Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti Asante sana kwa kunipa nafasi hii niweze kuchangia mapendekezo ya mpango wa Maendeleo ya Taifa 2019/2020.

Mheshimwa Mwenyekiti, nianze kwa kuungana na Waheshimiwa Wabunge wengi waliochangia kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais wetu Dkt. Pombe Magufuli kwa utendaji wake wa kazi mzuri, ametimiza mwaka wa tatu lakini tumeona Mheshimiwa Rais wetu akitekeleza kwa vitendo ule usemi kwamba penye nia pana njia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaendelea kumpa moyo Rais wetu na tuombe Watanzania waendelee kumuunga mkono ili miradi mikubwa ya maendeleo ambayo Rais wetu ameonesha kwamba Watanzania tukithubutu tunaweza tuweze kuiitekeleza iweze kusaidi kizazi hiki na vizazi hii na vijavyo.

Mheshimiwa Mweyekiti, pia nitumia nafasi hii kumshukuru Waziri Mkuu hivi karibuni alitembelea Mkoa wa Kagera kuangalia mwenendo wa msimu wa kahawa. Mheshimiwa Waziri Mkuu aliweza kutatua changamoto nyingi katika ziara, lakini pia alitoa maelekezo ya namna bora ambayo Serikali inahitaji kujipanga ili msimu ujao wa kahawa wakulima wetu waweze kufaidika na kilimo cha kahawa na katika hili niweze kushauri Serikali badala ya kusubiri msimu ukikaribia ndipo twende kwenye kukabiliana na changamoto za msimu basi on quarterly basis Serikali iwe inaita wadau, tunajadili namna ya kujipanga vizuri ili msimu wa kahawa na wa mazao mengine unapofika basi tujikite kwenye kutekeleza na kusimamia mazao haya ya biashara ili yaweze kuwasaidia wakulima lakini yaweze kuchangia kwenye pato la Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nimshukuru sana na nimpongeza Mheshimiwa Waziri Dkt. Mpango pamoja na shemeji yangu Dkt. Ashatu kwa mapendekezo kama rasimu, nasema kama rasimu kwa sababu ni mapendekezo bado na sisi Wabunge tuna nafasi ya kuboresha na nitumie nafasi hii kuwapongeza sana Kamati ya Bajeti hata muda wangu usipotosha, Kamati ya Bajeti wamatoa mapendekezo mazuri naunga mkono asilimia mia moja naamini Mheshimiwa Waziri kama mkiachukua yale pamoja na mapendekezo mazuri ya Waheshimiwa Wabunge basi tutakuwa na mapendekezo ya mpango mazuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya utangulizi huo nianze kuchangia mapendekezo ya mpango kuhusu suala la ufungamanishaji wa uchumi na maendeleo ya watu na nita-argue katika sehemu tatu ambazo ili tuweze kufungamisha uchumi na maendeleo ya watu lazima tuwe na Taifa lenye afya na nguvu kazi. Na katika hili niipongeza Serikali katika sekta ya afya Serikali imefanya kazi nzuri kwenye vituo vya tiba kote nchini dawa inapatikana na Serikali tunaona ikiendelea kujenga vituona katika hili Mheshimiwa Waziri kwa vile tupo kwenye mapendelezo ya mpango basi vile vituo vya afya viwili vya Nyabioza na Kanoni katika Wilaya ya Karagwe vile kwenye mapendekezo ya mpango. (Makofi)

Mheshimwia Mwenyekiti, jambo la pili ambalo ningependa kusisitiza na kuipongeza Serikali ni kuleta Mamlaka ya Maji Vijijini. Na katika hili Mhemimiwa Waziri tuombe sana Serikali pia ingalie kuwa kama kuna uwezekana zile shilingi 100 ambazo zinatoka kwenye mafuta zinaenda kwenye barabara kwa sababu ya umuhimu wa kuwatua akina mama ndoo nchini basi ikiwezekana iwe 75 kwa 75 halafu tukimaliza changamoto za upatikanaji wa maji safi na salama nchini turudi tena kwenye ile ratio ya 100kwenda kwenye mchango wa barabara na 50 kwenda kwenye mfuko wa maji hii itasaidia kutatua changamoto ya maji nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo ningependa kuchangia na kusisitiza sana pamoja na jitihada nzuri ya Serikali elimu bila ada lakini bado kuna changamoto kubwa ya upungufu wa madarasa, upungufu wa matundu ya vyoo, maabara katika shule za sekondari hazikamilika na hosteli kwa ajili ya vijana wetu wasichana. Sasa nipende katika kwenye mapendekezo ya mpango hili mlione ni jambo muhimu sana kwa sababu CDG haziendi lakini Serikali kupitia vipaumbele tumeona hela ikienda kusaida kwenye miradi mbalimbali ya maendeleo kwenye sekta nilizozitaja, lakini tukumbuke kwamba kuna miradi viporo upande wa zahanati, upande wa shule na kwenye mapendekezo haya basi tuiombe Serikali iangalie kwa uzito huo kama tulivyofanya Mheshimiwa Rais alivyosimamia zoezi la madawati nchini basi hali kadhalika twende kufanya hivyo kwenye shule za msingi, matundu ya vyoo na maabara kwa ajili ya sekondari nchini.
(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo ningependa kuchangia ni haya mazao ya vipaumbele. Kuna wengine wamezungumzia takwimu ya post harvest losses asilimia 30 ya mazao ya wakulima yanaharibikia mashambani. Lakini ukienda viwanda Mheshimiwa Mwenyekiti viwanda vinahitaji malighafi za wakulima hawa Kamati ya Viwanda na Biashara tulivyotembea viwandani sasa hivi robbot ndizo zinafanya kazi zime-replace ajira za Watanzania, lazima ajira hizi tuzitengeneze kwenye sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti lakini ukiangalia post harvest losses asiliamia 30 mkulima anahangaika lakini zao lake 30% linaharibika shambani na huku viwandani wanahitaji hizi malighafi nitolee mfano...

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji)

Eeh, naunga mkono hoja.