Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya mimi kuweza kuwa na mchango wangu kama Mbunge katika kuishauri Serikali yangu, Serikali ya Chama cha Mapindinzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nianze kwa unyenyekevu mkubwa kabisa kutambua kazi kubwa na commitment kubwa inayofanya na uongozi wetu katika kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi, ikiongozwa na jemedari wetu Dkt. John Joseph Pombe Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, its an disputed kabisa kwamba amesema dada yangu Mheshimiwa Munde, legacy ambayo inakwenda kuandikwa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi ya Awamu ya Tano is an questionable na inakwenda kuonesha vitu ambavyo Taifa litakumbuka vizazi na vizazi.

Mimi nitumie fursa hii kwa dhati ya moyo wangu kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri Mkuu ambaye kwa muda mwingi tumekuwa naye humu Bungeni, tumekuwa tukisema na kupongeza watu wengine lakini tumemsahau kiongozi huyu mkubwa kabisa wa shughuli za Kiserikali Bungeni. (Makofi)

Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa amekuwa akifanya kazi kubwa ya kuhangaika mikoani na kwenye majimbo kupambana na mambo ya kahawa, kupambana na mambo ya korosho, kupambana na mambo ya maji, Mheshimiwa Waziri Mkuu leo mimi kijana wako nataka nitambue kazi yako kubwa unayoifanya katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia nitumie fursa hii kumpongeza sana kaka yangu Dkt. Mpango, the good thing kwa Dkt. Mpango ninachokiona mimi miongoni mwa viongozi wenye msimamo hasa katika sekta na Wizara nyeti kama hii, Dkt. Mpango ninakupongeza. Mimi nimebahatika kufanya kazi na Dkt. Mpango nikiwa Mkuu wa Wilaya ya Igunga, kuna kipindi nilifanya coordination ya kuwa-organize vijana wa vyuo vikuu katika sekta ya kilimo, Dkt. Mpango akiwa anafanya kazi Tume ya Mipango alifunga safari kuja kutembelea miradi ya vijana kwa muda wa siku tatu Igunga na kutoa ushauri. Kwa hiyo Dkt. Mpango mimi ninakupongeza wewe ni mzalendo na kubwa zaidi ni kiongozi usiyeyumba katika masuala ya kodi, hiyo ni sifa kubwa sana kwa kiongozi. (Makofi)

Naomba nijikite katika mchango wangu kwa Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaishauri Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi, kwanza, Rais wetu amekuja na vision akitekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya ku-industrialize nchi, hili nimelisema toka nilipoingia hapa katika Bunge hili kikao cha kwanza kabisa, tunapozungumzia habari ya kutaka ku-industrialize nchi hatuwezi kuacha kuweka connectivity kati ya mambo ya industrialization na masuala mazima ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niishauri Serikali ya Chama cha Mapinduzi, katika sekta ya kilimo mwanzo tulivyoanza nilianza kuona kwamba tunakwenda vizuri, lakini katikati naona kuna mahali tuna-stuck, tulianza kuzungumzia mazao ya kimkakati, Bunge la kwanza nilizungumzia na kaka yangu Dkt. Mpango uko hapa nilizungumzia habari ya wakulima wa pamba wa lake zone, nilizungumzia habari ya wakulima wa mazao ya alizeti katika mikoa ya kanda ya kati na baadhi ya mikoa ya mashariki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilisema Tanzania (Taifa letu) tunapoteza fedha nyingi sana katika kuingiza mafuta kutoka nje ya nchi mafuta ya kula nikasema potential tuliyonayo katika kilimo cha alizeti tukiamua kufanya intensive investment Taifa letu litaondokana na habari ya importation ya mafuta tuta-save foreign currency na tutaweza kuinua uchumi wa nchi. Ninachokisema ni kwamba sijaona connection iliyopo kati ya Viwanda na sekta ya kilimo hasa katika kilimo cha alizeti. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaishauri Serikali, ni wakati muafaka sasa kuhakikisha ya kwamba Serikali inatoa incentive package kwa wakulima wa mazao ya alizeti, kaka yangu Dkt. Mpango lichukue hili na mwakani kwenye bajeti

lilete toeni incentive katika mbegu za alizeti, toeni incentive katika masuala mazima ya pembejeo tuweze ku-boost productivity na kuongeza tija ili Viwanda viweze kupata raw material. Mimi hapa ninapozungumza Jimbo langu linapakana na Jimbo la Iramba, kuna kijana mmoja mjasiriamali amefungua Kiwanda cha Alizeti hapa ninapozungumza amepata market Rwanda, anauza Congo, anauza Zambia…

MHE. MARTHA M. MLATA: Anaitwa Yaza.

