Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Yussuf Haji Khamis

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Nungwi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. YUSSUF HAJI KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema ya uhai na afya njema. Nakushukuru wewe na mimi kwa kupata fursa nichangie ingawa kwa uchache.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu ina migogoro mikubwa ya ardhi katika sehemu mbalimbali, kwa kiasi kikubwa migogoro hii inarudisha nyuma maendeleo ya nchi yetu. Tanzania ya viwanda itakuwa ni ndoto kama hatutaweza kupima ardhi na tukatenga maeneo kwa shughuli mbalimbali za kilimo, ufugaji, viwanda na makazi ya binadamu na tukiweza kufikia katika hatua hiyo, kwa kiasi kikubwa tutapunguza migogoro isiyo ya lazima na kufikia malengo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Ardhi ni muhimu sana katika kufikia malengo makubwa ya kimaendeleo Kitaifa. Napendekeza Wizara hii ipewe kipaumbele kwa kutengewa bajeti ya kutosha kukidhi mahitaji ya mipango ya Wizara. Naomba Wizara iendelee kushirikiana na wadau mbalimbali katika kutekeleza mipango yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie kuhusu umiliki wa ardhi. Sheria za Ardhi zinatambua haki sawa, umiliki wa ardhi kati ya mwanamke na mwanaume. Hata hivyo uhalisia ni tofauti, kwani mila na desturi zilizopo nchini, nyingi hazitambui usawa huu hasa katika haki ya kurithi ardhi. Pamoja na wanawake kuwa zaidi ya asilimia 50 ya idadi ya watu wote nchini, pia wanawake wanazalisha kati ya asilimia 60 hadi asilimia 80 ya chakula tunachokula ukanda wa Jangwa la Sahara. Tafiti nyingi zinaonesha wanawake asilimia 20 ndio wamiliki ardhi Kusini mwa Jangwa la Sahara. Hali hii kwa kiasi kikubwa inachangia wanawake kuwa maskini, kunyanyaswa na kudhalilishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, usawa wa umiliki ardhi na urithi wa ardhi upo kisheria kati ya wanawake na wanaume, naomba Wizara isimamie usawa huu kwa ukamilifu hasa vijijini. Wizara ipige vita mila na desturi zenye kukandamiza wanawake katika urithi wa ardhi na umiliki.