Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kuchangia mchango huu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa najaribu kufikiria na kusoma soma hivi vitabu vya mipango ambavyo tumekuwa tunaletewa hapa kwa muda wa miaka mitatu hivi sasa tangu nimekuwa Mbunge, lakini nimegundua kwamba mipango hi ni mingi sana, lakini siyo tu mingi, mipango hii inahitaji muda sana, lakini mipango hii inahitaji udadavuzi wa kutosha kabisa ili kuweza kutekeleza mipango hii kutokana na intricacies zake zilizopo, Waingereza wanasema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maana yangu ni nini? Kwa sababu Wizara hii imepewa majukumu mengi sana, Wizara ya Fedha kazi yake ni kuleta mipango yote ya fedha, kutengeneza bajeti ya fedha, kuzipa Wizara zote fedha na utekelezaji wake kufuatilia, lakini tumeipa kazoi nyingine ya kutengeneza mipango na kusimamia mipango. Mimi nilikuwa nashauri kwamba mamlaka zinazohusika Serikali itenganishe kuwe na Wizara ya Mipango na kazi yake iwe ni kutunga mipango na kusimamia mipango pekee, lakini kuwe na Wizara ya Fedha lakini kuichanganisha, kuziunganisha kama ilivyo hivi sasa ndiyo maana tunaona baadhi ya maeneo yanasahaulika, baadhi ya mambo ambayo yamepangwa na Serikali yanashindwa kufuatiliwa kwa sababu Wizara hii imepewa jukumu kubwa sana. Nashauri Serikali itenganishe ziwe Wizara mbili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na nilikuwa napitia mpango hapa huu muelekeo wa mpango kwenye changamoto hizi amezungumza Mheshimiwa hapa kwamba miongoni mwa changamoto ni uwezo wa wakandarasi wanaopewa zabuni za ujenzi katika miradi inayofuatiliwa kutokuwa na uwezo wa kutekeleza miradi hiyo kwa wakati uliopangwa kwenye mikataba. Sasa ni jambo la kusikitisha sana kwamba Serikali yenyewe ndiyo inachagua hao wakandarasi, Serikali ndiyo inayofuata taratibu za manunuzi na tukachangua wanunuzi ambao hawa wakandarasi ambao ni best kutokana na Sheria ya Manunuzi lakini mwisho wa siku inafuatiliwa, inaonekana kwamba wale wasimamizi au wale watekelezaji au wale waliopewa zabuni hawana uwezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumze jambo moja hapa, mwaka jana wakati Mheshimiwa Rais amekuja Mtwara kuja kuzindua pale ujenzi wa bandari lakini pia kuweka jiwe la msingi la barabara kutoka Mtwara Mjini mpaka Mnivata kilometa 50, alizungumza wasiwasi wake huu kwamba kuna mkandarasi yule amepewa ujenzi wa barabara ile kutoka Mtwara Mjini mpaka Mnivata kilometa 50 barabara ya uchumi, yule mkandarasi alisema kwamba hana uwezo wa kutosha. Sasa tunashangaa kwamba mtu hana uwezo wa kutosha na anajulikana na Serikali lakini bado anapewa ule mradi kutekeleza, mpaka leo ule muda ambao alipangiwa kumaliza ule mradi, mradi unasuasua mopaka leo ile barabara kilometa 50 tu sasa ni jambo la ajabu sana.

Mimi niishauri Serikali kwamba yale ambayo tumeyaona kwamba ni mapungufu na wale ambao hawafai, wazabuni ambao tumewapa tender hawawezi kusimamia na kutekeleza sawa sawa kwa wakati basi wasipewe hizi kazi ndiyo lengo la Serikali kuliko kuchelewesha kazi tunawapa wale wale ambao tumeona wana makosa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nilikuwa napitia kitabu cha Mheshimiwa Mpango hapa kana kunavyopanga hii mipango tunatakiwa tuangalie usawa wa nchi yetu kwa sababu lengo la nchi hii ni kuondoa umaskini. Sasa tulikuwa kwenye bajeti tunazungumza suala la ujenzi kwa mfano wa viwanja vya ndege na humu kwenye mpango nimeona pia kwamba Serikali imejipanga kukarabati na kuendeleza viwanja vya ndege, sasa naangalia hapa kwenye ukurasa huu wa 30 sioni kiwanja cha ndege cha Kanda ya Kusini ambacho ndiyo chanzo kikuu cha uchumi kwa ndege zetu za Kanda ya Kusini, uwanja wa ndege wa Mtwara hapa haupo wa Kanda ya Kusini sasa ni jambo la ajabu sana tunazungumza maeneo mengine na Kanda zingine zinaachwa kwa makusudi kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na tulizungumza wakati wa bajeti hapa kwamba kiwanja kile kilitengewa shilingi bilioni 54 kwa ajili ya ujenzi lakini humu kwenye mpango hakipo na miradi ambayo inatekelezwa ambayo imepangiwa bajeti tumeiona humu yote ipo imetajwa na Mheshimiwa Waziri wa Mpango. Sasa tunaomba utuambie Mheshimiwa Waziri wa Mpango kwamba tunavyopanga na maeneo mengine tunasahau ama tunayaacha? Badala ya kwenda mbele tunarudisha nyuma, lengo ni nini Mheshimiwa Waziri Mpango?

