Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikupongeze kwa uongozi wako wa kuhakikisha kwamba tunaitekeleza ipasavyo Katiba yetu Ibara ya 63(3)(c). Wewe unafahamu siku za nyuma tulikuwa hatufanyi hivi, lakini tangu tumeanza Bunge hili kila mwezi Novemba tumekuwa tukikutana na kutekeleza matakwa ya kikatiba. Kwa hiyo, napenda nikupongeze wewe binafsi kwa uongozi wako katika jambo kama hili, nashukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nami pia niende kwenye baadhi ya mambo ambayo napenda kuchangia kwa ajili ya kuboresha mpango kama jinsi ambavyo wenzangu wametoka kuzungumza. Jambo la kwanza ni eneo la vipaumbele vya mpango.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukitazama tuna hotuba tatu sasa tangu tumeanza, kuanzia 2016 mpaka sasa. Ukichukua hotuba ya 2016, ukatazama vipaumbele vya mpango, wakati ule viliitwa miradi ya kielelezo, ukaenda 2017, 2018 jambo moja ambalo naliona ni kukosekana kwa sequencing. Unaanza na mambo fulani mwaka unaofuata una-drop baadhi, hata ambayo hayajatekelezwa kabisa, mwaka unaofuata una-drop mengine, hata ambayo hayajatekelezwa kabisa, matokeo yake ni kwamba kila mwaka tunakuwa tunaanza upya bila kufanya yale ambayo tungekuwa tumepaswa kuyafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukitazama mwaka 2016 kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri Mpango ukurasa wa 18, jambo la kwanza kabisa Makaa ya Mawe Mchuchuma na Chuma cha Liganga. Ukienda mwaka 2017 ukurasa wa 29 lipo lakini kuna jambo la Mji wa Kilimo wa Mkulazi limegeuzwa kuwa shamba, halafu ukija 2018 hayapo kabisa na ni kwa sababu huko nyuma tumekuwa tukishindwa kuyatekeleza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukitazama hilo maana yake ni kwamba tunakuwa tunapiga mark time, tunakutana, tunajadiliana, tunatoa mawazo, mwezi Februari yanakuja tunayaidhinisha vizuri, tunaenda kwenye bajeti, tunaweka bajeti na nitakuja kwenye hiyo hoja ya bajeti credibility halafu hakuna kinachofanyika. Mfano dhahiri kabisa ni hili jambo la Mchuchuma na Liganga ambalo tangu 2016 linaonekana kwenye mpango kama mradi kielelezo, kufika sasa limeondolewa kabisa kama mradi kielelezo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba hili lifanyiwe marekebisho. Tujaribu kurudi 2016 tuangalie ile miradi vielelezo na tui-update utekelezeaji wake. Kuna ambayo imetekelezwa kama Reli ya Kati na kadhalika na ile ambayo imeachwa tuweze kuiboresha ili tutakapokuja mwezi Februari, tuwe na kitu ambacho tumeanza nacho kuanzia mwaka 2016.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni suala la credibility ya tunachokijadili hapa. Mwaka 2016 tulijadili na kukubaliana kwamba Serikali ikatenge shilingi trilioni 13.2 kwa ajili ya utekelezaji wa mpango wa maendeleo ambao tunaujadili kwa siku tano, wakaenda wakatoa trilioni 5 tu. 2017 tukasema zikatengwe shilingi trilioni 12, zikaenda zikatengwa trilioni 6 tu. Mwaka 2018 ndiyo tunapendekeza sasa zikatengwe tena shilingi trilioni 12. Hii inaonesha dhahiri kwamba kama hatutakuwa makini na kuanza kuhitaji uwajibikaji upande wa Serikali, tunapiga porojo. Kwa sababu kile ambacho tunakubaliana kukifanya wenzetu wakakifanye hakifanywi vile ambayo tumekubaliana kikafanywe. Hiyo ni problem ya credibility ya mpango na bajeti yenyewe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la tatu, limezungumzwa kidogo na Mheshimiwa Bashe, tuna tatizo kwenye exports. Mwaka 2016 tuli-export bidhaa za dola za Kimarekani bilioni 9.8, kwa mujibu wa taarifa ya Serikali