Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

Hon. David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kupata fursa hii ya kuchangia Taarifa ya Kamati ya Bajeti. Nianze kwa kusema jambo moja tu; moja ya vitu ambavyo ninamwonea huruma sana Rais, Dkt. Magufuli, ni anazungukwa na watu wanaompa taarifa za uongo sana. Bahati mbaya sana, tunapokaribia kwenda kwenye Uchaguzi Mkuu, watu wanaongea uongo sana, yaani unaweza kumwambia mtu jambo ambalo hata yeye mwenyewe anajua kabisa unamdanganya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesikiliza hoja zilizokuwa zinajadiliwa tangu tulipoanza Bunge hili, hususan siku ya jana na mwendelezo wa siku ya leo, bado hatujibu maswali ya msingi wanayohitaji Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unaweza kuiangalia Taarifa ya Kamati ya Bajeti, unaweza ukapata maelezo ambayo sisi Wajumbe tulikuwa tunapewa ndani ya Kamati ya Bajeti. Kuna vitu havipo kwenye taarifa yetu ambavyo ndivyo vingekuwa vina uwezo wa kujibu maswali ya msingi ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna taarifa tulipewa ya Mfuko wa Maji. Mfuko huu ambao Serikali ya Chama cha Mapinduzi ilisema inakwenda kumtua mama ndoo kichwani, kati ya shilingi bilioni 299.9 ambazo Serikali ilitakiwa itoe kupeleka katika Mfuko wa Maendeleo ya Maji, imetoa shilingi bilioni 1,637 sawa sawa na asilimia 0.6. Haya hampendi kuyasikia, lakini ndiyo ukweli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wahisani waliahidi kutoa shilingi bilioni 284, mpaka sasa wametoa shilingi bilioni 4,320, sawa sawa na 4%. Haya sasa hebu niambie, unatatuaje tatizo la maji? Unamtuaje mama ndoo kichwani katika kipindi hiki cha miaka minne, kuelekea uchaguzi, hili haliwezi kuzungumzwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iliahidi ndani ya Bunge kwamba itamalizia majengo yote ya wananchi wa Tanzania waliyoyajenga kwa nguvu kazi yao; kwenye shule na afya; kwa maana ya Shule za Sekondari na Msingi, maboma yote, waliahidi. Ikapigwa hesabu fedha iliyokuwa inahitajika katika mwaka wa fedha uliokuwa unapita, shilingi bilioni 251. Sisi kwenye Kamati ya Bajeti tulipambana na Wizara ya Fedha tukawaita mbele ya Kamati ya Uongozi Serikali ikaji-comit kwamba katika Mwaka wa Fedha unaokuja robo ya kwanza tutatoa shilingi bilioni 29. Mpaka leo tunavyozungumza, hawajapeleka hata senti moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa haya ndiyo maswali ya msingi ambayo wananchi wanataka majibu ya moja kwa moja. Sasa unakwenda kujadili mambo makubwa. Amezungumza vizuri sana Mheshimiwa Balozi Dkt. Kamala, ukuaji wa uchumi. Kwenye takwimu za Serikali zinaji- contardict zenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Kamati ya Bajeti, niwaeleze, katika mwaka wa fedha uliopita, ukisoma taarifa yao, inasema, mwaka wa fedha kipindi kama hiki kilichopita, ukuaji wa uchumi ulikua kwa asilimia 5.8, yaani Julai – Desemba na mwaka huu uchumi umekuwa kwa 6.0% yaani imeongezeka 2%. Ukirudi nyuma ukapitia taarifa ya mwaka 2018, uchumi wa Tanzania ulikua kwa 6.8%; yaani ni uongo uliopindukia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2018 kwenye taarifa yao ambayo ipo; sasa bahati mbaya sana, taarifa ambayo iko ndani ya Hansard ambayo Wabunge wote tunazo, mimi ninazo na Wabunge wote mnazo, labda kama hamsomi, inaonesha 6.8%. Taarifa ya leo imebadilisha matokeo ya mwaka 2018, halafu wanakuja wataalam wanakwambia huwa tuna-adjust, yaani what a fix? Yaani can you fix a country like this? I wonder! Hii ndiyo bahati mbaya. Sasa ndio watu waliopo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unakwenda kuangalia DSE, ndani ya mwaka mmoja Soko la Hisa la Dar es Salaam limepoteza mtaji wa shilingi trilioni nne. (Makofi)

MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, haya hayazungumzwi na ndiyo yanayohusu mzunguko wa fedha wa Taifa. (Makofi)

MWENYEKITI: Ndiyo Mheshimiwa Obama.