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine pia ni suala hili la reli ya Ukanda ule wa Kusini wenzangu wamezungumza na ukanda huu wa Kusini Mheshimiwa Akbar kasema kwamba ndiyo ufunguzi wa uchumi na tunapotaka kuondoa umaskini lazima hii nchi tu-decentralise uchumi wetu, tufungue milango yote; reli ya katikati standard gauge ni jambo jema sana, lakini reli ile ya Kusini ambayo iling’olewa miaka ya 1963 na kupelekwa maeneo mengine basi irudishwe sasa ianzie pale Mtwara Mjini, Bandari ya Mtwara ielekee kule isiwe kila mwaka tunaandika kwenye mipango, utekelezaji unakuwa ni mdogo. (Makofi)

Kwa hiyo, nilikuwa naomba sana kwamba ule tunaoita upembuzi yakinifu ule ambao unataka kuanza kutoka Mtwara Mjini mpaka kule Mbambabay, kule Mchuchuma na Ligfanga basi uweze kupelekewa fedha siyo kila mwaka tunaandika kwenye mipango fedha hazipelekwi na utekelezaji unakuwa ni mdogo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo lingine kuna suala la uendelkezaji wa viwanda ili viweze kuleta ajira kubwa sana kwa Watanzania na kuondoa umaskini, lakini jambo la kusikitisha chuma kinapatikana Mchuchuma na Liganga ndipo kwenye chuma pale na chuma ndicho kitatoa material chuma kinapatikana Mchuchuma na Liganga lakini kiwanda cha kutengeneza chuma kinakwenda kuwekwa Moshi, ni jambo la ajabu sana. Serikali hii inatakiwa iangalie kwa sababu tunavyowekeza katika uchumi wetu tunahakikisha ya kwamba tunawekeza kwa gharama nafuu sana sasa unavyotoa chuma kutoka Mchuchuma na Liganga kama huo mradi ukikamilika then ukakipoeleka Moshi kwenye Kiwanda cha Chuma gharama inakuwa ni kubwa sna na inakuwa badala ya kwenda mbele bado utatumia rasilimali kubwa snaa katika kusafirisha material. (Makofi)

Mimi nashauri kwamba kiwanda cha chuma kijengwe kule kule Songea, kule kule Mchuchuma na Liganga ambako ndiko material yale yanatoka kule na tusiende kuweka umbali mrefu kama ilivyokwenye taarifa mbalimbali ambazo tumekuwa tunazisoma za Kamati. Hii itapunguza ile hali ya kuweza kutumia gharama kubwa kwenye kusafirisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nilitaka kuzungumza kwenye mpango hili limezungumzwa suala la afya kwamba Serikali imejipanga na inamkakati wa kurekebisha suala hili la afya nalo pia kama ilivyo kwenye maeneo ya viwanja vya ndege kwamba Mikoa ile ya Kusini ukisoma kwenye taarifa hapa ya Mheshimiwa Mpango kwamba amepanga kuboresha hospitali za rufaa kwenye ukurasa wa 24. Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini haipo, nikiangalia humu hakuna kabisa, haijatengewa hata kuwekwa tu kwenye mpango kwa sababu tunaanza kuweka kwenye mpango halafu tunaingia kwenye bajeti. Sasa Hospitali ya Kanda ya Kusini haipo humu ndani na tumezungumza wakati wa bajeti, tumezungumza miaka yote, kwenye mipango yote iliyopita sasa kama unaondoa kwenye kitabu cha mpango vipi kwenye bajeti inayokuja? Kwahiyo mimi nishauri sana kwenye ukurasa wa 24 ihakikishwe ya kwamba hospitali hizi za Kanda basi ziangaliwe Kanda zote ili Watanzania waweze kuwa na afya bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, nakushukuru.