Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kabla sijaanza kuchangia, naomba Bunge hili lijue mimi ni mjumbe wako wa Kamati ya Kanuni za Bunge na wewe kama Mwenyekiti wangu umenifundisha kweli kweli kuzisoma kanuni hizi na kuzizingatia. Kwa taarifa hiyo, naomba niwakumbushe Wabunge wenzangu kwamba tutumie tu lugha nzuri pale tunapokuwa tunachangia na tusiseme uongo Bungeni, tunamlazimisha Mheshimiwa Spika wakati mwingine kutubeba lakini si jukumu lake, tuwe na busara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze kwa kutoa quotation ya Mheshimiwa Makamu wa Rais, Mama Samia Hassan Suluhu alipokuwa akiutubia katika sherehe za utoaji za tuzo za heshima, wakati ule alikuwa ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano. Mama Samia Suluhu alisema yafuatayo, imeandikwa kwa Kiingereza tafsiri nitakayoitoa haitakuwa ya moja kwa moja lakini alisema; “On the bilateral front the European Union is Tanzania key development partner both in terms of magnitude and financial support”.

Akaendelea kusema zaidi; “Let me therefore avail this opportunity to express our sincere gratitude and appreciation for the European Union in valuable assistance which has enabled the Government of Tanzania in many ways undertakes social economic development programs for sustainable development”.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa wajomba zangu kama Mheshimiwa Mzee Musukuma, Mama Samia Hassan Suluhu wakati anahutubia mkutano huu...(Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, alikuwa anamaanisha kwamba anatambua mchango mkubwa wa wadau wa maendeleo ambao wanatuchangia na bajeti yetu ya Tanzania. Mama Samia Hassan Suluhu ambaye sasa ni Vice President alitambua kabisa kwamba ili tuweze kutengeneza mpango wa maendeleo unaotekelezeka Tanzania haiwezi kujiendesha kwa pato la ndani peke yake.

T A A R I F A . . .

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama alivyoniita Salome ameniita kwa Kisukuma, ni mjomba wangu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mama Samia Hassan Suluhu, nikianza kwa kum-quote alitambua mchango mkubwa wa wadau wa maendeleo kwenye bajeti yetu akiamini kwamba ili tuweze kufikia malengo ya mipango tunayoitengeneza ni lazima tuheshimu na tuthamini wadau wakubwa wa maendeleo katika nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ilivyo hivi sasa katika nchi yetu, mimi naomba nisisitize, kuna hali ya sintofahamu kubwa sana kati ya mahusiano yetu na wadau wetu wa maendeleo. Labda nianze na ndani ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wafanyabiashara kama tulivyoahidiwa wataishi kama mashetani wanaishi kama mashetani. Wafanyabiashara hawana security. Juzi tumeshuhudia billionaire mdogo Afrika ametekwa, amejirusha mwenyewe, halafu ameenda kuhojiwa akiwa nyumbani kwake na Serikali ipo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwangu pale Shinyanga tunao wafanyabishara wa maduka ya kati. Siku za hivi karibuni kwenye vyombo vya habari, Waheshimiwa Wabunge wenzangu mlishuhudia, Mkuu wa Mkoa amekwenda pale anafanya operesheni sijui ya ukaguzi, maana operesheni zimeshakuwa nyingi siku kila mtu anafanya; kwenye operesheni ile amefunga kwanza maduka yote ya pale mjini bila kujali athari za kiuchumi za matendo ambayo anayafanya. Kafunga maduka yale, kawachukua wafanyabiasha kaita vyombo vyote vya habari, anawasimamisha mbele ya vyombo vya habari anawaambia wafanyabiashara wale eleza ulichokifanya, haya kiri kwamba ulifanya hivi, haya eleza hivi, kinyume na haki za binadamu, utu, sera ya biashara na sera ya uwekezaji. Ndipo tulipofika kwa sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, korosho na kahawa zinakufa. Mazao yote ya biashara ambayo kimsingi kama walivyoeleza Wabunge wenzangu ndiyo yanayochangia kwa kiasi kikubwa tuweze kutekeleza mpango huu ambao leo tumekaa Dodoma tunaujadili yanakufa lakini nobody cares. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikupe taarifa iliyotokea jana. Jana kwenye Citizen TV kwa Wabunge wenzangu ambao mmetazama, wavuvi 36 wa Kenya wamezuiliwa kwenye Ziwa Victoria wakisemekana kwamba ni wavuvi haramu na wamekatwa na watu wa Usalama wanaambiwa hawawezi kuachiwa mpaka walipe faini ya milioni 26. Je, watu wa Usalama wanatoza faini? Uvuvi haramu mamlaka husika zinajulikana lakini sasa ndipo tulipofika leo, tunasema refa wewe, mchezaji wewe, mfunga goli wewe, mtu mmoja anafaya kila kitu na niliwahi kusema humu ndani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimetoka kusema asubuhi habari ya watu ambao ni watetezi wa waandishi wa habari Tanzania. Kuna sintofahamu kubwa, watu wamekuwa detained hotelini wamenyang’anywa passport.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema leo Serikali itoe kauli kukemea vitendo hivi ambavyo vinaweza kutuingiza kwenye migogoro ya kidiplamasia, hatuelewani humu ndani. Mpaka natamani neno diplomasia lingetafutiwa neno lingine labda ni msamiati mgumu ambao viongozi wa Serikali hawaelewi. Wale watu wamekuwa detained BBC na CNN wame-report. Hivi inaleta image gani kwa nchi yangu leo kudhalilika namna hiyo kimataifa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri Mahiga alitoa statement baada ya Balozi wa EU kuondoka, akasema eti ameondoka kwa anavyojua mwenyewe, amepangiwa kazi nyingine sisi hatuwezi kujua. Hata hivyo, Balozi wa EU ametoa statement kwenye tovuti yake, anasema kuwa alifanya na mazungumzo na Serikali ya Tanzania na akaeleza grievances zake kwamba Tanzania hawaelewani na EU kwa sababu kuna uvunjifu mkubwa haki za bidanamu, Tanzania kuna shida kubwa ya utawala wa sheria, ameeleza black and white. Alikuja akafanya mazungumzo mpaka anaondoka nobody cares. Serikali, Waziri mkongwe mdiplomasia ninayemuamini anatoka public anasema ameenda kupangiwa kazi nyingine mimi sijui bwana, inawezekana tukaletewa mtu mwingine, recalling of an Ambassador is not a joke ,naharibu image ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasimama leo hapa kutaka kukuonyesha kwamba hawa European Union inachangia…

T A A R I F A . . .

MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwakumbushe Watanzania wenzangu kwamba leo tunapozungumza hapa ndani kwenye kwa Taarifa ya Hali ya Uchumi ya mwaka huu 2018, European Union yenye nchi 27,28 imechangia kwenye kahawa dola milioni 149.