T A A R I F A

MWENYEKITI: Mheshimiwa Silinde.

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, mara nyingi huwa sina muda wa kudanganya na sipendi kumjibu Mheshimiwa Obama, nafikiri alikuwa anatafuta tu nafasi ya kuzungumza humu ndani. (Kicheko/Vigelegele/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mzunguko wa fedha ni asilimia 3.2, mfumuko wa bei ni asilimia 3.3. Uki-calculate namna ya ukuaji wa Pato la Taifa, tunakua kwa asilimia moja, wala siyo sita. Ukiwauliza Serikali juu ya hizi takwimu, soma taarifa ya Benki Kuu, soma taarifa wanayotoa Serikali, yaani ni vitu viwili contrary. Nami najua kwa nini BoT wanataja taarifa ya ukweli, ni kwa sababu inasomwa na IMF, inasomwa na World Bank, inasomwa na watu ambao wanajua. Taarifa ya wanasiasa inakuja kisiasa kweli kweli na hilo ndilo tatizo kubwa sana ambalo linalikabili Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Watanzania wanataka kujua maswali madogo madogo; mfumuko wa bei umeshuka kwa nini bei za vyakula, bei za bidhaa zinapanda? Serikali inapaswa kujibu mambo madogo madogo. unataka u-deal na micro economy ambayo hujaifanyia feasibility study, ni kama tu umekurupuka, hujui jambo lolote inavyokwenda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa angalia matumizi; ukienda kuangalia kwenye Fungu la matumizi huku, unakuta Hazina, ndani ya nusu mwaka tulitakiwa tuwape bilioni 144 mpaka sasa wamepewa bilioni 414 asilimia 286. Ukiangalia Tume ya Uchaguzi 1.2 wamepewa 8.3 billion sawasawa na asilimia 674. Kaangalie yale Mafungu yaliyozidishiwa fedha, narudia kusema, siku Mheshimiwa Dkt. Magufuli atakapomaliza utawala wake, mtu wa kwanza kwenda Jela atakuwa ni Katibu Mkuu wa Hazina. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti,na msimdanganye, atakwenda, kwa sababu Mheshimiwa Rais akishaondoka madarakani hana power tena ya kumlinda mtu aliyeko. Anayekupenda anakwambia ukweli, ukipitia matumizi kwenye hivi vitabu, mwakani CAG akipitia haya taarifa itakayoletwa ndani ya Bunge kutakuwa na zaidi, yaani matumizi ya fedha, mtakuja kuambiwa hapa, safari hii mmetajiwa 1.5 trillion, itakuja trillion nane, kwa sababu fedha zilizokuwa misallocated, is too much na Bunge hatuletewi kile kitabu cha kuonesha Serikali inafanya reallocation kila mara, hakiji humu ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tungependa kufahamu, Serikali ni kwa nini hailipi fedha za Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na mashirika ya umma, ni kwa nini Serikali katika robo ya kwanza mwaka 2018 tulipitisha kwenye fungu kwamba Serikali kama bilioni 60 za kulipa milioni 50 kila kijiji kwenye pilot study, mpaka sasa hivi, ni kwa nini hawjapeleka na ndiyo ahadi yao katika Uchaguzi Mkuu? Tunahangaika na uchumi mdogo ili kuutengeneza uchumi mkubwa, hilo ndilo ambalo tunalihitaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, pamoja na yote haya machache niliyoyasema, lakini naiomba Serikali pamoja na Kamati ya Bajeti tuliyopendekeza, siyo tu ije iyajibu, lakini tunataka commitment ya Serikali kwenye kutekeleza haya na wala siyo…

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Silinde.

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)