Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Awali ya yote niombe Mheshimiwa Waziri atakapokuja kuhitimisha atuambie kwanini kwenye Mpangu huu hatuoni Hospitali ya Kanda ya Kusini, haipo kwenye mpango huo, haionekani kabisa kwa hiyo hatuelewi kama haitakuja kutekeleza ujenzi wake kuendelezwa au vipi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hilo niseme kwamba wafanyabiashara siku zote wanabembelezwa au kunatakiwa kuwe na majadiliano yenye kuleta tija na sio vitisho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachokiona watu tukisema biashara zinakufa mnasema zinazaliwa zingine. Wewe hata ukiwa na watoto 10 hautamani hata mmoja afe, isipokuwa unachokuwa unatamani uzae wengine waongezeke. Sasa mtu leo akiona biashara zinafungwa anashangilia kwamba wale walikuwa wezi, walikuwa nini! Baba yangu Dkt. Mpango huko tunakoelekea sio kuzuri.

Mimi nakusahuri kwa nia njema kabisa kaa na wafanyabiashara, muelewane, muone vikwazo vyao, mnatakiwa mtatue vipi na mfikie negotiation, ukija kwa mfano kwenye suala la korosho, watu wameitwa wamekaa mezani, wameitikia labda kwa hofu baada ya kuitikia tumefuata nini wewe mwenyewe unajua mimi sina la kulieleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumzie hili la kusema kwamba kuna wafanyakazi wachache TRA, vifaa havitoshelezi; ni kweli hata ukisoma ripoti ya CAG imeeleza Halmashauri ya mama yangu pale Dkt. Kijaji inatakiwa kuwe na mashine 100, ziko 22 kwa mujibu wa ripoti ya CAG. (Makofi)

Sasa mimi nishauri mzee wangu Mkuchika hapa wa Utumishi, hebu muangalie wapatikane wafanyakazi wa kutosha kwa ajili ya TRA, kutokuwa na wafanyakazi wa kutosha ndiyo huko kunakosababisha wale wachache wanawafikia watu wale wale kila siku, wanawalazimisha kulipa kodi zisizowezekana wakati kuna sehemu zingine mnaziacha. Kidogo kidogo hujaza kibaba kuliko mnapotamani mkamue ng’ombe kwa kiasi kikubwa, matokeo yake mnamfilisi, anakufa! At the end of the day hamfaidiki ninyi wala hafaidiki yule mfanyabiashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna jambo lingine ninalotaka nilizungumze, ukiangalia kwenye mpango nimesoma kwenye hotuba ya Kamati wanasema kwamba bajeti ijayo mnapendekeza iwe trilioni 33.5 kutoka trilioni 32.47 na wakati huo huo utekelezaji ulikuwa 57%. Sijaelewa ni kwanini mnataka iongezeke wakati huo huo ukienda kwenye misaada na mikopo mnasema imepungua lakini kuna ongezeko la asilimia 26.3 kwenye pendekezo lijalo. Hii pesa inatoka wapi wakati mnasema imepungua, kwa nini tena mnazidi kuongeza na kwa nini wamepunguza?

Je, mmefanya analysis mkajua kwanini inapungua? Mahusiano yetu na hizo nchi wahisani yakoje? Labda ndiyo yanasabbisha haya mambo kwa hiyo utakapokuja kuhitimimisha naomba tupate majibu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala langu lingine ninalotaka kulizungumzia nataka kuzungumzia mradi wa gesi katika Mkoa wa Mtwara. Kuna issue ya LNG plant pale Lindi nataka kujua Serikali hivi vitu vimewashinda au mna mkakati gani wa dhati wa kuhakikisha vinatekelezeka?

Mheshimiwa Mwenyekiti, endapo uwekezaji katika sekta ya gesi ungefanyika kikamilifu nchi hii ingekuwa na umeme wa kutosha na ninyi Wabunge ndiyo mlikuwa mnashangilia tunafanya uwekezaji katika gesi, gesi itatusaidia, gesi ina manufaa mengi, lakini leo wote tumegeuka tunashangilia, wote mmegeuka mimi simo, wote mmegeuka mnashangilia Stiegler’s Gorge habari ya gesi tena basi! Sasa tunakwenda wapi? Our vision ni nini? Kwa sababu kwenye gesi tungepata viwanda vya mbolea, kwenye gesi tungeongeza ajira na vitu kama hivyo.