Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Usimamizi wa Matumizi ya Fedha za Umma katika Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2017

Hon. Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2018 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Usimamizi wa Matumizi ya Fedha za Umma katika Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2017

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru, na mimi kuweza kunipatia nafasi ya kutoa maoni yangu juu ya hoja ambayo iko mbele yetu. Kwanza kabisa nipende kuzipongeza Kamati zote mbili kwa kuweza kutuletea taarifa iliyosheheni maoni na mapendekezo ambayo yana maslahi mapana ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, labda tu niwakumbushe wenzangu ambao wanajifanya kusahau kwamba hawafahamu msingi wa Kamati hizi mbili kitu gani ambacho wanatakiwa kufanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, msingi wa kazi za Kamati ya PAC...

MBUNGE FULANI: Ooohhh Khadija.

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: …zinatokana na taarifa iliyokaguliwa na CAG. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitawaelezea machache tu ili waweze kurudisha kumbukumbu zao na hisia zao karibu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati iliweza kubaini mapungufu na madhaifu mbalimbali katika ripoti ya CAG, nitayaelezaa machache. Kamati yetu iliweza kubaini mapungufu katika makusanyo ya mapato yetu ya nchi. Lakini baada ya Kamati ya PAC kuishauri Serikali iliweza kuleta mfumo mzuri wa makusanyo wa mapato yetu na sasa hivi tunaweza kuona tija, ya mapato yetu ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati yetu iliweza kubaini mapungufu katika mikataba yetu ya madini baada ya Kamati yetu kuishauri Serikali iliweza kuchukua hatua mbalimbali. Kamati yetu iliweza kubaini upungufu wa kiutendaji, kwenye mashirika na taasisi zetu za umma, baada ya Kamati kuishauri Serikali iliweza kuteua Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu, na sasa hivi Mashirika yetu yanaweza kufanya kazi vizuri baada ya kuweza kuweka ile mianya ambayo ilikuwa iko wazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati yetu iliweza kuona mapungufu katika ufanisi wa kazi katika Halmashauri zetu. Baada ya Kamati yetu kuishauri Serikali, Serikali imeweza kuzidisha ufanisi, sasa hivi Halmashauri zetu nyingi zimeanza kupata hati safi katika mchakato wetu wa Ukaguzi. (Makofi)

MHE. BONIPHACE M.GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

WABUNGE FULANI: Endelea wewe, endelea.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Getere.

T A A R I F A

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Khadija Nassir unaipokea taarifa hiyo?

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, naipokea taarifa hii. Hiyo ni moja ya kati ya…

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Taarifa.

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: …na utekelezaji wa Serikali baada ya kupata maelekezo ya…

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Bungara.

T A A R I F A

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Khadija Nassir unaipokea taarifa hiyo?

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa hiyo siipokei, Mheshimiwa Zitto ni kati ya wahasibu ambao tupo hapa Bungeni, tupo very competent, yeye ni mmoja kati ya wengi ambao tupo wazi na macho kuangalia ufanisi wa Kamati na Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuendelea. Kamati yetu pia iliweza kubaini madeni ya Serikali kwenye taasisi na mashirika yetu ya umma, lakini baada ya kamati yetu kuweza kushauri Serikali, Serikali imeweza kuanza kulipa madeni hayo na sasa mashirika na taasisi zetu za umma zimeanza kufanya vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya hayo sasa naomba niende kwenye uwekezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo. Napenda kuipongeza Serikali yangu na ninapenda kuwashauri Wabunge wenzangu, kwa vile Serikali yetu ni sikivu, inasikia maelekezo ya Kamati na ushauri mmoja mmoja wa Wabunge tuendelee kufanya kazi yetu ya kikanuni kuisimamia na kuishauri Serikali katika mambo mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali yetu imeanza kwenye uwekezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo. Tumeona Serikali imewekeza kwenye mradi wa SGR ambayo inaenda kuipa vijana ajira zaidi ya 3,000. Mradi huu unaenda kutoa uboreshaji wa Wilaya zaidi ya 16 nchini na kutoa uwezeshaji wa vijiji zaidi ya 120 katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia Serikali imewekeza katika ununuzi wa ndege, ndege hizi zitarahisisha usafiri wa wananchi na kutatua changamoto katika sekta ya utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia Serikali imeweza kuwekeza katika miradi mikubwa ya umeme ambayo ita- stabilize uwezeshaji na uwekezaji katika miradi ya viwanda vya ndani. Mradi huu pia utachangia na kumwezesha Mtanzania mmoja mmoja katika kuweza kujikimu kimaisha. (Makofi)

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inafanya mambo mazuri sana…

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba ulinde muda wangu.

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Bungara taarifa.

T A A R I F A

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, tumezoea kuwaona wanachukua muda mwingi kupotosha, lakini sasa tumeamka na tupo tayari kuwaeleza wananchi nini Serikali inafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kueleza hayo naomba sasa niende moja kwa moja katika utekelezaji wa miradi mikubwa ambayo Serikali yetu imejikita…

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba ulinde muda wangu.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mwakajoka.

TA A R I F A

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Khadija Nassir unaipokea taarifa hiyo?

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, siipokei taarifa yake. Kwanza tu nimueleze kati ya majukumu ya Kamati ya PAC ni kusimamia mashirika changa na kusimamia mashirika ambayo yameanza kazi yake. Kwa hiyo miradi ambayo tunaielezea hapa ni miradi ambayo tumeianzisha sisi na kuisimamia kama Kamati ya PAC. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa niendelee na mchango wangu ambao nitajikita kuelezea…

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Taarifa ya mwisho hiyo inayomuhusu Mheshimiwa Khadija Nassir, Mheshimiwa Yussuf.

T A A R I F A

NAIBU SPIKA: Sawa, Mheshimiwa Khadija Nassir unaipokea taarifa hiyo?

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, siipokei taarifa yake na kwa vile walizoea tantalila na kwa vile walizoea baada ya kuimba nyimbo zao hatuwajibu walijua kwamba hakuna watu specific wa kuweza kuwajibu tantalila zao. Naomba niwaambie hivi uwekezaji ambao Serikali imefanya… (Makofi)

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mbilinyi kwa Mheshimiwa Khadija Nassir nimesema ile ilikuwa ni taarifa ya mwisho, Mheshimiwa Khadija Nassir una dakika mbili malizia muda wako.

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuendelea na naomba ulinde muda wangu.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa nielezee fursa ambazo tutazipata…

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mbilinyi unasubiri kunyolewa Mbeya 2020.

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama mradi wa SGR tutaweza kupata nafasi za ajira 2,500 nchini, uchumi wa Wilaya zaidi ya 16 na uchumi wa vijiji zaidi ya 106.

Mheshimiwa Naibu Spika, hapo hapo naomba nitoe ushauri, kwa vile Serikali imejikita katika kuwekeza katika miradi mikubwa naomba wakati wananza kuwekeza katika miradi mikubwa waweze kuanzisha miradi wezeshi ili tuweze kupata muda sahihi ambao tunatakiwa kuutumia katika uwekezaji. Pia kiasi sahihi ambacho tunaweza kukitumia katika uwekezaji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, kama kwenye mradi wa SGR tungeweza kuanzisha mradi wa kokoto, mradi wa chuma na miundombinu mizuri kabla ya kuanzisha huo mradi wa SGR tungeweza kupata specific term ambayo tutaitumia katika mradi wa SGR lakini pia tungeweza kubana matumizi katika uanzishaji wa mradi huu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile, mimi ni mwanakamati nimeshatoa maoni mengi sana kwenye Kamati…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)