Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichangie katika hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu madini Mchuchuma, ni muda mrefu sasa mradi huu wa makaa ya mawe huko Mchuchuma Serikali imekuwa ikiahidi kuanza lakini bado haujaanza. Nataka kujua ni kwa nini ahadi hizi za Serikali hazitekelezeki miaka nenda rudi. Naomba Waziri atakapotoa majumuisho atueleze kwa uhakika ni lini mradi huo wa uchimbaji wa makaa ya mawe ya Liganga na Mchuchuma utaanza.

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa maeneo ya Mchuchuma na Liganga wameondolewa lakini bado hawajalipwa fidia zao. Naomba Waziri atueleze kwa uhakikia ni lini wananchi hao watalipwa fidia zao?

Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wanaosafirisha kokoto, matofali na mchanga wanasumbuliwa sana na kodi nyingi wakati vifaa hivyo ni vya kuwasaidia wananchi ili wajenge nyumba bora lakini wanabanwa sana na watu wa madini. Naomba kodi zisizo na tija zipunguzwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba wachimbaji wadogo wapewe leseni ili waweze kujipatia kipato halali, hasa wachimbaji wadogo wadogo wa Liganga na Mchuchuma.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa wachimbaji wadogo wadogo hawana mitaji, Serikali itoe ruzuku kwa wachimbaji hawa ili wachimbe kwa tija na kuweza kuleta maendeleo ya nchi hii, tofauti na wachimbaji wakubwa wanaonufaisha nje.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.