Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wapima Ardhi Binafsi. Nipende kushauri Serikali kutambua kazi kubwa inayofanywa na sekta binafsi ya uendelezaji wa ardhi kwa kupima na kusaidia uendelezaji wa ardhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe Serikali kuwaondolea VAT katika malipo yao au kodi ambayo itafanya kuongeza gharama kwa wananchi wanaohitaji kupimiwa ili kufanya kazi ya kupanga miji yetu na vijiji kufanyika kwa haraka ili kuokoa janga la ujenzi holela.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wapimaji binafsi wameongeza kasi ya upangaji miji kutokana na Serikali kutokuwa na wafanyakazi wataalam wa kutosha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mgawanyo wa Ardhi. Nishauri Serikali kuhakikisha kuwa inatenga ardhi kutokana na uhitaji mbalimbali. Kwa mfano, ardhi kwa ajili ya wafugaji; ieleweke kwamba kila mkoa, wilaya, kata zinatenga maeneo ya wafugaji na wakulima ili kuondoa migogoro inayopelekea wananchi kuuana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nishauri Serikali kuangalia upya juu ya hifadhi za wanyama au maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya misitu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali ifuatilie migogoro inayoendelea kati ya wananchi na Hifadhi za Taifa ili kujiridhisha mipaka ya awali badala ya kuwachomea wananchi nyumba zao na kuwanyang’anya mifugo yao au kupiga risasi mifugo ya wananchi, jambo ambalo limezalisha chuki baina ya wananchi na wahifadhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Gharama za Upangaji Ardhi na Malipo ya Majengo. Niishauri Serikali kuliangalia hili kwani limekuwa kikwazo kikubwa kwa wananchi. Mwananchi analipia ada ya kiwanja kila mwaka halafu analipia kodi ya jengo ambapo pia amelipa kodi wakati wa kununua vifaa vya ujenzi, hivyo mwananchi kuona kuwa na ardhi au kujenga nyumba ni kosa kwani kodi nyingi zinamfuata mwananchi huyu. Naishauri Serikali kuchagua kodi mojawapo ilipwe ili kuwapunguzia misururu ya kodi iliyopo sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hati za Kimila Kutotambuliwa Kisheria. Niishauri Serikali kuliangalia hili kwani hati za kimila hazitambuliwi mara mwananchi ahitajipo mkopo benki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Maeneo yasiyoendelezwa yarudishwe kwa wananchi au kupangiwa matumizi mengine. Nishauri Serikali maeneo ambayo hayatumiki mfano eneo kubwa la Shirika la Elimu Kibaha ambalo limekuwa pori na kusababisha mauaji na ubakaji mkubwa. Niombe Shirika la Elimu Kibaha kuchunguzwa.