Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii ili niweze kuchangia mapendekezo ya mpango wa mwaka 2019/2020.

Kwanza na mimi nianze kwa kutoa pongezi kwa Rais wetu mpendwa John Pombe Magufuli kwa kazi nzuri anayoifanya, hakuna mtu ambaye hakubaliani kwa utekelezaji wake, ndani ya miaka mitatu amefanya kazi nzuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili nichukue nafasi kupongeza Mheshimiwa Waziri wa Mipango pamoja na Naibu Waziri kwa kazi nzuri mliyoifanya bahati nzuri sana mimi niko kwenye Kamati ya Bajeti na ukisoma hivi vitabu ni vitabu ambavyo vinaeleweka vizuri kabisa.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa vile hapa tunafanya ni mapendekezo ya mpango naona kuna watu wengi labda hapa hatujaelewa vizuri haya ni mapendekezo ya mpango ni mpango ambao tunaupendekeza sio mpango tunaoukosoa, sasa mimi naomba nipendekeza kwa sababu katika mpango inaonyesha kwamba malengo makubwa ni kupunguza umasikini na bahati nzuri sana ameonesha data kwamba kutoka 2012 mpaka 2020 kiwango cha umaskini kitapungua mpaka kitafika asilimia 16.7 hii nimeona ni nzuri sana. Sasa ili tufikie asilimia 16.7 ambayo tumepunguza kiwango cha umaskini nini kifanyike. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi sasa hivi walio wengi tunaomba sana tuimarishe sana na tuboreshe kwenye sekta ya maji. Sekta ya maji ni muhimu sana, bahati nzuri na kwenye mapendekezo umeeleza lakini nafuu niseme kwamba mpango unatuelekeza baadae tuweze kupangia bajeti sasa mimi napenda nipendekeze kwamba pamoja kwamba umeweka kwenye vipaumbele kuimarisha miundombinu ya maji kuhakikisha kwamba kila mwananchi anapata maji, kwenye eneo hili niombe Serikali tuwe makini sana lazima tuhakikishe kwamba tuliposema kwamba mwananchi kutafuta maji hatembei mita 400 ziwe mita 400 na kufikia mwaka 2019/2020 asilimia kubwa ya Watanzania wapate maji hilo litakuwa limetusaidia sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti , jambo la pili ameonesha kwamba ataimarisha vituo vya afya, imeoneshwa hapa na mimi nakubaliana na wewe, lakini lazima tuweke mikakati, kuna vituo vya afya ambavyo havijaisha kwa hiyo tuhakikishe kwamba 2019/2020 vile vituo vya afya ambavyo hatujakamilisha vyote tuwe tumeshakamilisha, bahati nzuri sana Serikali imeanza kujenga hata maeneo kuna maeneo kuna Wilaya nyingine zinajengewa hospitali bahati nzuri hata Jimbo la Mufindi Kusini kule tunajenga hospitali/katika Wilaya Mufindi tunajenga hospitali na Serikali imeshatoa shilingi milioni 500 nimefurahi, lakini tuhakikishe kwamba tunaweka mikakati zile fedha ambazo zinatengwa kwa ajili ya kuboresha hospitali mpya zinasimamiwa vizuri, zinatumika vizuri kwa sababu ile ni kodi ya wananchi na kuhakikisha kwamba zile hospitali zinazojengwa zinakuwa nzuri na zinakuwa standard.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna tatizo kubwa sana la watumishi katika hospitali sasa hili lazima liende sambamba, tukimaliza hospitali basi na ajira mpya kwa watumishi hasa wa upande wa afya waweze kuajiriwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna eneo lingine la msingi sana kwa sababu tumesema tunapunguza umaskini sasa nataka niongeee kwenye upande wa REA. REA vijijini niombe Serikali tumeanza vizuri tumalize vizuri tunategemea kufikia mwaka 2020 vile vijiji vyote ambavyo havijapata umeme vimepata umeme vijiji vyote na bahati nzuri Waziri wa Nishati huwa anaongea vizuri sana kwamba kila kitongoji hiyo ni mikakati ya Serikali kwamba kila kijiji kila kitongoji na kila kaya ziweze kupata umeme hiyo ni mipango mizuri na tumeonautekelezaji unafanyika na makandarasi wako site hiyo naipongeza sana Serikali, ila mimi nisisitize tuzidi kuongeza juhudi saa hivi makandarasi hawaendi na speed ile ya mara ya kwanza, wakishaongeza juhudi ya makandarasi kufikia mwaka 2020 vitongoji vyote na vijiji vyote vikiwa vimepta umeme basi umasikini moja kwa moja automatically utakuwa umepungua.