Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili nami niweze kuchangia katika hoja hii ya mpango. Awali ya yote, namshukuru Mungu ambaye ametujalia uhai nami siku hii ya leo kusimama hapa na kuweza kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, nachukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Halima Mdee kwa uwasilishaji mzuri na kwa taarifa nzuri aliyoitoa. Naomba Waziri, Mheshimiwa Dkt. Mpango ayachukue mawazo ya Upinzani, ni mazuri sana, ayafanyie kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nianze kuchangia hoja hii kwa kuanza na sekta ya kilimo. Katika hotuba hii, ukurasa wa 29, imeeleza kwamba kiwango cha ukuaji wa sekta ya kilimo umeongezeka kwa asilimia 7.1 mwaka 2017 ukilinganisha na ile ya 2016 ya 5.6. Suala la kilimo ni changamoto kwa wananchi wetu. Mwaka huu wakulima wengi wamekata tamaa kulima na hasa wa zao la mahindi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli wananchi wetu wamejitahidi wamelima sana na wakapata mazao mengi sana ya mahindi, lakini kihoja kilichopo, sasa hivi wamefungia mahindi yao, yako ndani ya nyumba, panya wanakula, kwa sababu debe moja la mahindi ni Sh.2,500. Huu ni mfano wa eneo moja tu ambako natoka Mkoa wa Njombe. Wananchi wanafika mahali wanashindwa mbolea wanunuaje kwa sababu akiuza mahindi hata debe sita au kumi na kitu bado hawezi kununua hata chakula cha nyumbani. Hata akiuza maroba matano hawezi kununua mbolea au hata sukari kwa hela hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sielewi tutawasaidiaje wananchi hawa. Pendekezo langu, kwa sababu bei ya zao la mahindi na mazao mengine kama mbaazi zimeshuka, basi na bei za pembejeo zishuke kusudi hawa wananchi wapate morali kuweza kulima tena mazao yao na mwakani waweze kuuza kama mtakuwa mmefanya utaratibu wa kuwawezesha kuuza mazao yao kwa bei zinazotakiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kwenye hotuba ya Upinzani, katika mwaka wa fedha 2016/2017, Wizara ya Kilimo iliidhinishiwa fedha za maendeleo shilingi bilioni 100, lakini hadi Machi 2017 fedha zilizotolewa ni shilingi bilioni 2.2. Halikadhalika mwaka 2017/2018, Wizara iliidhinishiwa fedha za maendeleo shilingi bilioni 150.2 lakini hadi mwezi Machi zilikuwa zinatolewa tu shilingi bilioni 16.5. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hali hii tunawezaje kuendelea na mpango huu kama kile ambacho tumepanga mwaka jana na mwaka juzi tumeshindwa kukitekeleza? Naiomba Wizara kufuata haya Waheshimiwa Wabunge tunayoyapendekeza. Tunapoidhinisha bajeti, maana yake ile bajeti itolewe, isiwe tunaidhinisha kwenye makaratasi halafu ukija kwenye hali halisi kiasi kinachotolewa sicho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kwenye suala la maji. Suala la maji nalo ni changamoto kubwa sana katika nchi nzima. Hata leo hii ukizunguka mkoa mmoja hadi mwingine, unaona kwa jinsi gani watu wanavyohangaika na suala la maji. Hata maeneo ambayo yana vyanzo vya maji vya kutosha kama vile Mkoa wa Njombe, bado pale Njombe Mjini hakuna maji. Hilo ni eneo ambalo lina vyanzo vya maji, sembuse maeneo ambayo hayana hata vyanzo vya maji vya kutosha! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri aone ni namna gani zinatengwa fedha za kutosha na kutafuta vyanzo vingine vya kuweza kukidhi haja na hitaji hili la wananchi. Kwa sababu kwanza fedha zinazotengwa ni kidogo sana hivyo wananchi hawa wanashindwa kupata mahitaji ambayo yangetakiwa wayapate. Naomba Mheshimiwa Mpango atenge pesa iende kwenye Wizara husika ya Maji ili iweze kutekeleza miradi yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hilo tu, kuna suala la wataalam wanaokwenda kwenye utekelezaji wa hiyo miradi. Katika Halmashauri nyingi wanapelekwa wataalam ambao wanaenda kuharibu ile miradi, wakishaharibu wanapelekwa sehemu nyingine, baada ya hapo sasa Halmashauri zinaanza kubanwa kwamba mbona miradi haikutekelezeka vizuri. Mfano mzuri ni Njombe, naweza nikatoa hata mfano wa Mradi wa Utengule Ngaranga. Mradi ule umetekelezwa chini ya kiwango. Mabomba hayafai, viungio vinakatika, hadi sasa hivi mradi umekamilika lakini maji hayatoki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kwenye taarifa ya Waziri anasema kwamba miradi ya maji vijijini iliyotekelezwa ni 1,595 na imeshakamilika. Naomba kujua, hii miradi anayosema imetekelezwa, je, imefuatiliwa na kuona inafanya kazi? Nachoomba, tunapoandika taarifa hizi, tuhakikishe tumetembelea na kuona kweli miradi inafanya kazi, ndiyo tuweze kuiingiza hapa kwenye taarifa yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kwenye suala la viwanda. Kwenye taarifa ya Waziri, ukurasa wa 31 amesema viwanda vipya ni zaidi ya 3,306. Naomba kujua, hivyo viwanda ni vya aina gani? Hivyo ni viwanda ambavyo vilikuwa toka kipindi cha Nyerere au?