yenyewe. Sasa hivi kwa taarifa ambayo Mheshimiwa Waziri Mpango ametuletea leo exports zetu zime-drop kwa dola bilioni moja. Tayari mwezi wa Agosti tumepata negative balance of payment for the first time in the last three years. Sekta ambazo zimekuwa zikituokoa hasa mwaka jana ni tatu, utalii, transit trade bandarini pale na korosho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana korosho zimetuingizia fedha za kigeni zaidi ya kahawa, pamba, chai, tumbaku, karafuu, pareto, katani combined. Mwaka huu production inashuka sana, kwa hiyo tunakwenda kwenye balance of payment crisis. Serikali inafahamu hatuendi huku kwa sababu ya bahati mbaya labda natural calamities au nini, tunakwenda huko kwa sababu ya kwanza mipango mibovu lakini pili utekelezaji mbovu wa mipango hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nilitarajia leo tungeweza kuletewa kwamba tunaenda kwenye crisis maana mafuta yanaenda kupanda bei na Mheshimiwa Waziri Mpango anafahamu sasa hivi tuta-import sana kwa sababu ya miradi mikubwa ambayo tunaitekeleza. Tuna- import mataruma ya reli, aibu lakini ndiyo hivyo tuna import. Maana yake ni kwamba by Desemba tunaweza tukawa na crisis kubwa ya balance of payment. Ni nini mpango wa Serikali wa kuhakikisha tunaongeza huo uzalishaji? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali pia imezungumzia katika utekelezaji wa mwaka huu suala la ASDP II. Katika ASDP II kuna suala la mbegu za GMO, mbegu ambazo sote tunajua zinakwenda kuielekeza nchi yetu kuwa koloni la kampuni kubwa za mbegu duniani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nita-share na Mheshimiwa Waziri wa Fedha barua ambayo mtafiti mmoja wa Kitanzania amefanya, anaitwa Dkt. Richard Mbunda ambaye aliandika barua kwa Mheshimiwa Rais kuhusiana na suala hili kwamba tunaenda kuua mbegu za asili, tunaenda kuwaua wakulima wadogo, tunajikuta sisi kazi yetu ni ku-import mbegu kutoka kwa Monsanto na kampuni kubwa za mbegu na hatimaye ule uhuru wetu wa chakula (food sovereignty) tunakwenda kuiondoa. Napenda tupate kauli ya Serikali hasa sera yetu kwenye GMO ni nini, tunakubali kwenda kujinyonga na kuwa nchi ambayo inategemea kampuni kubwa kuleta mbegu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ni jambo ambalo napenda Wizara ya Fedha ilitazame vizuri. Tuna tatizo la reporting accounting, nitaliandika vizuri kwenye mchago wa maandishi. Ukitazama taarifa ya Serikali ya sasa hivi tunarudi kwenye lile tatizo la 1.5 trilioni tena. Ukitazama kwenye report ambayo Serikali imetoa, page 10 na page 11 utaona taarifa ya mapato ambayo Serikali ime-report kuwa imeyakusanya mpaka mwezi Juni na taarifa ya matumizi ambayo Serikali imesema imetoa fedha hizo kwenda kwenye mafungu, kuna tofauti ya shilingi trilioni 2.1. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbaya zaidi, ukitazama hotuba ya Mheshimiwa Waziri ya mwaka 2017, kama ingekuwa imezingatiwa hii na Treasury tatizo ninalolizungumza sasa ambalo PAC wanalifanyia kazi la 1.5 trilioni lisengekuwepo kwa sababu wali-report sahihi vile ambavyo wamekusanya na vile ambavyo wametoa, wakatazame ukurasa wa 11 na 12. CAG baadaye alionyesha kwamba kilichokuja kuripotiwa kuna hiyo tofauti ya 1.5 trilioni; sasa hivi 2018 tatizo limejirudia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi sitaki kusema kwamba kuna wizi, namjua Mheshimiwa Dkt. Mpango si mwizi na sisi watu wa Kigoma hatuna historia ya wizi lakini kuna tatizo kubwa la accounting. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.