Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze mchango wangu kwa kumwomba Waziri aje Wilayani Liwale ili kutatua migogoro kwenye Wilaya ya Liwale. Kuna mgogoro wa muda mrefu katika Kijiji cha Kikulyungu na Hifadhi ya Selous. Pia kuna mgogoro kati ya Kilwa na Liwale migogoro hii miwili imeshindikana kwenye ngazi zote, hivyo kuhitaji ngazi ya Wizara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Kanda ya Mtwara ni sehemu ya tatizo katika Halmashauri ya Liwale, kwani imekuwa ikisababisha migogoro badala ya kutatua migogoro. Mfano, Halmashauri ya Liwale imeingia mgogoro na mwananchi baada ya Halmashauri kupima shamba la mwananchi huyo, shamba ambalo lina Hati Miliki ya miaka 99.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri wamepima viwanja bila ridhaa ya mwenye shamba, Kamishna wa Ardhi anajua mgogoro huu lakini hadi leo hakuna hatua iliyochukuliwa. Pamoja na Halmashauri kuvunja sheria ya kupima kwenye ardhi ya mtu inayomilikiwa kihalali, mwananchi huyu ni Ndugu Hemedi Mewile katika Kijiji cha Mangando Wilayani Liwale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua vigezo vinavyotumika na Shirika la Nyumba la Taifa kujenga nyumba za bei nafuu katika maeneo mbalimbali nchini. Kwani mimi kwenye Halmashauri yangu ya Liwale kuna uhitaji mkubwa sana wa nyumba hizo hasa kwa wakati huu wa mazao ya korosho na ufuta kufanya vizuri. Ni lini Shirika hili litakuja Liwale kujenga nyumba hizi za bei nafuu? Ukizingatia kutokana na shida ya usafiri, hivyo vifaa vya ujenzi ni ghali sana na kufanya wakazi wengi wa Liwale kushindwa kumudu kujenga nyumba bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Msitu wa Nyera-Kipelele umechukua vijiji vingi sana, naomba Serikali kuangalia upya mipaka ya Msitu huu ili wanavijiji wanaozunguka Msitu huu wapate maeneo ya kulima na shughuli nyingine. Mfano, Kijiji cha Kiangara, Kipelele, Naujomba, Miruwi, Mtawatawa na Kitogoro, vijiji hivi havina misitu kabisa kwa shughuli za ujenzi kwani sehemu zote zinamilikiwa na Hifadhi ya Msitu wa Nyera-Kipelele.