Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Wilfred Muganyizi Lwakatare

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Bukoba Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. WILFRED M. LWAKATARE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Awali ya yote nitoe pole kwa familia ya Marehemu Mheshimiwa Bilago kwa kuondokewa na mpendwa wao. Pia pole kwa Waheshimiwa Wabunge wote hususan Chama cha CHADEMA. Pia namwomba Mwenyezi Mungu aweze kumsimamia na kuweka mkono wake kwenye operation ya Mheshimiwa Lissu ambayo inasemekana ni ya mwisho ili iweze kufanyika vyema na aweze kupona na kuweza kuungana nasi pia. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hoja zangu ni mbili ambazo nimetumwa na wananchi wa Bukoba Town, ambazo kimsingi zinawagusa Watanzania wote kwa ujumla wao. La kwanza ni suala la property tax. Siku chache zilizopita, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri ambaye ni shemeji yangu, alitoa ufafanuzi mzuri sana kuhusiana na nyumba ambazo zinapaswa kulipa property tax na categories ambazo zimepangwa.

Mheshimiwa Spika, kuna nyumba ambazo kimsingi, kiutaratibu zilipangiwa kulipa Sh.10,000/= ambazo ni nyumba zilizopo kwenye squatters ambazo ni unsurveyed na nyumba za ghorofa ambazo zipo katika maeneo hayo. Nyumba hizi za squatters ni Sh.10,000/= na nyumba za ghorofa ambazo zipo kwenye sehemu ambazo haziko surveyed na wala hazijafanyiwa evaluation ni Sh.50,000/=. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hoja ninayoileta hapa, wananchi wa Bukoba wanaamini wanatapeliwa na TRA, kwa sababu hivi sasa TRA inatoza karibu almost nyumba zaidi ya asilimia 70 za ndani ya Mji wakidai kwamba zimefanyiwa evaluation; wakati utaratibu uliotumika kuzungumzia hicho kiwango ambacho kinasemekana kilifanyiwa evaluation ni kwamba taratibu za Sheria ya Uthamini hazikufuatwa.

Mheshimiwa Spika, kilichotokea ni kwamba ni watu wameunda kikundi wakawaendea wataalam ndani ya Halmashauri husika. Wanakwenda kwenye nyumba mbalimbali, wao wana-dictate terms wana-dictate zile rates kwamba hii nyumba thamani yake shilingi milioni 50, hii ni
shilingi milioni 100 bila kufuata Sheria ya Uthamini. Kwa hiyo, hivi sasa ni disaster na naamini iko katika maeneo mbalimbali ya miji mbalimbali hapa nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, watu wamebambikiwa rates ambazo siyo sawasawa na thamani ya nyumba; na nyumba zenyewe ziko vichochoroni. Mbaya zaidi tunajua Sheria ya Uthamini lazima iwe shirikishi, aidha na Uongozi ulioko katika eneo hilo la mitaa, eneo ambalo watu wenyewe, wahusika wenye nyumba hizo, wanapaswa washirikishwe, wanapaswa wataarifiwe. Sasa watu wamekuwa wanakutana na bili za TRA wakishangaa zinatoka wapi, kwa sababu wakati wa zoezi la evaluation hawakushirikishwa wala hawajui lilifanyika lini? Kwa hiyo, huu mimi naweza nikausema ni utapeli wa hali ya juu na kwa kweli wananchi wa Bukoba Town wamenituma kwamba wanataka maelezo yenye misingi iliyosimamiwa na Sheria ya Tathmini.

Mheshimiwa Spika, vinginevyo, kwa kuwa kule kuna watafiti wengi, hivi sasa zoezi tunalolifanya, tunakusanya data za nyumba ambazo evaluation imefanyika kinyemela na baada ya kukusanya hizo data tutatafuta ushauri wa hatua gani ya kuchukua na hata ikibidi kuipeleka TRA Mahakamani, kusimamisha zoezi hili mara moja kwa sababu halikufuata utaratibu wa kufanya tathmini.

