Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. SILVESTRY F. KOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kupongeza na kuishukuru Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi kwa kazi kubwa inayoifanya katika miradi mikubwa ya maendeleo, bila kusahau mradi mkubwa wa umeme ambao utatutoa katika matatizo ya umeme wa Stiegler’s Gauge ambao Mheshimiwa Rais ameuvalia njuga na tunamuunga mkono; mradi wa reli ambao utaondoa tatizo la usafiri, ikiwa ni pamoja na Wabunge kuja Dodoma itakuwa ni chini ya saa tatu, tunaunga mkono na tuna imani tutainua uchumi wetu kwa kiasi kikubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niendelee kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa sababu ameendelea kutekeleza miradi mikubwa katika maeneo mbalimbali. Pwani tuna mradi wa barabara, Awamu ya I, kutoka Ubungo mpaka Kibaha ambayo ni six lane pamoja na Daraja la Ubungo. Nilisikia mtu akisema kwamba Daraja la Ubungo halina thamani kwa wakulima vijijini lakini ukweli ni kwamba mazao ya wakulima yanayotoka katika vijiji yatafika Dar es Salaam na yatanunuliwa kwa bei nzuri na mkulima kule atafaidi lakini hata sisi watoto wa huyo mkulima na ndugu zao tutatumia daraja lile na uchumi utachangamka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yote haya yanafanyika kwa ajili ya Watanzania. Mheshimiwa Rais na Serikali yake atajenga miradi hii, haondoki nayo inabaki, tutaendelea kuitumia na atakapomaliza kipindi chake, watoto wetu na wajukuu wetu. Jambo kubwa ni sisi tumuunge mkono Mheshimiwa Rais na Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi na tuishauri iendelee kufanya kazi nzuri ili maendeleo katika nchi yetu yaweze kuja kwa haraka.

Nataka niseme na kumpa moyo Mheshimiwa Rais kwamba hata wafanyabiashara walio wengi sasa voluntarily wanalipa kodi kwa sababu wanaona matokeo ya kodi zao kwamba zinakwenda kufanya mambo makubwa ya maendeleo katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nishauri tu kwamba katika miradi hii, iko miradi mikubwa na ambayo ni complicated kuiendesha kama Shirika la Ndege na ninajua ndege nyingine zinakuja, tusiogope kushirikisha experts. Tushirikishe experts wenye uzoefu kutoka nje, washirikiane na management ya Kitanzania ili tuweze kufikia malengo na mafanikio ya miradi hii mikubwa. Nina imani kama tuta-blend skills na expertism kutoka nje na ndani ya nchi ni wazi kwamba tutaweza kupeleka mbele gurudumu la maendeleo kwa kuhakikisha miradi hii inakwenda kuleta mafanikio makubwa na kuibadilisha kabisa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka vilevile nizungumzie suala la mazingira ya kufanya biashara. Nafahamu ili mipango hii ya maendeleo iweze kufanikiwa ni lazima mazingira ya ndani ya kufanya biashara yaboreke. Najua Serikali imeshachukua hatua ikiwa ni pamoja na kutengeneza ile blueprint ya kuhakikisha kwamba taasisi zinazohusika na kudhibiti ufanyaji wa biashara zinakuwa ni msaada kwa wafanyabiashara wa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachokiomba hapa sasa, Serikali ihimize utaratibu huu, ile blueprint sasa iende kwenye vitendo ili isaidie ukamilishaji na utekelezaji wa miradi hii ya maendeleo na ili kila Mtanzania aweze kufanya biashara katika hali ambayo haina usumbufu na yenye tija. Masuala ya kodi yakae vizuri, masuala ya compliance mbalimbali ikiwa ni pamoja na TBS, TFDA pamoja na taasisi nyingine ziweze kumsaidia mfanyabiashara achangamshe uchumi, kodi zilipwe na hatimaye tufikie malengo yetu. Naomba blueprint sasa iende kufanyiwa kazi na iende kwenye utekelezaji na isiendelee kubakia katika vitabu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali yetu imechukua hatua na hatua hii ni hapohapo katika kwenda kuboresha mpango wetu wa maendeleo. Imechukua hatua ya kulinda viwanda vya ndani ikiwa ni pamoja na kuongeza baadhi ya tariffs na imechukua hatua hata ya kupunguza kodi katika bidhaa mbalimbali. Lengo na madhumuni siyo kumfaidisha mfanyabiashara peke yake bali pia kumfaidisha Mtanzania aliye kijijini anayetumia bidhaa zile. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini baadhi ya wafanyabishara sasa hawafanyi hivyo, matokeo yake baada ya kuweka tariffs za bidhaa za nje zikaenda juu na wenyewe wanapandisha bei ya bidhaa zao badala ya ku-capitalize katika kuuza zaidi kwa sababu bidhaa zao sasa ni bei rahisi. Niombe sana, azma ya Serikali kufanya hivyo ni kulinda viwanda na kumrahisishia Mtanzania kupata bidhaa kwa bei nzuri na kuhakikisha viwanda vinazidisha uzalishaji. Rai yangu hapa, wenye viwanda na wafanyabiashara walichukue jambo hili au wachukue hili punguzo au ongezeko la bei za bidhaa kutoka nje kuzalisha zaidi na wasiongeze bei kumuumiza yule mlaji wa mwisho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika miradi hii mikubwa ya maendeleo ambayo Serikali imejikita ni wazi kwamba utekelezaji wake unahitaji fedha nyingi na ili fedha ziweze kupatikana ni lazima ulipaji wa kodi uwe mkubwa na ili ulipaji wa kodi uweze kuwa mkubwa ni pamoja na Serikali kwa makusudi kuchangamsha biashara za ndani. Ili biashara za ndani ziweze kuchangamka ni pamoja na kuhakikisha madeni mbalimbali ya wafanyabiashara Serikalini yanalipwa kwa sababu, the main stimulant ya uchumi katika nchi yoyote ile ni Serikali. Katika uchumi wa nchi yetu ulio mdogo ni wazi kwamba mwajiri wa kwanza wa makampuni madogo katika nchi ni Serikali. Kwa hiyo, nina uhakika Serikali ikijikita katika kulipa madeni siku ya mwisho zile fedha zitarudi katika utaratibu wa kodi na uchumi utachangamka na miradi hii itaweza kukamilika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi hii na hakika naunga mkono hoja na tuko pamoja katika kuhakikisha miradi na mipango hii ya maendeleo inatakamilika. Ahsanteni.