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo lilinishtua sana na namshukuru Waziri wa Fedha aliahidi kulifanyia kazi. Tulipitisha measure hapa ya kuongeza kodi kwenye crude oil, tukaongeza 35% matokeo yake zaidi ya 90% ya mapato katika kipande hicho imeshuka. Tukauliza swali, mbona hamna matatizo ya mafuta nchini? Tukaambiwa wana-import zaidi refined oil. Tafsiri yake ni nini? Viwanda vya ndani, re-export component na taarifa za BoT zimeonyesha re-export imeshuka. One the product ambayo tulikuwa tunafanya re-export ilikuwa ni crude oil tukiingiza nchini, tukisafisha yakawa refined tunayauza Congo na mataifa ya nje. Matokeo yake sasa hivi sisi tunaokaa kwenye boader mafuta yanatoka nchi za jirani, it is counter productive. Kwa hiyo, ushauri wangu kwa Wizara ya Fedha, umefika wakati wa ku-come up na mpango wa kikodi ambao uta-stimulate production.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kuhusu kilimo. Kilimo kinachangia almost 30% ya GDP yetu ukiacha tourism. Umefika wakati kama nchi ni lazima tuje na mkakati wa ku- protect agro-sector. Tusipokuja na mkakati wa kulinda sekta ya kilimo tutarajie maafa huko mbele kwa sababu kilimo kinatuletea mambo mawili; moja food security lakini mbili ni component inayotuingizia forex. Leo tumbaku imeshuka, zao pekee la kilimo linalo-grow kwenye export ni cotton peke yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu wa mwisho kwa Serikali, just a minute, mazao ya mahindi, karanga na kadhalika yaacheni katika regional level. Wizara ya Kilimo ichukue mazao strategic kama Korosho, katani, kahawa, tumbaku ili tuwe na big plan kwa ajili ya ku-increase the export yetu. Bila ya hivyo, traditional crops na non-traditional crops zinashuka export matokeo yake tutapata shida kama nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. (Makofi)