Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii na mimi niweze kuchangia mpango huu.

Kwanza kabisa nimpongeze Waziri kwa wasilisho lake zuri, kwa kweli mpango tumeupitia, mpango wako ni mzuri kwa sababu umejaribu kupitia tulipotoka tulipo na tunakoenda. Kwa hiyo, nikupongeze kweli kweli na Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi, lakini kipekee naipongeza Kamati yetu ya Bajeti na mimi nipo kwenye Kamati hiyo tumeipitia bajeti yetu, tumetoa maoni yetu kwenye Kamati yetu ya bajeti nafikiri maoni yetu unayo.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mimi sitaki hata kupita sana kwa sababu yote tulishayasema kwenye Kamati na mengine tumekushauri ndani ya Kamati yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kipekee niipongeze Serikali kwa mipangilio ambayo imeshatekelezwa na miradi iliyokwisha tekelezwa ni ukweli usiofichikwa kwamba mmefanya kazi nzuri na miradi hii ni miradi mikubwa ambayo kwa kweli inahitaji kuwa serious ili uweze kui-achieve, kama hautakuwa serious hautaweza ku-achieve kwa sababu inahitaji fedha ngingi. kwa hiyo nakupongeza sana Waziri nampongeza Rais, napongeza na chama changu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukija kwenye mpango wenyewe kwenye sheria pale kwenye Sheria ya PPP. Pale umeandika kwenye page 43 kuna miradi ya maji nayo ambayo inatakiwa kwenda na PPP. Sasa mimi wazo langu ni kwamba ile miradi sasa ambayo ya maji ambayo unataka iende kwa PPP katika ile orodha ya miradi ambayo unataka iweze kuwepo kuwa solicited au iko solicited na Serikali hatujaweza kuipata, ni vizuri kwenye mpango unaokuja tuweze kuona kwenye maji, miradi ya maji ulivyoitaja ukurasa wa 43 ni miradi gani hiyo ili tuweze kuielewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, page ya 47 ya hotuba ya Waziri kuhusu miundombinu amesema tuweze kuunganisha Tanzania na nchi jirani kwa upande wa miundombinu. Wazo langu langu pale sasa Mheshimiwa Waziri kwa sisi ambao tuko mpakani tunaomba kwenye mpango wako utuwekee madaraja kuunganisha nchi na nchi, tunayo matatizo specifically kwenye Jimbo la Mheshimiwa Obama pale tunatenganishwa Burundi na Tanzania na mto ambao sasa ule mto ni mkubwa tunahitaji madaraja. Kwa hiyo katika kupitia page yako ya 45 tunaomba madaraja pale uweze kuyaweka ili angalau iweze ku-facilitate biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wa page 37 ya hotuba yako upande wa kilimo umetaja mambo ya michikichi tungeomba kwa sababu Waziri Mkuu alikuja kwa heshima kubwa sana Mkoa wa Kigoma akawa ameimiza michikichi. Kwa hiyo, tunaomba Wizara ya Kilimo iweze kulichukulia hilo na wewe umeliweka kwenye mpango ili iweze kuwa serious Mkoa wetu wa Kigoma michikichi mbegu na utafiti viweze kuwa vimeimarishwa.(Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ambalo amelisema Ndugu yangu Silinde kwenye hotuba yake ame- challenge sana pale kwenye hotuba yako ukurasa wa 34 aliposema changamoto umezieleza pale, sasa siamini kama mpango wowote ule ambao unaweza ukawa umepita ambao changamoto hazipo. Sasa kutupia tu kwamba changamoto zipo sisi tulitegemea kama Wabunge sasa tutoke pale tumpe mawazo namna ya kwenda kwenye mpango unaokuja. Lakini kusema kwamba changamoto kwenye mpango wowote hamna mimi nafikiri siyo sahihi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine la mwisho ni mifano ambayo sasa tunaanza kuingizia mfano nchi ya Rwanda, sisi ni Wabunge wa Tanzania tuko proud na mambo yetu ya Tanzania. Kusema kwamba Rais Kagame anawashauri wengine nchi za nje siyo sahihi na sina uhakika JPM kama anahitaji washauri kwa sababu kama niwashauri Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi bado yuko hai, Benjamin William Mkapa bado yuko hai, Jakaya Mrisho Kikwete bado tuko hai Chama cha Mapinduzi ambacho ni imara bado kiko hai, Kamati Kuu bado iko iamara Wabunge wa CCM tuko imara, tutaendelea kumshauri tuhakikishe kwamba nchi yetu inaenda vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo naunga mkono hoja.