Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kukushukuru kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kutoa mchango wangu katika haya maandalizi ya mpango wa bajeti 2019/2020.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii nianze kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Mpango pamoja Naibu wake kwa maandalizi ya mpango mzuri na niseme tu kwamba katika mpango huu yapo yale mambo ambayo yamepewa kipaumbele kama kuendelea kufanya kazi ya ununuzi wa ndege, lakini vilevile mradi wa Stiegler’s Gorge pamoja na wa reli ya kisasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia leo katika nchi yetu Tanzania ni nchi ambayo tuna vivutio vingi vya watalii, lakini ni kwamba wenzetu Wakenya wanatushinda watalii kwa wingi na mapato ya utalii ni kwa sababu hatuna direct flight za kuja Tanzania. Kwa hiyo, leo nilipoona humu tunataraji kwa na direct flight za kutoka China kuja Tanzania, kutoka India kuja Tanzania huo ni mwanzo mkubwa na mwanzo mzuri unaonyesha tunatarji na sisi kupata mapato ya fedha za kigeni kutokana na watalii kwa hiyo nasema big up katika hilo. Lakini ukiangalia mradi wa Stiegler’s Gorge ambao baadhi yetu tunaubeza tunatambua kwamba ili nchi yetu iweze kuendelea inahitaji muwekezaji na mwekezaji yoyote akitaka kuwekeza moja wapo ya factor kubwa anayoingalia ni gharama ya uendeshai ambayo anakwenda kwenye umeme.

Kwa hiyo, wote tunafahamu gharama za umeme wa maji kwa namna zilivyo chini, kwa hiyo, matokeo yake ni kwamba tuna nafasi kumbe ya kuvutia watu wengi wawekezaji wengi kuleta viwanda vyao nchini. Kwa sababu ya gharama za umeme tunatarja kuwa chini, kwa hiyo, tunaendelea kuishukuru Serikali kwa mpango huo. Lakini Mheshimwa Dkt. Mpango nikuombe tu ufanye jambo ambalo ni la haraka na litaonesha matokeo ya haraka. Kwenye huu mpango wa reli ya kisasa leo Watanzania wengi tukiwemo Mikoa ya Mara, Mwanza, Kagera pamoja na wote ambao usafiri wa Dar es Salaam kuja kwenye mikoa yetu tunatumia zaidi ya siku moja maana yake abiria lazima walale njiani.

Sasa kwa sababu tumeona kutoka Dar es Salaam kuja Morogoro ni kilometa 300 na mpaka sasa umeshatengeneza 24% ni mategemeo yangu by mwaka kesho au mwaka kesho kutwa mwanzoni kile kipande kitakuwa kimekamilika. Sasa nini kifanyike wakati huu ujenzi unaendelea hebu tuanze kabisa kununua vichwa vya tayari tayari kwa ajili ya treni, kwa ajili ya kuleta abiria hapo, pamoja na mabehewa lakini pamoja na stand kwa ajili ya mabasi, matokeo yake yatakuaje kutoka Dar es Salaam treni iwe inaondoka saa 11 naamini saa 12 itakuwa Morogoro, abiria wote wa mikoani wakipanda pale saa 12 tafsiri yake kwamba hakuna abiria hata mmoja atakayelala njiani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ninaamini huo mpango peke yake utaanza kuonesha matokeo ya haraka wakati huo ujenzi wa reli kadri unapofika kwenye kituo kimoja mfano ukifika Dodoma utaratibu mwingine unaendelea yaani huduma zote zinaendelea kupatikana kuliko tutakaposema tusubiri tujenge kwa muda mrefu au kipande kirefu halafu ndipo hizo huduma zianze kutolewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini baada ya kuwa nimesema hayo sasa katika mpango huu wa 2019/2020 wote tunafahamu kwamba kilimo ndio uti wa mgongo, kilimo kinachukua 70% ya Watanzania, nini kifanyike kwenye upande huo hebu kama tunahitaji kuajiri watu wengi na maisha yetu yawe mazuri lazima tujikite kwenye kilimo cha umwagiliaji na tutakapojikita kwenye kilimo cha umwagiliaji na tutakapojikita kwenye kilimo cha umwagiliaji tutambue mabonde yaliyopo katika nchi hii na mabonde hayo leo tunaweza kuamua mfano tusema tunalima mpunga, katika mabonde yote tuliyonayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini baada ya kuwa nimesema hayo sasa katika mpango huu wa 2019/2020 wote tunafahamu kwamba kilimo ndio uti wa mgongo, kilimo kinachukua 70% ya Watanzania, nini kifanyike kwenye upande huo hebu kama tunahitaji kuajiri watu wengi na maisha yetu yawe mazuri lazima tujikite kwenye kilimo cha umwagiliaji na tutakapojikita kwenye kilimo cha umwagiliaji na tutakapojikita kwenye kilimo cha umwagiliaji tutambue mabonde yaliyopo katika nchi hii na mabonde hayo leo tunaweza kuamua mfano tusema tunalima mpunga, katika mabonde yote tuliyonayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukuzungumza zao la mpunga kwanza ni zao la biashara, lakini vilevile ni zao la chakula, lakini vilevile nchi zote zinazotuzunguka ni nchi ambazo zinahitaji mchele wa Tanzania. Ukienda Kenya, Uganda, Rwanda, Kongo na Zambia, mchele wa Tanzania ukiruhusiwa tu kuuzwa unao kila nchi unaupenda. Sasa nini kifanyike tukishaanisha hayo mabonde wakati mwingine tunaweza kutangaza wakandarasi kama tunavyotangaza kazi za bararaba. Tukasema tunahitaji mkandarasi hekta 2000 hizi zipo hapa, basi tunachohitaji wewe mkandarasi weka miundombinu ya irrigation watu watalima mfano zao moja kama niilivyosema la mpunga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukizungumzia zao la mpunga, mpunga ni zao hakuna kinachotupwa yale mabaki yake kwa maana ya majani mifugo inakula, zile pumba hata wale wachoma matofali sasa hawataharibu mazingira kwa kukata mita watatumia kuchomea matofali. Lakini sisi wote ni mashaidi zile wanaita rice polish kwa maana zile chenga zake ndio tunakula vitumbua, lakini na mchele wake tunauza.

