Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Peter Joseph Serukamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi nianze kwa kumpongeza sana Waziri wa Fedha na timu yake kwa mpango huu mzuri sana. Mpango huu mimi naukubali wote kama ulivyo shida yangu mimi ipo kwenye ku-finance kama kuna eneo tukubaliane vizuri ni namna ya haya tuliyoyapanga tutayatekeleza namna gani? Hapa kwangu mimi ndiyo napaona ukienda page ya 50 na mwenyewe amesema mpango huu unatarajiwa kugharimiwa na sekta ya umma na binafsi kupelekea uwekezaji wa moja kwa moja au kwa njia ya ubia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesoma mipango yote sijaona popote ambapo tunajadili kama miradi hii itatekelezwa kwa ubia ama miradi hii itatekelezwa na private sector na mimi Mheshimiwa Waziri hili ninaliamini nitalisema kila nitakapo simama, nina amini iko miradi ingeweza kutekelezwa na private sector na bado tukapata mambo mazuri zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, duniani kote ukienda, China, Malaysia, kote nchi zimeendelea juzi wanatumia sana PPP kwenye miradi mingi hasa hii ya kiuchumi. Kwa bahati mbaya sijaelewa tunatunga sheria na juzi umeleta sheria nzuri sana, lakini sioni miradi ambayo tuna i-push kwa ajili ya PPP. Kwa mfano, barabara ya kutoka Dar es Salaam kuja Chalinze utmeongea huu mwaka wa 10 ambao mimi ninaamini barabara hii tukiamua ku-push tutapata mtu wa kuijenga na kwa kweli tukitafuta private sector kitakachotokea tutapata fedha nyingi ambazo tutapeleka kwenye social services kwa maana ya elimu, kwa maana ya maji, kwa maana ya afya na tutapandisha mishahara ya wafanyakazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kama tutaamua miradi yote hii mikubwa tunafanya kama Serikali peke yake, madhara yake yako kwenye social services. Mipango hii ni mizuri sana kwa hiyo mimi ningeomba Mheshimiwa Waziri jambo hili kubwa na miradi hii umeipana vizuri, vipaumbele ni vizuri lakini umefika wakati tubadilishe mindset yetu, twende kutafuta watu tutakaosaidiana nao kufanya miradi hii ya maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, umeme, pamoja tunaenda kutengeneza umeme mwingi sana mimi nakubali jambo kubwa, lakini tufanye energy mix, tukipata mtu mwingine akazalisha kwenye jua, akazalisha kwenye upepo, akazalisha kwenye gemotheo, sisi tunazalisha kwenye maji maana tutakuwa na umeme mwingi kama Taifa labda megawatts
5,000/10,000 ambao tutaanza ku-export na mwingine tutatumia ndani, lakini bado tutakuwa tume-achieve kama nchi, lakini tukitafuta kitu kimoja tu mimi nasema ningeomba sana umefika wakati tujandiliane suala la kutumia private sector. Lakini private sector ije Tanzania cha kwanza lazima sheria zetu ziwe predictable, pesa zetu za kodi ziwe predictable kila kiwe kinaaminika, lakini kama tunabadilisha magoli kila siku ni kweli baadhi ya investors hawawezi kuja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu hawana hakika kesho tutafanya nini? Kwa hiyo mimi nina amini nchi yetu ina resorce nyingi sana, Mungu ametubarikia kila tu, naombeni sana imefika wakati tutumie private sector ili tuweze kwenda mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala la kilimo tunakiongea sana hapa ndani, lakini mimi nasema kilimo tulichoongea miaka yote jambo moja Serikali naona hatufanyi kwa nini nimesoma humu ndani, hatuongelei commercial farming, bila commercial farming matatizo ya kilimo hayatakwisha, matatizo yote ya kilimo yatatatuliwa na mashamba makubwa, sisemi tunyang’anywe mashamba. Mungu katupa ardhi bado ardhi hii watu watakuja wenye uwezo mkubwa. Mtu mwenye shamba lake kwa mfano hili jambo la korosho hivi kwa mfano mtu ambaye ana hekari 10,000; amelima korosho zake hawezi kumtafutie soko ninyi, hata omba pembejeo, kwa hiyo nasema tufike sehemu haya mawazo kila mtu anaweza akalima, haiwezekani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nasema tumeanza ku- push command economy hata hili la korosho, naomba mimi mwenzangu silielewi sana, Serikali ituache demand and supply ifanye kazi. Serikali kuingia ku-detect terms sio sawa, ndiyo matokeo yake wataingia watu katikati, watatuvuruga. Bei kuanguka za mazao imekuwepo hivyo duniani, kote kwa sababu inategemea soko la dunia. Lakini tuongelee zao moja, watu wa mahindi hali ni mbaya, mtama hali ni mbaya, kahawa hali ni mbaya, chai hali ni mbaya, why?

Kwa hiyo, mimi nasema ningeiomba Serikali jambo hili tuache market force ndizo ziamue bei, ikitokea bei safari hii imekuwa mbaya mwaka kesho mnatafuta namna kutoa incentive ili kuwainua wakulima, lakini tunaanza kuangaika wote just because kuna eneo moja mazao yameanguka haiwezekani? Kwa sababu bajeti ya kununua tunaitoa wapi? Tukiamua kununua sisi tunatowa wapi bajeti? Bajeti tumeipitisha hapa ndani kwahiyo, mimi ningeiomba Serikali tuache market force zi-determine biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe Serikali, tuache biashara tupo kwenye soko huria, kurudi kwenye command economy maana yake itabidi tuanze kuleta tume ya bei, tukileta tume ya bei, tukileta tume ya bei tutarudi kule kule, wako watu wanasema tu-own sisi unajuwa maana on lazima uweke mtaji, ukipata hasara lazima uweke mtaji mwingine, kitakachotokea tutashindwa kufanya yale makubwa ambayo ni ya Kiserikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala la watu wa TRA, task force nilishalisema huko nyuma, jamani naombeni biashara zinafungwa, niwaombeni biashara ni mahusiano. Mwaka 1987 Mahathir aliulizwa na Rais Mwinyi kwanini Malaysia inafanya vizuri, jibu lake ilikuwa nini? Wakiwa kwenye Commonwealth ya Zimbabwe akasema mimi ninafanya vizuri kwa sababu kuna asilimia 30 ya kila anayefanya biashara kwenye Malaysia yangu.

Kwa hiyo ninachosubiri ni asilimia 30 kazi yangu ni kuweka mambo mazuri ili tupate asilimia. Juzi ameingia at 94 anaulizwa anasema shughuli yangu mimi ni kulinda 24 percent kwamba wafanyabiashara anawawekea mazingira mazuri wao ndiyo partners wangu na sisi partners wetu ni wafanyabiashara, tunalo jukumu la kuwalinda, tunalo jukumu la kuweka mazingira mazuri ili wakifanya vizuri tutapata faida asilimia kubwa itaongezeka nchi itaenda mbele.