Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuchangia Mpango wa Taifa wa Serikali. Nianze kwanza kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wetu, nimpongeze pia Waziri Mkuu wetu, nipongeze Mawaziri wote wa Serikali ya Awamu hii ya Tano kwa kazi nzuri sana ambayo wamekuwa wakiifanya kwa kipindi cha miaka mitatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niendele pia kumpongeza sana, kupongeza sana Wabunge wote ambao wamehamia CCM kutoka upinzani kwa kuona kazi nzuri sana inayofanywa na Mheshimiwa Rais, kwa kuona kazi nzuri sana inayofanywa na Mawaziri wetu na kuamua kuja CCM, kwa hiyo nikwambie Mheshimiwa Jenista jiandae kazi yako ni nzuri tutaendelea kujaa huku kwetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpongeze Mheshimiwa Dkt. Mpango, kama jina lake lilivyo kwa mpango mzuri, Naibu wake, Dkt. Kijaji, watendaji wote wa Wizara ya Fedha kwa kazi nzuri ambayo wametuletea huu mpango mzuri wa maendeleo ambao kwa kweli umepanga ukapangika, na ndio maana sasa hivi unatekelezeka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee, mimi leo nikupongeza kwa sababu mambo mazuri yanaonekana, niendelee kumpongeza Rais wetu na Serikali yetu na Chama chetu cha Mapinduzi kwa miradi ambayo sasa hivi yameanza kutekelezeka ya kielelezo ujenzi wa reli ya kati, ujenzi wa barabara wa barabara ya juu (Mfugale fyover) ujenzi wa viwanja vya ndege, uboreshaji wa shirika la ndege, mradi wa kuzalisha umeme maji - Rufiji, mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Uganda mpaka Tanga na miradi mingine mingi tu nikiitaja hapa muda utaisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda katika ukurasa wa 32 wa kitabu cha hotuba ya Waziri Mpango, niendelee kupongeza marekebisho ya Sheria ya Madini, kwa kweli niendelee kuwapongeza Mheshimiwa Rais, Mheshimiwa Spika, Naibu Spika na Wabunge wote wa Bunge la Jamhuri kwa kufanya marekebisho ya Sheria za Madini zilizofanyiwa
mapitio ili kuwezesha Serikali yetu kunufaika zaidi na rasilimali za madini ambayo imewezesha ongezeko la mapato kwa kipindi cha mwaka 2017/2018 lengo ambalo lilikuwa limewekwa na Serikali kwa mrabaha na ada za mwaka za leseni ilikuwa shilingi bilioni 194; lakini imeweza kukusanya bilioni 301.2 ambayo sawasawa na asilimia 56, kwa kweli hilo ni jambo kubwa sana. Tutakumbuka kwamba jinsi sheria hii ilivyokuwa imeleta matatizo makubwa wenzetu walikuwa hawaielewi lakini sasa hivi Serikali imeweza kupata mapato makubwa sana kupitia marekebisho ya sheria hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kupitia sheria hii imeweza kuweka katazo la kusafirisha madini ghafi ambayo hayajawekewa thamani. Ushauri wangu kwa Serikali, Serikali iweke mazingira wezeshi kwa kuondoa kodi katika mashine za ukataji wa madini ya vito. Hii itasaidia kuwa na wakataji wengi wa madini ya vito na pia itasaidia ajira kwa vijana wetu kupitia madini. Pia kuweka mazingira wezeshi ya kusaidia shughuli za wachimbaji wadogo wadogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia niombe Serikali iweze kuwasaidia kuwawekea mazingira wakina mama ili waweze kujiajiri kupitia madini kama vile kuna Chama cha TAWOMA ambacho ni chama cha wachimbaji wanawake kote nchini pia kiwezeshwe ili sisi wakina mama pia tuweze kujiajiri kupitia madini. Pia nishauri kwamba wawepo Maafisa Madini wa Mkoa kuliko walivyo wa kanda ilivyo sasa hivi ili kusaidia hii sekta ya madini waweze kukusanya pesa katika mikoa yote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ukienda katika ukurasa wa 33 unaelezea kuhusu elimu. Niipongeze Serikali yetu kwa utaratibu wa kutoa elimu bila malipo katika shule zetu ambapo wameweza kutumia shilingi bilioni 20.9 kila mwezi. Ukifungamanisha uchumi na maendeleo ya watu, mpango wa kuendeleza ufaulu katika masomo ya hesabu na sayansi na kuendelea kutoa elimu inayozingatia mahitaji halisi ya soko la ajira. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tunaelekea kwenye uchumi wa viwanda, sasa naiomba Serikali iwe na mikakati ya kuhakikisha kwamba shule zetu nchini zinaboreshewe maabara kwa sababu maabara katika shule nyingi bado hazijakamilika, lakini pia walimu bado hawatoshelezi kuwepo katika shule kufundisha hii elimu ya sayansi, lakini pia na vifaa vya maabara Serikali ijitahidi kwa sababu sasa hivi tunatakiwa tuandae wanasayansi wengi sana ili kusaidia huu uchumi wa viwanda, vijana wetu waweze kuajiriwa na tuweze sisi wenyewe kuwa na vijana ambao wanatumikia viwanda vyao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile naomba tu nitoe mfano wa nchi ya Singapore; unaona nchi ya Singapore ilikuwa ni nchi ambayo ina uchumi duni sana, lakini kuna yule Waziri Mkuu ambaye ni kiongozi wao anaitwa Lee Kuan Yew yeye kwakweli kwanza kabisa alivyoanza kuinua uchumi wa Singapore walimuona kama dikteta lakini sasa hivi alipofariki wamemkumbuka kwa sababu uchumi wa Singapore sasa hivi umekuwa upo juu sana na unaona yeye aliamua kutoa elimu kwa vijana wake wa Singapore na sasa hivi vijana wameweza kujiajiri, kuajiriwa na kutengeneza uchumi kwa kutumia viwanda walivyonavyo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja, asante sana.