Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi hii adimu ili na mimi niweze kuchangia na kutoa maoni kwenye Mpango wetu wa Maendeleo kwa mwaka kesho 2019/2020.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpongeza Waziri na timu yake yote. Kwa kweli huu mpango ni mzuri sana, umeangalia vipaumbele vyote muhimu na umetengenezwa kitaalam sana kiasi ambacho hata ukiangalia na maoni ya Kamati nayo yamefanya kazi nzuri sana, yameuchambua vizuri na maoni yake yote naomba niyachukue na mimi labda niongezee pale tu ambapo hayakugusa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika huu mpango wetu ukiangalia vilevile unaangalia tulikotokea, tumefanya nini katika miundombinu, katika kilimo, uvuvi, elimu na kadhalika. Na ukiangalia mwenendo trend inaonesha tumefanya vizuri katika sehemu nyingi, zinaridhisha. Na kwa kujikumbusha tu kwamba bajeti haina maana ya kwamba umepewa license ya kutumia, hapana, ni matarajio, ni mategemeo. Kwa hiyo, kwa kiasi pale ambapo tumefanya vizuri mimi nilikuwa namuomba Waziri aangalie ni namna gani tuweze kuboresha huko nyuma wakati tunaangalia na mipango ya vipaumbele vya sasa hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa tukifanya vizuri sana katika uboreshaji wa bandari, ununuzi wa ndege na ujenzi wa reli. Tumefanya vizuri katika hayo maeneo, lakini mimi naomba tu nipendekeze, kwa sababu kwa Bandari yetu ya Dar es Salaam tu sasa hivi ina ushindani mkubwa sana kutoka kwa majirani zetu, ukanda wa kusini, nchi kama Angola, Namibia na Msumbiji. Hizo nchi zimelilenga soko letu na zimelilenga soko la Bandari ya Dar es Salaam. Sasa je, sisi tumejipanga vipi kupambana na hilo? Kwa sababu huwezi kuzuia watu wasikuingilie kwenye soko lako, wewe ndio unatakiwa ujipange namna ya kujiimarisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa maboresho niliyokuwa napendekeza mimi kwa sababu hili soko bado tunalihitaji sana pamoja na utengenezaji na ujenzi wa standard gauge lakini soko la nchi za DRC, Zambia na Malawi ni soko muhimu sana kwa Bandari yetu ya Dar es Salaam na kwa uchumi wa nchi yetu. Sasa wenzetu wamefanya nini, wamejenga reli ya kutoka Lobito Port, Angola kuja kwenye nchi za DRC na wanazipeleka mpaka kwenye machimbo, reli ambazo ni za kisasa ni standard gauge ambazo zinaweza kuchukua mzigo mkubwa sana na hizo reli vilevile zinalenga kuziunganisha Bandari za Msumbuji lakini na kwa kiasi fulani wanalenga vilevile na kuiunganisha na Bandari yetu ya Dar es Salaam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa angalia nia yao nini hawa; wamepunguza gharama zao kwa kiasi kikubwa, gharama zimekuwa ndogo kiasi wafanyabiashara wote sasa hivi wanaangalia ni namna gani watumie Bandari ya Lobito ambayo ni kilometa 1,300 tu kutoka DRC ukilinganisha na sisi zinakaribia karibu kilometa 2,000.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mapendekezo ya kwangu kwenye mpango wa mwaka kesho, Serikali ilikuwa inafikiria kujenga bandari kavu Mbeya na hiyo bandari kavu ni muhimu kwa vile imekaa mahali kwa kimkakati ambapo inaliangalia soko la Malawi, soko la Zambia na soko la Kongo, lakini kwa miaka miwili sasa hivi Mamlaka ya Bandari haijaruhusiwa kuwalipa fidia wananchi waliotoa maeneo yao kwa ajili ya kujenga bandari kavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa wenzetu malengo yao ni kujenga bandari kavu nyingi kwenye nchi za Namibia – kuna sehemu inaitwa Walvis Bay, Namibia, lakini vilevile na Angola nako wanajenga bandari kavu, ukija Msumbiji nao wamejiimarisha, nao wamejenga reli kutoka kwenye bandari ambayo ni kubwa namba mbili kwa Msumbiji inaitwa Nacala, wamejenga hiyo bandari mpaka nchi ya Malawi na sasa hivi wanalenga kuingia Zambia na wakiishaingia Zambia wanalenga vilevile iende mpaka DRC, sasa ukiangalia sisi tutabaki na nini tusipokwenda kishindani zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo naomba katika huu mpango nimeona kwamba kuna jitihada za kuboresha TAZARA ambazo ni jitihada nzuri, zitasaidia, lakini mkazo uwe hapo; hatutatumia pesa nyingi sana lakini ukiweza kwenda pamoja ku-improve ile mipango ambayo wameshaitekeleza inasaidia vilevile hata kutekeleza mipango inayokuja ya mwakani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye suala la umeme tumefanya vizuri sana, REA inakwenda vizuri na pesa nyingi ambazo kwa kiasi kikubwa ni za ndani zimefanya kazi nzuri sana. Sasa je, katika mpango wetu tutaboresha vipi hii mipango ya umeme vijijini iwe endelevu? Sasa huioni moja kwa moja kama iko kwenye hii mipango kwa sababu bila hivyo kama hakutakuwa na mipango ya kuifanya hii mipango yetu utekelezaji wetu unakuwa endelevu tutakuwa tunapoteza hela bure.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naangalia kwa hizi pesa nyingi tulizotumia, je, zimeigia katika Mfuko wa TANESCO kama capital? Na kama imeingia capital mbona inaonekana ni hela nyingi sana, je, zinaisadia vipi TANESCO kupata faida?

Sasa wakati Waziri anaangalia namna ya kuboresha mapato ya ndani aangalie ni namna gani wakati hizi pesa nyingi tunaweza kwa wakati mwingine tunasahau kwamba pesa zote ambazo tumezitumia kwenye ujenzi wa umeme vijijini (REA) zimehamishiwa TANESCO kama kuziongezea mtaji, je, ule mtaji unatuzalishia kiasi gani? Je, tunaiona hiyo? Ukiangalia vijiji vingi sana sasa hivi vimeongeza wateja kwa TANESCO, je, tuione wapi hiyo faida ya investments ambazo tumeziweka kwenye umeme? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukija kwenye maji vilevile pesa nyingi sana tumezitenga kwa ajili ya miradi ya maji lakini ukirudi nyuma kuangalia ufanisi wa miradi ya maji huwezi kuiona kwa sababu nayo hatukujiwekea mipango endelevu ya hii miradi ya maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana, naunga mkono hoja.