Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

Hon. Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa jinsi anavyoiongoza nchi yetu na kwa hatua kubwa aliyoifanya katika kurekebisha mifumo mingi ya Wizara hii na sekta ya madini kwa ujumla.

Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Waziri wetu wa Madini na Naibu wake wote wawili kwa jinsi wanavyotendea haki nafasi zao pamoja na watendaji wote wa Wizara.

Mheshimiwa Naibu Spika, mchango wangu kwa Wizara hii ni kama ifuatavyo:-

(a) Tunaomba sana Serikali itazame upya mikataba ya uchimbaji wa madini kote nchini ili kuona ni kwa namna gani nchi yetu inanufaika kupitia rasilimali hii ya asili kutoka kwa Mungu.

(b) Serikali itazame mpango wa kuwasomesha wataalam wabobezi wa sekta hii.

(c) Serikali ifanye mpango wa kutumia wataalam watakaobaini maeneo yalipo madini nchini hasa katika maeneo ya wachimbaji wadogo kote nchini.

(d) Kwa kuwa wachimbaji wadogo kwa sasa wanachimba kwa kubahatisha basi Serikali yetu itumie wataalam wake ili kurahisishia wachimbaji hao wadogo nchini kutumia njia bora.

(e) Kwa kuwa maeneo mengi nchini yanasemekana kuwa na leseni na kwa kuwa maeneo hayo yanashikiliwa na watu hao ambao hawachangii Taifa letu mapato ya uhakika basi Serikali ifanye mapitio au tathmini ili kuona njia bora na zenye manufaa katika kurekebisha suala hili.

(f) Nimuombe Mheshimiwa Waziri afanye ziara katika Jimbo la Mbulu Mjini kwenye machimbo ya Tsawa, Kata ya Gehandu, Mbulu Mjini.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho natanguliza shukurani zangu na naunga mkono hoja kwa asilimia 100.