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo moja kwa moja ita-connect hata uboreshaji wa uzalishaji wa bidhaa katika viwanda vyetu. Tukitaka kuboresha viwanda lazima tuwe na umeme wa kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimefurahi sana kuona Serikali ina mpango mkubwa na ule umeme wa maji Rufiji wameonesha kwenye mipango tukiwa na umeme wa maji kutoka Rufiji nadhani tutakuwa tumetimiza lengo la kupeleka umeme vijijini kwa sababu tutakuwa tuna miundombinu mingi sana ambayo inaweza ku-connect kila kijiji na kila kitongoji kupewa umeme.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ambalo nilitaka niliongele kwenye elimu, elimu ameongea vizuri Waziri wa Mipango, ameeleza vizuri sana, lakini naomba tuongeze kipengele kingine Serikali iongeze juhudi kwa kujenga hosteli kila shule ya sekondari. Tuna tatizo kubwa ya hosteli kwenye mashule yetu watoto bado wanatembea kilometa mpaka 10 mtoto wa sekondari binti anatembea kilometa 10 na hii inasababishia wanafunzi wengi sana kupata mimba mashuleni. Sasa kwenye mipango yetu niombe Serikali tuhakikishe kila sekondari tunaweza kuijengea hosteli ili watoto wakae bweni, hili litasaidia sana kupunguza matatizo na kuongeza kiwango cha ufaulu kama watoto wetu watakuwa wanakaa hosteli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye elimu tena bado kuna upungufu wa walimu wa sayansi, tuiwekee mikakati kabisa, niliwahi kuongea siku moja nilisema wanafunzi wanaosoma vyuo vikuu wanachukua elimu ya sayansi wapewe mkopo asilimia 100 na hii itasaidia ku-motivate wanafunzi wengi wajiunge na masomo ya sayansi ili tupate walimu wengi tutapata madaktari wengi na hiyo itasaidia na zile maabara ambazo tumejenga kwa sababu Serikali imehamasisha kuna maabara zimejengwa zimeshaisha lakini hakuna wanafunzi wanajitolea kusoma sekondari kwa sababu akienda Chuo Kikuu hapati mkopo asilimia 100. Sasa niombe Serikali kwenye hilo tuiliwekee kwenye mkakati kwenye mpango ionekane kwamba wale wanafunzi wanaojitolea kusoma sayansi wapewe asilimia 100. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala lingine ambalo nimeliona kuwepo kuna upendeleo katika mikopo hasa watoto wa kike, watoto wa kike bado asilimia ile ya kupeleka hizi masomo ya juu bado kwa sababu mkopo hawapewi katika vyuo vikuu, sasa niishauri Serikali katika mipango utoaji wa mikopo mtoto wa kike apendelewe zaidi kuliko mtoto wa kiume kwa sababu mtoto wa kike kwa mfano hajapata mkopo anaanza kufuatilia bodi ya mikopo Dar es Salaama anakaa mwenzi mzima anafuatilia mkopo Dar es Salaama hii imeleta madhara makubwa sana kwa watoto wa kike matokeo yake wanaweza wakajiingiza kwenye mambo mengine ambayo hawakutegemea kwa sababu ya kufuatilia mikopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Serikali ikitoa mikopo kwa watoto wa kike wote hii itakuwa inapunguza hata ile madhara ya kupata mimba mashuleni hii itakuwa imesaidia sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono asilimia 100 mpango huu ambao ni mzuri ahsante sana.