Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naipongeza Serikali kwa kazi zote inazozifanya na jinsi mpango huu ulivyotengenezwa na unavyotupa direction ya wapi tunapokwenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kusema jambo moja kwamba kwenye mpango huu sijaona ule mradi wa umeme wa Kakono ambao unazalisha megawatts 78. Benki ya Maendeleo ya Afrika ilishamaliza kazi yake na kuna vitu vilikuwa vinaendelea lakini siuoni kwenye mpango hapa. Waziri atakapokuja atuambie huu mpango umefikia wapi kwa sababu megawatts 78 siyo kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la maji linaonekana kwa nchi ni tatizo kubwa sana. Nashauri tuongeze Sh.50 kwenye mambo ya simu, tulete hizi pesa kwenye maji baada ya miaka miwili tutakuwa hatuna madeni lakini miradi mingi ya maji nchini itakuwa imemalizika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye kilimo nataka kushauri kwamba tunaweza kuigawa nchi yetu kwa zone, nimeona kwenye mpango hapa ukionyesha mikoa tofauti tofauti, tuigawe nchi yetu kwenye zone lakini tunapofanya zoning tutengeneze zile agro-processing centers huko huko ambazo zitaweza kuwa-managed na Watanzania na foreigners watakaokuja ku-invest pesa zao wakae na Watanzania huko huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri hawa investors watakaokuja kwenye hizo agro-processing plant katika maeneo hayo washirikiane na Watanzania. Kama Mtanzania anaweza kuingiza 30% aendelee yule mwekezaji akija na 50% aendelee, 20% iwe ni ya wale outgrowers wadogo wadogo waweze ku-manage uchumi kwenye vile viwanda vitakavyokuwa kwenye maeneo hayo ili growth ya economy iende sambamba na uhalisia wa maisha ya watu wetu tunaowaona kule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kufanya hivi ita-protect wale wakulima wadogo kwa sababu tulipobinafsisha hivi viwanda vya chai anazalisha ile chai yake akimaliza ana- determine chai price ya yule mkulima ambaye ni outgrowers. Kwa hiyo, mwisho wa siku yeye akisema anapunguza bei anapunguza kwa sababu already ana mashamba. Suala hili naomba Serikali iliangalie sana kwamba anakuwa na kiwanda, hana involvement na shareholders wadogo mwisho wa siku lazima awanyonye na awaamulie anavyotaka, atawamaliza na mwisho wataning’inia bila mazao yao kununuliwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili litasaidia jambo lingine kwamba hata kama atakuwa na hicho kiwanda atazalisha mwisho wa siku atakachofanya chochote kile kwa sababu outgrowers wetu na wao wana share pale ni wanufaika wa ile income atakayopata. Kwa maana hiyo, itatusaidia hata ku-protect price ya wale wakulima. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo lingine hawa foreigners watakapokuja nao watatusaidia ku-oversee masoko ya nje ya haya mazao tunayozalisha. Leo tumepata shida ya mbaazi kwa sababu hatuna watu nje. Leo tunapata shida ya korosho ni kwa sababu hatuna watu nje lakini ingekuwa tunabangua korosho hizi siasa uchwara usingezisikia Mtwara, usingesikia udalali, usingesikia kelele pale Mtwara kwenye korosho kwa sababu wale wakulima wenyewe wangekuwa ni shareholders kwenye zile agro- processing plants ambapo ni beneficiary, nani angezalisha siasa pale?

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Uganda inakwenda kuwa nchi ya kwanza Afrika kwenye uzalishwaji wa maziwa na teknolojia wameichukua Tanzania ten years back. Niombe Mheshimiwa Waziri hebu tafuta timu ya watu kutoka Ofisi yako ya Mipango, Kilimo, Mifugo, Uvuvi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TIC, Benki ya Kilimo na Benki Kuu, team up hawa watu waangalie ni mbinu gani tunaweza kuzitumia kuhakikisha kwamba Tanzania inaweza kuwa the biggest producer of milk Barani Afrika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Uganda leo wana-export zaidi maziwa na kwenye contribution ya uchumi wao sasa hivi maziwa yanaenda kuiondoa kahawa na chai, kahawa inaenda kuwa ya tatu, chai inakuwa ya pili na maziwa yanakuwa ya kwanza. Ukiangalia ecological area na environment yetu sisi tuna maeneo makubwa lakini yenye weather sawa na Uganda, kwa nini hatujafanikiwa kwenye sekta hii?