Kwa hiyo, kumbe ni imani yangu kwamba kwa kulima mpunga ni zao ambalo linaweza likamsaidia Mtanzania yeyote yule na likapandisha kipato chetu na hela yenyewe haina kwamba soko limeanguka kwa sababu mahitaji ya soko yapo ndani na nje ya nchi. Kwa hiyo ni imani yangu tukikipa kilimo kipaumbele cha kwanza hasa kilimo cha umwagiliaji itatusaidia sana katika kuukomboa na kunyanyua kipato cha Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kipaumbele cha pili tufanye nini1 Kwangu mimi kipaumbele cha pili tukipeleke kwenye suala la uvuvi. Kwa bahati mbaya watanzania wengi kila fursa tunayoipata inabadilika tena inakuwa hatari kwa watu wetu. Leo wale watu waliopo baharini, waliopo Ziwa Tanganyika, waliopo Ziwa Victoria ni kilio kitupu. Ni kilio kitupu kwa sababu badala ya yetu sisi tuone namna kuwasaidia, kazi yetu ni kwamba mtu amekosea anapigwa faini ambayo haiwezi. Kwa hiyo, wale watu wetu wengine wanafungwa, kwa hiyo hali ya maisha inakuwa ngumu, lakini nini kifanyike?

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo ili watu wetu tuweze kuendeleza uvuvi, ili wale watu wetu waweze kuthamini maana ya uvuvi, kinachopaswa kufanyika hebu Serikali itenge fedha, tuwe na uvuvi ule ufugaji wa kufugia ziwani, ufugaji wa kufugia baharini kwa maana ya kutengeneza zile cage, ukishalianzia lile kwa vyovyote vile uvuvi haramu hautakuwepo kwa sababu wale wananchi wenyewe ambao ni wafugaji wa samaki wao wenyewe ndio watakaokuwa walinzi wa ziwa letu na walinzi wa bahari zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni imani yangu kwa kufanya hivyo kwanza watakuwa wanapata kipato lakini vilevile watakuwa walinzi wazuri katika maziwa yetu na bahari zetu kwa kuhakikisha kwamba uvuvi haramu haufanyiki. Lakini hata zile fedha ambazo watu wa patrol huwa wanawatoza wakienda kuwakamata wakati mwingine huwa wanawatoza shilingi milioni mbili mpaka shilingi milioni tano zile fedha zinapaswa ziwarudie, zirudi kwa kutengeneza miundombinu kama hiyo ili watu wetu waendelee kuona umuhimu wa uvuvi na imani yangu kwamba mambo yatakuwa mazuri na wale watu wetu watafanya vizuri zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo katika ushauri wangu tunapaswa tujikite, katika kuwasaidia wananchi wetu na Watanzania wetu, ni ukweli usiopingika kwamba leo yupo mtoto anasoma mpaka chuo kikuu, anatoka na bachelor yake ya sociology, lakini huyo mtoto ukimchukua na yule mtoto ambaye amesoma VETA akamaliza, huyu wa VETA bado yupo better of kuliko yule ambaye ana degree yake ya sociology.

Mheshimiwa Mwenyekiti, unakuta kwamba mpaka leo kipaumbele kikubwa tunakitoa zaidi kuhakisha kijana asome mpaka degree yake, kumbe kati ya eneo ambalo tunahitaji kuliendeleza tunapaswa kuendeleza maeneo ya vyuo kwa maana hivi vyuo vya certificate na diploma ambavyo watu wetu wataendelea kupata ujuzi na itawasaidi zaidi katika kujiajiri kuliko huu utaratibu ambao tunathamini zaidi wale watu ambao wana bachelor kumbe wakati mwingine bachelor yake anazidiwa na mtu mwenye certificate.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo naomba kuunga mkono hoja na kupongeza sana, ahsanteni sana.