Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

Hon. Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, naanza kwa kuipongeza hotuba ya Waziri wa Madini. Pia nwapongeza Waziri na Naibu wote wa Wizara ya Madini.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kutoa ushauri wangu kidogo kuhusiana na upotevu mkubwa wa mapato yatokanayo na madini ya dhahabu. Mfano, kuna wachimbaji wadogo Wilayani Nyang’hwale ambao wanachimba na kupata dhahabu bila ya kulipa mapato ya Serikali. Sababu kuu ni kutowapatia leseni ya uchimbaji au kutowatambua lakini yako maeneo mengi yanayochimbwa kama Kijiji cha Chibaranga, Ifugandi, Bululu, Isonda, Nundu, Nyamalapa, Iyenze, Ujulu, Isekelinyugwa, Nyijundu na kadhalika.

Mheshimiwa Naibu Spika, ombi langu, kwa kuwa Wilaya ya Nyang’hwale haina maeneo yaliyopimwa kwa ajili ya wachimbaji wadogo. Maeneo niliyoyataja yapimwe na kutolewa leseni ili Serikali iweze kukusanya mapato kirahisi pia kuwaepusha wachimbaji kusumbuliwa na kuhamahama.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.