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Mheshimiwa Dkt. Mpango asije kusema tunahitaji big investment kwenye hili, hakuna pesa nyingi. Shida tunayoipata ni kwamba hatuna access ya grants kwenye agro-business na kwa wakulima wetu. East Africa Tanzania ni ya mwisho ku-access grants, Ulaya watu wanashusha grants Kenya na kwenye nchi nyingine, wanaweka miundombinu na vitu vyote wakimaliza wanakwambia wewe fanya kazi, maisha ya raia wao wanakuwa vizuri wewe unakusanya kodi. Mheshimiwa Dkt. Mpango hapa usije kutuambia unahitaji hela, hakuna hela, wale watu wana uwezo wa kua-access grants. Team up your people waende wakafanye kazi hizo na sisi wakulima wetu wa-access grants waweze kufanya kazi na sisi tupate msaada. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, Mheshimiwa Dkt. Mpango wala usije ukatuambia chochote nenda katafute washauri Marekani hata wapi waje wakushauri wakuambie ni mipango gani inatufaa. Wewe usitusikilize sisi wanasiasa, panga pangua, panga vitu vyako sisi tunataka kuondoka kwenye umaskini na hizi shida tulizonazo. (Makofi)

T A A R I F A . . .

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nimesema wanasiasa siyo Wabunge, maana hata kule mtaani tuna wanasiasa kwani wanasiasa ni sisi peke yetu tuliomo humu ndani? Hatuna waandishi wa habari wanaamka asubuhi wanatangaza ya kwao? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa namshauri Waziri wangu, mambo mengine usiwe unatuaga, wewe nenda kachape kazi tunatafuta maendeleo, hapa tunakuja kuku- support mambo mengine tu. Wewe unatuaga kufanya nini?

Tafuta pesa na wataalam huko watusaidie, Tanzania hatuwezi kuifunga, hii siyo kisiwa, nchi imeshakwenda na duniani nyingine, Watanzania wanatakiwa watoke na wapate ajira. Tafuta technical persons watusaidie, sisi siyo kisiwa, siyo kwamba ni wajinga lakini kupata ushauri na akili ni kuhemea brain, unaingiza hapa tunapata maisha, watu wanahitaji kubadilika, wewe tusaidie. Mtu mwingine akija kwako analeta siasa unamsikiliza, nunua ream za karatasi mwambie nenda kaniandike ya kwako kwenye makaratasi akupe nafasi ya kufanya kazi uweze kupumua. (Makofi/ Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kushauri jambo lingine la mwisho kwamba Watanzania hawafanyi kazi. Nchi nyingine they are working over night, kadiri wanavyofanya kazi usiku na mchana ndivyo zile mashine zinatema kodi. Saa nne tumelala, saa mbili tayari, Dar es Salaam saa tatu wako barazani wanazungumza habari ya wanawake, mama ana tako, mama ni mnene, utafanya lini hiyo biashara, utapata kodi saa ngapi? (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuombe na Bunge hili mnikubalie nchi hii ifanye kazi usiku na mchana. Watu waondoke kwenye ufuska na kufikiria mawazo mabaya na kutukanana hovyo hovyo, tufanye kazi, watu wafanye kazi mchana na usiku. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukichukua Kariakoo nzima leo, ukaamua maduka yote fungueni mchana na usiku, you are creating employment to our graduates ambao wako mtaani wanacheza na simu. Vilevile una-create employment kwa watu ambao ni jobless wanafanya kazi mchana wengine wanafanya kazi usiku, tunaongeza ajira, shift zinakuwa mchana na usiku halafu kodi inaendelea kukusanywa. Kwani saa nane usiku mashine ya EFD haitoi risiti, inatoa. Je, wewe Mheshimiwa Dkt. Mpango haupati fedha? Nashauri tuanze biashara usiku na mchana. (Makofi/ Kicheko)


Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kushauri jambo lingine kwamba huu mpango wetu sisi twende kushauri Serikali lakini tusibeze yale yanayofanyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la mwisho nashauri kwamba Benki ya Kilimo TADB, niungane na Mheshimiwa Saada, Mheshimiwa Dkt. Mpango angalia ni namna gani unaweza kufanya isiwe kama commecial bank iendane na hali halisi ya mazingira ya Watanzania, waweze kukopesheka vinginevyo zile pesa zitakaa pale, utalaumu watendaji, utawafukuza, utaajiri wengine na pesa hazitatoka. Mheshimiwa Waziri angalia ni namna gani ya kushusha zile pesa katika mfumo ambao ni reasonable. Utamwambia aandike business plan na yeye ana heka zake mia mbili anataka akakope trekta na TADB inatakiwa impe hela PASS im-garantee atatokea wapi? Punguzeni masharti, angalieni ni namna gani ya kui-handle ile benki ili iweze kwenda sambamba na life brain na stahili za wakulima wetu kule kwenye grassroot. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naunga mkono hoja.