Mheshimiwa Spika, hivi sasa nyumba zinazotozwa hela, unakuta mtu ni mzee kabisa amestaafu, anaambiwa ile nyumba ambayo masikini ameijenga katika mazingira magumu kwa hela ya pensheni mtu anaambiwa atoe Sh.150,000/= kwa mwaka, atazitoa wapi? Kuna nyumba watu wengine wamerithi kutoka kwa wazazi wao ambao wameshafariki, unakuta amebaki mjane, wote hao wanatozwa hela kwa rates ambazo kwa kweli ni unaffordable, hawana uwezo wa kuzilipa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sambamba na majibu aliyoyatoa Mheshimiwa Waziri, namshukuru alitoa majibu ambayo yamesimama vizuri, lakini kwa mazingira ya Bukoba Town ni kwamba lile zoezi la evaluation ambalo wanadai ndiyo linasimamia rates ambazo zinatozwa na TRA, zoezi halikufanyika katika taratibu za kisheria. Namwomba Mheshimiwa Waziri anapo-wind-up azungumzie Bukoba, tutakwenda hivyo au twende na route ya kutafuta haki mbele ya vyombo vingine.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili ambalo kimsingi nalo linalalia huko huko, ni kwamba Mheshimiwa Waziri amekuwa katika takwimu zake na katika vyombo vya Habari na taarifa zinazotolewa na TRA kwamba wanakusanya vizuri, hongera kwa hilo. Kwa mtu anayekusanya vizuri, vilevile kuwepo na vielelezo na taswira na mazingira ya kuonesha anakusanya vizuri lakini pia analipa vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimekuwa katika bajeti ya Wizara kwa kuwa nimo ndani ya Kamati, kwa nini fedha hazitoki? Mbona Wakandarasi wengi wanadai? Mbona Wakandarasi wanasaini mikataba nje ya wakati? Naomba kabisa Mheshimiwa Mpango, asione haya, pesa inakwenda wapi? Nieleze linalozungumzwa, mimi sina minong’ono, wanasema yeye anabana mno, mpaka penalty. Pesa hazitoki. Zina mlango mmoja wa kuingia, lakini wa kutoka ni mwembamba kama ule tunaoambiwa wa kwenda Mbinguni. Kwa nini pesa haitoki? (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Spika, nilifikiria labda hapa tukiwa pamoja na Kambi ya Upinzani na wenzetu wa CCM, kama anatuonea haya, hebu wakiwa kwenye caucus huko wazungumze, wanong’one, kwa nini pesa haitoki? Kwa hiyo, maendeleo ambayo tutaendelea kuyazungumza kimsingi yanakuwa ni maendeleo ya vitu, siyo ya watu. Watu wamechacha ile mbaya, maisha hayatamaniki.

Mheshimiwa Spika, kuna watu wanakula mlo mmoja pamoja na kwamba wengine hawakufunga Ramadhani, lakini inabidi wafunge kwa sababu hela haiko katika mzunguko. Watu wa Bukoba wanauliza hela iko wapi? Hela nyingi inayokusanywa, inakwenda wapi? Naomba atupe majibu hapa. Kama ataona hapa kuna soo, wakikutana huko, najua caucus watakutana, hebu awaeleze Wabunge wenzetu wa CCM hela inakwenda wapi? Mbona matatizo! (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili sambamba na hilo kuhusu madeni, nawazungumzia wapiga kura…

TAARIFA . . .

MHE. WILFRED M. LWAKATARE: Mheshimiwa Spika, nimepokea na kukupongeza kwa hilo.

Mheshimiwa Spika, nazungumzia specifically madeni ya Wakandarasi wa Mji wa Bukoba na Mkoa wa Kagera ambao wamenituma. Tunazungumzia kwa mfano, Wakandarasi wa Mradi wa REA ambao tunaambiwa mpaka leo wanadai. Kimsingi, bahati nzuri wale Wakandarasi wakubwa wana watu wa kuwazungumzia. Nataka kuzungumzia kwenye local content, niite local content basi ya miradi hii, kwamba kuna ma-supplier wadogo wadogo ambao wanakuwa wanawa-supply hawa Wakandarasi wanaowadai. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nina ma-supplier zaidi ya 20 hapa ambao wamem-supply contractor aliyekuwa anasimamia na kuendesha mradi wa REA katika Mkoa wa Kagera. Hawa watu wanadai zaidi ya Sh.1,300,000,000/= hawajalipwa. Wengine majuzi Benki zimetangaza kuwafilisi na kunadisha nyumba zao. Kuna mama mmoja alikuwa ana-supply vyakula kwa wafanyakazi wa Kampuni hii, yule mama ameukimbia mkoa kwa sababu ya madeni. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nataka watueleze haya madeni yanalipwa lini? Kwa sababu yasipolipwa yana-affect hata wengine ambao wapo chini wanao-supply vitu mbalimbali kwa hawa Wakandarasi. Kuna bwana mmoja ambaye mpaka katika kituo chake cha mafuta ameshindwa kununua mafuta mengine kwa sababu alikuwa supplier wa huyu Mkandarasi, anadai mamilioni ya hela.

Mheshimiwa Spika, naomba Mheshimiwa Waziri anapo-wind-up atueleze kwa sababu haya madeni hayawa- affect hawa Wakandarasi wakubwa tu, yanawa-affect hata ma-supplier wadogo ambao kimsingi ndio wapo wengi kule chini. Ndiyo maana circulation ya hela inakuwa haipo na watu wanaishia kwenye umaskini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala la tatu ambalo naomba Mheshimiwa alifafanue, ni hiki kitu ambacho kinaitwa uhakiki. Nashangaa na nitaomba kwa kweli nipewe tuition kidogo.