MHE. ELIBARIKI I. KINGU: Anaitwa Yaza, ahsante Mheshimiwa Mama Martha Mlata. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo haya tukiweza kufanya Mheshimiwa Waziri tutaweza kulisaidia Taifa hili na tutaweza kutengeneza wajasiriamali wa kati watakaoweza kufanya investment kwa sababu hawa ndio wazawa wenye uchungu na hili Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ushauri wangu ninaoutoa kwa Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi, tunazungumzia suala la viwanda, Rais John Joseph Pombe Magufuli amekuja na ideology ya kutoa elimu bila malipo shule ya msingi, kaka yangu Mheshimiwa Dkt. Mpango uko hapa na mama yangu Mheshimiwa Profesa Ndalichako najua uko hapa ninajua wewe ni mama bingwa ni Waziri uliyeimudu Wizara yako ya Elimu, mimi ninakupongeza sana mama yangu ushauri wangu ninaoutoa, mwakani njooni na mpango wa kuhakikisha vocational education inakwenda kuwa bure kuanzia mwakani, tukifanikiwa kuweka vocational education kuwa bure tutaweza kutengeneza class ya technocrats ambao watakwenda kutumika katika viwanda ambavyo tunampango wa kuhakikisha kwamba Taifa letu linakwenda kuwa Taifa la viwanda. Kama tumeweza kutoa elimu bila malipo kwa shule za msingi Mama Ndalichako ukiwasiliana na Mheshimiwa Dkt. Mpango mkafanya coordination ya kuangalia tuna vyuo vingapi vya ufundi Tanzania, skills zinazohitajika kwa ajili ya kwenda ku-feed watu kwenye viwanda, tukawekeza kwa vijana wetu wa vocational education mimi nataka niwaambie in next ten years viwanda vinavyojengwa hatutategemea technocrats kutoka nje ya nchi tutawatumia wazawa kutoka katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kaka yangu Mheshimiwa Dkt. Mpango huu ndio ushauri wa Kibunge mimi nataka muuchukue achaneni na watu wanaopiga blaa blaa! Watu wanaotaka kutukatisha tamaa, kazi ya Wabunge ni kuja kuishauri Serikali na kutoa mawazo mbadala kwa maslahi ya kuhakikisha Taifa letu linasonga mbele, habari ya kuja hapa kuja kuanza kumtukana Dkt. Mpango sijui mpango umefanyaje. Mimi nataka niwaambie jimbo ninalotoka la Singida Magharibi nimezaliwa kijijini mimi baba yangu alikuwa ni mwalimu for almost 30 years chini ya kipindi hichi nimeshuhudia kwa macho yangu najengewa vituo karibu vinne vya afya on the spot mambo haya hayakuwepo kwani hizi fedha zamani hazikuwepo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapozungumza habari ya kuja uchumi wa nchi ni pamoja na ku-improve social service ku-improve social welfare za watu wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Dkt. Mpango ushauri wangu mwingine ninaoutoa tuiangalie sasa sekta binafsi kwa kuwaangalia entrepreneurs wa Kitanzania tuwaangalia entrepreneurs wa Kitanzania na kuwalinda. Ndugu zangu nataka niwape mfano mdogo kwa nini tunasema kwamba Kenya is one of the largest ten investers kwenye nchi yetu, Kenya ni miongoni mwa mataifa kumi yaliyowekeza Tanzania sana kwa sababu gani wamekuwa wajanja sana wanachukua private sector yenye teknolojia kutoka nje, wanakuja wanazisajili kwao kazi zote zinatoka East Africa wanatokea Kenya wanakuja Tanzania wanachukua kwa sababu wameangalia fursa kwa jicho la pili. Niwashauri Mheshimiwa Dkt. Mpango na timu yako tusi-dicourage private sector kwa maana ya kuwalinda Wazawa wanapokuwa wamebuni na kuanzisha vitu ninaiomba Serikali yangu ya CCM iangalie hili kwa jicho la ukaribu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti tutakapoweza kutengeneza middle class na entrepreneurs ya kwetu hawa ndio watakaokwenda kuwekeza kwenye Viwanda vya korosho tunavyovitaka hawa wahindi wanaokuja Wafanyabiashara tunawapenda hawawezi kuwa na uchungu kwenda kuwekeza kwenye viwanda vya kubangua korosho tukiwezesha middle class ya kwetu, entrepreneurs wa Kitanzania hawa Mheshimiwa Dkt. Mpango wanatakuwa na uchungu viwanda ambavyo Rais Magufuli anavipigia kelele vitafunguliwa ninawashauri kwa dhati ya moyo wangu kila mahali alipo entrepreneur wa Kitanzania tusimvunje moyo, ninawashukuru sana ninajua hili linaeleweka na ninajua mna- take note na ninajua kaka yangu Dkt. Mpango unaelewa mdogo wako ninachokisema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaunga mkono hoja kidumu Chama cha Mapinduzi.